nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Waandishi Wetu
3 Aug 2011
Toleo na 197
KILE kilichoelezwa kuwa kilikuwa ni siri kati ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Pius Msekwa na watuhumiwa waliotakiwa kujitoa ndani ya uongozi, zimeanikwa katika kikao cha Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu ya chama hicho (NEC) kilichowajadili mwishoni mwa wiki.
Mbali ya kubainishwa kwa siri za kikao cha faragha kati ya Msekwa na watuhumiwa hao, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, aliipa meno zaidi Sekretarieti ya chama hicho kwa kupuuza maneno ya baadhi ya wanaosema kwamba inakivuruga chama hicho tawala.
Watuhumiwa hao, Mbunge wa Igunga Rostam Aziz, ambaye tayari amejitoa na wenzake; Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa na Andrew Chenge ambaye ni Mbunge wa Bariadi Magharibi, walikutana na Msekwa kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam na kati yao hakuna aliyekuwa tayari kuzungumzia kilichozungumzwa.
Ni Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Kikwete, ambaye alitoa siri hiyo katika kikao cha Kamati Kuu alipotuliza baadhi ya wajumbe wa kikao hicho cha juu cha chama hicho waliotaka watuhumiwa hao watimuliwe mara moja.
Kikwete alitoa siri hiyo akimtuliza Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais mstaafu, Mzee John Malecela, aliyeonekana kikaoni kuanza kufanikiwa kushawishi wajumbe kushinikiza Kamati Kuu iwafukuze moja kwa moja, akina Lowassa na Chenge, kabla kikao kijacho cha Halmashauri Kuu. Kikwete awaokoa kina Lowassa
Kwa mujibu wa mtoa taarifa wetu, Kikwete, akionekana kama kusoma nyuso za wajumbe, alieleza kuwa ni busara zaidi kusimamia uamuzi wa NEC uliowapa muda wa kujivua gamba watu hao kuwa mwisho ni kikao kijacho cha Halmashauri hiyo Kuu.
Katika kile kinachoweza kuelezwa kuwa kufichuka kwa sehemu ya siri ya Msekwa moyoni, Kikwete alimgeukia Msekwa akiuliza; hivi si walikwambia wanaomba muda wa kutafakari? Naye msekwa alijibu ndiyo.
Kilichokuwa kikirejewa na Kikwete katika swali lake kwa Msekwa ni kilichojadiliwa kwenye kikao kati ya Makamu huyo Mwenyekiti na Lowassa, Chenge na Rostam ambao alikutana nao kwa nyakati tofauti katika ofisi ndogo za CCM, Lumumba Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa maelezo hayo ya Msekwa, imebainika kuwa katika mazungumzo ya faragha, Lowassa, Chenge na Rostam walipobanwa waliomba muda zaidi wa kutafakari kabla ya muda wa mwisho waliopewa kufika.
Katika hilo, Kikwete anatajwa kuwashawishi wajumbe kuwapa muda zaidi kama ilivyokubaliwa faragha, na wasipoamua kama mwenzao Rostam, hatua nyingine zitafuata.
Tayari baadhi ya wajumbe walionekana kukubaliana na uamuzi wa kuwatimua wanasiasa hao wawili waliogoma kujitoa hadi sasa baada ya mwenzao Rostam Aziz kufanya uamuzi mgumu wa kuachia nafasi zote ikiwamo ubunge, kabla ya Rais Kikwete kuokoa jahazi.
Chenge, Lowassa bado hawajaamua
Baada ya kimya cha muda mrefu, Chenge ameibukia mjini Dodoma akichangia bajeti ya Wizara ya Ujenzi, alipowataka wapiga kura wake kupuuza yale aliyoyaita maneno ya mitaani kumhusu, akizima tetesi za hivi karibuni kwamba alikwishajiondoa katika nafasi zake za uongozi kutekeleza maamuzi ya kikao cha NEC kilichopita.
Kwa upande wake, Lowassa amekuwa akitoa matamshi ya chini chini kuonyesha kutokuwa tayari kujitoa; huku akiahidi kutoa tamko rasmi wakati mwafaka utakapowadia, baadhi ya watu wakitabiri kishindo kutoka kwa mwanasiasa huyo anayetajwa sana kuwania nafasi ya urais kumrithi Kikwete mwaka 2015.
Kikwete aipa nguvu Sekretariati mpya
Katika kikao hicho cha CC, Rais Kikwete alirudia kuipa nguvu Sekretarieti ya chama hicho kwa kuwapinga moja kwa moja wanaoibeza wakiwamo baadhi ya wenyeviti wa mikoa ambao wamekuwa wakisema inapotosha uamuzi wa NEC.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari, Rais Kikwete alitamka ndani ya kikao cha Kamati Kuu akisema; there are some stupid guys (wajinga fulani), wanaosema Sekretariati hiyo inakivuruga chama kwa namna wanavyosimamia utekelezaji wa uamuzi wa NEC; hasa wa kujivua gamba.
