Sheria ya Ardhi namba 4 ya 1999. 2)
Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 ya 1999.3)
Sheria ya Mahakama za Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi namba 2 ya 2002.4) Marekebisho ya sheria ya Ardhi namba 2 ya 2004.5) Marekebisho ya sheria namba 11 ya 2005 sehemu ya nne.
Sheria ya Ardhi namba 4 na Sheria ya Ardhi ya Vijiji namba 5 zilipitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 1999 na kuanza kutumika rasmi mwezi Mei mwaka 2001.
Sheria ya Mahakama za utatuzi wa migogoro ya ardhi ilipitishwa mwaka 2002 na kuanza kutumika rasmi mwezi Oktoba 2003.
Misingi Mikuu ya Sheria Hizi ni:• Ardhi ni mali ya umma na imekabidhiwa kwa Rais kwa niaba ya Watanzania wote.
Naona utata hapo............
jana nimesikia taarifa ya habari watu wamevamia mashamba/misitu na kuanza kufyeka wakisema wao hawana sehemu za kulima wala kupata kipato wala kuishi na hawana hata uwezo wa kununua ardhi hivyo wameona wajichukulia, it is a very very good step in this country because for sure we will get to the bottom of all the nonsense about investors. eti wawekezaji sasa ngoja tu waendelee kununua maeneo kupewa hakuna shida lazima maskini na tajiri watagawana tu hapo mbele na hii itachochewa na huku kutokunufaika na chochote. hii nchi imenichosha kwa kweli maana sijui maono yetu ni nini?vipaumbele vyetu ni nini?mijitu inakula haiwazi hata wajukuu zao wataishi vipi kama si laana ni nini?
mgeni njoo mwenyeji anyongwe!
Tanzana ni nchi pekee ambayo mwekezaji anaonekana ni wa muhimu kuliko raia wake...
ndio maana huwezi kushangaa ukiona polisi wakitumika kulazimisha raia kupisha eneo wnalokaa ili tu kumfurahisha mwekezaji..
haya mambo yamekuwepo siku nyingi. Wewe jiulize wenyeji waliokuwepo mitaa ya posta mpya walienda wapi na walifidiwa vipi baada ya serikali ya mkoloni kutwaa hilo eneo kwa ajili ya kuliendeleza. Au jiulize wale wenyeji asilia wa bukoba mjini waliokuwa na mashamba yao ulipo uwanja wa mpira wa kaitaba walielekea wapi na walifidiwa vipi baada ya hilo eneo kuporwa kwa ajili ya kujenga uwanja? Je wana hisa kwenye huo uwanja au kwenye vitega uchumi vilivyoanzishwa maeneo waliyokuwepo kabla? Tatizo nadhani siyo watu kuhamishwa ila ni jinsi nzuri ya kuwaandalia malipo stahiki yatakayowawezesha kuendelea na maisha huko waendako. Hii haijalishi kabila, rangi, uraia wala dini ya mununuaji wote wanatakiwa kulipa fidia stahiki kwa wenyeji asilia.
Sasa tuziangilieje ndugu yangu, sababu hata tukipiga kelele na watawala wakaamua kuturidhisha kwa kuanzisha mchakato wa kuzibadilisha huo mchakato utapoanzia mpaka utakapoishia sisi hatutashiriki sana sana tutakuwa hapa JF kujifahamishana namna wabunge wanavyochangia kwenye mswada wa mabadiriko ya ardhi bla bla bla bla bla.
Mimi nadhani tuangalie kama ni feasible economically kuwa tunapiga kura kuridhia ama kutoridhia sheria fulani fulani kisha rais atazisign kwa niaba yetu, ama sivyo kwa umbumbu walionao viongozi na watawala wetu wanaweza kuishia kubadirisha lugha tu basi, nakumbuka mwaka jana kuna mtawala kutoka wizara ya ustawi wa jamii kama sikosei akiwa kwenye kongamano la wazee alisema serikali inasubiri africa kusini wamalize mchakato wa kutengeneza sheria ya mafao kwa wazee ili waitumie kutengeneza yetu, nilikuwa na katoto kangu tunaangalia TV ilibidi niizime haraka sana kasielewe yule jamaa alikuwa anamaanisha nini.
Pia, jana nilikuwa napitia sheria za kodi za Kenya na Uganda nimekuta zote zinafanana na yakwetu, nikabaki najiuliza inamaana sheria yetu ya kodi wakati inakopiwa kutoka kenya au uganda au kokote kule hao wacopiji hawakukumbuka kwamba tuna assets za kuwa na tax treatments na political tax motives tofauti kabisa na za kenya pamoja na uganda?
Ninaimani kubwa sana, hata kwenye sheria ya ardhi kama itafanyiwa mabadiriko makubwa haitatofautiana na ile iliyopo kenya na huo ndio utakuwa mwanzo wa kutuingiza kwenye matatizo ya ardhi kama ya uko.Last edited by Sangarara; Yesterday at 12:31.
[MENTION]Unaweza kutafsiri hivyo, kwani amekabidhiwa kwa mamlaka ya umma, huo umma ni kina nani? na je wakati wanapotwaa ardhi kwa manufaa ya umma huo umma unashirikishwa vipi kwenye hayo "manufaa"
Kama alivyosema Rutashubanyuma kunahitajika mabadiliko kwenye hizi sheria, tuangalie upya hizi sheria za umiliki wa ardhi
[MENTION]Unamaanisha kwamba, uonevu wote unaofanywa kwa kuhamisha wananchi kutoka kwenye makazi yao huwa yana approval ya president?
Mamzalendo it is not a good step at all.......kwa sababu hao kulingana na shgeria zilizopo watatambuliwa kama wavamizi na siku mwekezaji njaa akijitokeza na "vijisenti" watatimuliwa tena kwa FFU..tunahitaji sheria za kuwalinda kuvamia ardhi ambayo haitumiki hata kama mmiliki yupo ila kashindwa kuiendeleza..............
[MENTION]my dear friend watu wakikaa kusubiri sheria zirekebishwe nchi hii watakesha na zitarekebishwa kufit hao wakubwa tu hivyo nafikiri wakifanya hivi sehemu kama tano especially arusha lazima serikali itaamka japo kidogo ingawa pia inaweza isishtuke ukiona nchi madaktari wanagoma na watu wanaokereka ni wachache wale wenye wagonjwa basi ni zaidi ya tatizo, sheria zilizopo zenyewe hakuna anayezifuatilia hata ukiweka za kuwalinda hazitafuatiliwa. hivi what is emergency in this country kifo cha kiongozi?vifo vya wananchi serikali inaona poa tu eh?
Bishop Hiluka kukaa kwetu kimya kunachangia tuendelee kunyanyasika...........
Rutashubanyuma ni kweli kukaa kimya kunachangiaq tatizo,
lakini pia kimya hiki hakimaanishi kuwa tumeridhika, tuukubali
ukweli na tuamue sasa...
ukombozi uko mikononi mwa mtanzania mwenyewe, la sivyo hawa viongozi walafi wakishapata 10% zao wananchi watanyang'anywa mpaka kile kidogo walichonacho...