Rais aagiza gereza la Songwe lihamishwe ili kuchimbwa madini ya bati

Ni athari za ukoloni mkuu, unajua India inasifika duniani kwa uuzaji wa vito vya Tanzanite na hawachimbi Tanzanite kule, sehemu nyingine utakuta matajiri wa Tanzanite dunia hii ni Toronto, inahuzunisha sana

Serikali ina uwezo kabisa wa ku-control haya madini, na hata kuwa wanunuzi wa haya madini na kutengeneza products.

Ten percent wapate wapi??

Nafikiri kuna haja ile sera ya majimbo ya CHADEMA kuwa applied , kama hawa jamaa watashika nchi.

Naamini mikoani kuna watu wenye akili zao ambao wanaweza ku-control madini kama wakipewa chance
Mkuu wangu muuzaji mkubwa wa Tanzanite Toronto ni Mhindi Mtanzania ambaye ana duka pia mjini Arusha. Hivyo sielewi mapatano yake na serikali yetu isije kuwa serikali yetu imemtumia mtu huyu kuanzisha biashara hii huko Canada kwa faida ya taifa letu hii poa kabisa na mdio maana nikasisitiza sana serikali yetu iwatumie Diaspora..
Kinyume cha hapo na navyoifahamu Nchi yangu, kina Richmond ni wengi sana....
 
Mimi nauliza kwamba JK aliondoka kwenda Mbeya akisema ziara kumbe ana lake jambo . Je ndilo hilo tu kuubw alilimpeleka kuwaha kikishia wazungu kwamba nitaenda na kutolea tamko huko ?

Jamani udhalilishwaji utamkwe wazi maana jamaa wana dhalilisha mno watu wetu .

Nilikua najiuliza kulikoni JK kwa Mwandosya anafuata nini!!? Kumbe ni geresha ana lake jambo.

Cha kushangaza huo mchanganua yakinifu umefanyika lini hata kufikia maamuzi ya kuhamisha gereza?
 
siku moja mtakuta nchi nzima mnatakiwa kuhama ili kuwapisha wawekezaji!

Mkuu huo ni ukweli na wala siku hiyo haiko mbali. Yamewakuta wamasai Loliona tumekaa kimya, Wasukuma shinyanga walifukiwa kwenye machimbo tukaona hayatuhusu kwa hiyo inaweza kumkuta yeyote kimya kimya hadi nchi nzima.

Sasa tufanye nini???
 
Ni kweli pale ikulu pana Uranium ndio maana ikajengwa pale na mkoloni ili ifichwe.Hata hilo gereza huko songwe kajenga Jeremani.
 
Hivi Rizwani huwa anamshauri nini baba yake kama mtoto wa rais nadhani unajukumu la kumshauri mzee, huyu jamaa huwa anamshauri nini mzee wake.

Wajukuu wa Rizwani watasoma shule gani, watakwenda kupata matibabu hospital gani, watarithi nini kutoka katika taifa letu hili?..
 
Hivi haya madini ya Aluminium yanategemewa kuanza kuchimbwa lini? How are we going to smelt maana refining Aluminium requires alot of energy supply. Smelters zake ndani ya Africa nasikia ziko Mozambique pale kwenye project inaitwa Mozal na pengine South Africa ingawa haya madini yanapatikana kwa wingi barani humu.
Mbona sisi umeme wa kuwashia taa unatusumbua, huu wa kuyeyusha aluminium tutaupata wapi?
Vinginevyo bado ni hadithi zile zile tulizozoea. Kwangu mimi it could make sense tu support refining ya Nickel inayotaka kuchimbwa Kabanga maana karibu kila kitu kimekamilika upande wa exploration and feasibility study. The only big puzzle to the investor is how to get reliable power supply. Using diesel or HFO generators could inflate the production cost unnecessarily, achilia mbali gharama za usafirishaji paka bandarini Dar.
 
Kwa viongozi kama tulionao Tanzania kuamisha gereza kupisha uwekezaji si jambo gumu kwao ilimradi tu wanapata percent yao. Wako radhi kuwaamisha watu bila kujali wanaadhirika au la. Kama wanauwezo wa kuwakingia kifua mafisadi wa EPA na makampuni yaliyo husika,kuwakana wananchi wa Loliondo kuwa si watanzania bali wakenya, Wananchi wengi wanaoadhirika kwa maji yenye sumu yanayotoka kwenye migodi ya dhaabu na maovu mengine mengi yanayoteka lakini serikali haichukui hatua,na kama walisha ahi kusema ni heri wat wale majani ili ndege na rada vinunuliwe, itakuwa ilo la kuamisha gereza?
Mimi naona hilo kwao ni kitu kidogo sana kutolea maamuzi.
 
RAIS AAGIZA.....
siipendi sana hii heading. nadhani kuna haja ya msukumo wa kupunguza madaraka ya raisi ili kuwepo na collective reqponsibility na best perfKwani maagizo yake mengi sidhani ni kwa ajili ya public interest siku hizi. ni kwa ajili ya wawekezaji. Inabidi wataalam wakae kumsaidia na kumshauri kuhusu faida na hasara za miradi aina hii. na pia inabidi awatumie sana wataalam badala ya kutoa maagizo (amri) kila kukicha. Je rais hajui kwamba tupo ktk zama za demokrasia (ya kuhoji kila tamko) na si zama za zidumu fikra...?
 
Si unajua tena kuwa viongozi wetu wamewekwa mfukoni na wawekezaji? Wao wameigia madarakani kwa msaada wa hao wawekezaji fisadi na ni lazima awatetee la sivyo atakosa kiti bwana.
 
Back
Top Bottom