Katika kile kinachoweza kutafsiriwa moja kwa moja kuwa ni kuwapuuza baadhi ya viongozi wanaodai kuwa Sekretariati imekuwa ikisimamia uamuzi wa kujivua gamba, kinyume cha matakwa ya Halmashauri Kuu, Kamati Kuu imeipongeza Sekretariati hiyo.
Hatua hiyo inatajwa kuwa ni pigo kwa baadhi ya viongozi wa sasa wa chama hicho, wakiwamo wanaopaswa kujiuzulu nafasi za uongozi katika chama hicho - Chenge na Lowassa; huku Rostam naye akijiuzulu kwa kulalamikia Sekretariati hiyo akisema inaendesha siasa uchwara.
Wengine katika orodha ya kuishambulia Sekretariati hiyo na hasa Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ni John Guninita, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM-Dar es Salaam na Hamisi Mgeja Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, wote wakitajwa kuwa karibu na viongozi wanaotakiwa kujiuzulu.
Taarifa kutoka ndani ya kikao cha Kamati Kuu zinaeleza kuwa Rais Kikwete ni kati ya viongozi walioweka wazi msimamo wao kuhusu mwenendo wa Sekretariati, akimtaja kwa jina Nape Nnauye.
Chanzo chetu cha habari kinamnukuu Rais Kikwete ambaye ndiye Mwenyekiti wa kikao hicho kilichotanguliwa na kikao cha Kamati ya Maadili ya Usalama, akiwaita watu wanadai kuwa Sekretariati hiyo haitekelezi uamuzi wa NEC kwa usahihi, kuwa ni wajinga fulani na kusisitiza kuwa amevutiwa sana na utendaji wao akitumia maneno ya Kiingereza.... I am very impressed. Malecela amgonga Rostam
Vyanzo vyetu vya habari vinaeleza kuwa Malecela ambaye wiki kadhaa alikuwa nje ya nchi kwa matibabu, alifanya mashambulizi ya hoja dhidi ya Rostam, akisema si mtu wa kulalamika kufanyiwa siasa chafu ambazo ameziasisi binafsi kiasi hata cha kuathiri raslimali za chama.
Akitaja mifano ya wazi inayogusa mwenendo wa uchumi wa CCM, Malecela ananukuliwa na vyanzo vyetu vya habari akisema CCM ilikuwa ikimiliki hisa katika kampuni moja kubwa, lakini baadaye katika mazingira yenye mafumbo, mmiliki wa hisa alibadilika, na kwamba hali hiyo ndiyo iliyopata kujitokeza katika baadhi ya vyombo vya habari nchini vilivyopata kuwa katika sehemu ya umiliki wa CCM.
3 Aug 2011
Toleo na 197
- Ni kikao chao cha faragha Lumumba
- Zawahusisha Rostam, Chenge
- Kikwete awaokoa kiaina, sasa wapumulia mashine
KILE kilichoelezwa kuwa kilikuwa ni siri kati ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Pius Msekwa na watuhumiwa waliotakiwa kujitoa ndani ya uongozi, zimeanikwa katika kikao cha Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu ya chama hicho (NEC) kilichowajadili mwishoni mwa wiki.
Mbali ya kubainishwa kwa siri za kikao cha faragha kati ya Msekwa na watuhumiwa hao, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, aliipa meno zaidi Sekretarieti ya chama hicho kwa kupuuza maneno ya baadhi ya wanaosema kwamba inakivuruga chama hicho tawala.
Watuhumiwa hao, Mbunge wa Igunga Rostam Aziz, ambaye tayari amejitoa na wenzake; Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa na Andrew Chenge ambaye ni Mbunge wa Bariadi Magharibi, walikutana na Msekwa kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam na kati yao hakuna aliyekuwa tayari kuzungumzia kilichozungumzwa.
Ni Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Kikwete, ambaye alitoa siri hiyo katika kikao cha Kamati Kuu alipotuliza baadhi ya wajumbe wa kikao hicho cha juu cha chama hicho waliotaka watuhumiwa hao watimuliwe mara moja.
Kikwete alitoa siri hiyo akimtuliza Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais mstaafu, Mzee John Malecela, aliyeonekana kikaoni kuanza kufanikiwa kushawishi wajumbe kushinikiza Kamati Kuu iwafukuze moja kwa moja, akina Lowassa na Chenge, kabla kikao kijacho cha Halmashauri Kuu. Kikwete awaokoa kina Lowassa
Kwa mujibu wa mtoa taarifa wetu, Kikwete, akionekana kama kusoma nyuso za wajumbe, alieleza kuwa ni busara zaidi kusimamia uamuzi wa NEC uliowapa muda wa kujivua gamba watu hao kuwa mwisho ni kikao kijacho cha Halmashauri hiyo Kuu.
Katika kile kinachoweza kuelezwa kuwa kufichuka kwa sehemu ya siri ya Msekwa moyoni, Kikwete alimgeukia Msekwa akiuliza; hivi si walikwambia wanaomba muda wa kutafakari? Naye msekwa alijibu ndiyo.
Kilichokuwa kikirejewa na Kikwete katika swali lake kwa Msekwa ni kilichojadiliwa kwenye kikao kati ya Makamu huyo Mwenyekiti na Lowassa, Chenge na Rostam ambao alikutana nao kwa nyakati tofauti katika ofisi ndogo za CCM, Lumumba Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa maelezo hayo ya Msekwa, imebainika kuwa katika mazungumzo ya faragha, Lowassa, Chenge na Rostam walipobanwa waliomba muda zaidi wa kutafakari kabla ya muda wa mwisho waliopewa kufika.
Katika hilo, Kikwete anatajwa kuwashawishi wajumbe kuwapa muda zaidi kama ilivyokubaliwa faragha, na wasipoamua kama mwenzao Rostam, hatua nyingine zitafuata.
Tayari baadhi ya wajumbe walionekana kukubaliana na uamuzi wa kuwatimua wanasiasa hao wawili waliogoma kujitoa hadi sasa baada ya mwenzao Rostam Aziz kufanya uamuzi mgumu wa kuachia nafasi zote ikiwamo ubunge, kabla ya Rais Kikwete kuokoa jahazi.
Chenge, Lowassa bado hawajaamua
Baada ya kimya cha muda mrefu, Chenge ameibukia mjini Dodoma akichangia bajeti ya Wizara ya Ujenzi, alipowataka wapiga kura wake kupuuza yale aliyoyaita maneno ya mitaani kumhusu, akizima tetesi za hivi karibuni kwamba alikwishajiondoa katika nafasi zake za uongozi kutekeleza maamuzi ya kikao cha NEC kilichopita.
Kwa upande wake, Lowassa amekuwa akitoa matamshi ya chini chini kuonyesha kutokuwa tayari kujitoa; huku akiahidi kutoa tamko rasmi wakati mwafaka utakapowadia, baadhi ya watu wakitabiri kishindo kutoka kwa mwanasiasa huyo anayetajwa sana kuwania nafasi ya urais kumrithi Kikwete mwaka 2015.
Kikwete aipa nguvu Sekretariati mpya
Katika kikao hicho cha CC, Rais Kikwete alirudia kuipa nguvu Sekretarieti ya chama hicho kwa kuwapinga moja kwa moja wanaoibeza wakiwamo baadhi ya wenyeviti wa mikoa ambao wamekuwa wakisema inapotosha uamuzi wa NEC.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari, Rais Kikwete alitamka ndani ya kikao cha Kamati Kuu akisema; there are some stupid guys (wajinga fulani), wanaosema Sekretariati hiyo inakivuruga chama kwa namna wanavyosimamia utekelezaji wa uamuzi wa NEC; hasa wa kujivua gamba.
Katika kile kinachoweza kutafsiriwa moja kwa moja kuwa ni kuwapuuza baadhi ya viongozi wanaodai kuwa Sekretariati imekuwa ikisimamia uamuzi wa kujivua gamba, kinyume cha matakwa ya Halmashauri Kuu, Kamati Kuu imeipongeza Sekretariati hiyo.
Hatua hiyo inatajwa kuwa ni pigo kwa baadhi ya viongozi wa sasa wa chama hicho, wakiwamo wanaopaswa kujiuzulu nafasi za uongozi katika chama hicho - Chenge na Lowassa; huku Rostam naye akijiuzulu kwa kulalamikia Sekretariati hiyo akisema inaendesha siasa uchwara.
Wengine katika orodha ya kuishambulia Sekretariati hiyo na hasa Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ni John Guninita, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM-Dar es Salaam na Hamisi Mgeja Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, wote wakitajwa kuwa karibu na viongozi wanaotakiwa kujiuzulu.
Taarifa kutoka ndani ya kikao cha Kamati Kuu zinaeleza kuwa Rais Kikwete ni kati ya viongozi walioweka wazi msimamo wao kuhusu mwenendo wa Sekretariati, akimtaja kwa jina Nape Nnauye.
Chanzo chetu cha habari kinamnukuu Rais Kikwete ambaye ndiye Mwenyekiti wa kikao hicho kilichotanguliwa na kikao cha Kamati ya Maadili ya Usalama, akiwaita watu wanadai kuwa Sekretariati hiyo haitekelezi uamuzi wa NEC kwa usahihi, kuwa ni wajinga fulani na kusisitiza kuwa amevutiwa sana na utendaji wao akitumia maneno ya Kiingereza.... I am very impressed. Malecela amgonga Rostam
Vyanzo vyetu vya habari vinaeleza kuwa Malecela ambaye wiki kadhaa alikuwa nje ya nchi kwa matibabu, alifanya mashambulizi ya hoja dhidi ya Rostam, akisema si mtu wa kulalamika kufanyiwa siasa chafu ambazo ameziasisi binafsi kiasi hata cha kuathiri raslimali za chama.
Akitaja mifano ya wazi inayogusa mwenendo wa uchumi wa CCM, Malecela ananukuliwa na vyanzo vyetu vya habari akisema CCM ilikuwa ikimiliki hisa katika kampuni moja kubwa, lakini baadaye katika mazingira yenye mafumbo, mmiliki wa hisa alibadilika, na kwamba hali hiyo ndiyo iliyopata kujitokeza katika baadhi ya vyombo vya habari nchini vilivyopata kuwa katika sehemu ya umiliki wa CCM.