RAI - Nguvu ya Hoja?

mhariri wa TZ daima na balile wote ni makanjanja tu!Balile anawatumikia kina RA na kikosi chake na wa TZ daima anawatumikia kina Mbowe na kikosi chake!1+1=1
Wote wale wale!


Tuthibitishie, Tanzania Daima wamekanusha hilo dai!, Kibaya zaidi ni kuwa aliyesaidia kulisajili Tanzania Daima alikuwa BALILE! Sasa nachanganyikiwa.

Inawezekana kweli hata kama unamtumikia Bwana inabidi ujue, Bwana gani , let say Mungu na Shetani? Ukimtumikia shetani hata watoto wadogo wanamwogopa! offcoursetunasema shetani huyoo, wanalala kwa hofu!

Waberoya
 
kumbe wewe una upande!mimi najadili ukweli!sina upande mimi nakosoa wote!sijali Rai wala cha TZ daima!

Ndiyo unakuwa kama refarii, sawa hakuna anayekataa, mimi pia sina upande, lakini unafikiri ni gazeti gani kati ya RAI NA TZ daima linalowakilisha mawazo ya wananchi? hata kama huna upande, lakini unajua kipi kizuri na kipi kibaya! Haihitaji mitume waje wakufunulie macho ili uone kuwa kati ya hilo mojawapo ni baya( scrap), AU TUELEZE UBAYA WA TZ DAIMA, then will agree with you!

Hata nikiwa na upande bado najua pande upi mzuri upi mbaya, hapo nakuwa mwanamapinduzi halisi, unafikiri BALILE NA RWEYEMAMU HAWAJUI WANAFANYA UBAYA? MATUMBO firs lady yametugawa wengi!
 
kumbe wewe una upande!mimi najadili ukweli!sina upande mimi nakosoa wote!sijali Rai wala cha TZ daima!



Sawa lakini rudi soma kwa mantiki hoja walizo andika wahariri wote kisha pembua kwa uyakinifu utaona mapungufu....wewe umecrash kote sasa tunashindwa kukuelewa wakati vitu vipo clear ....Kumbuka Balile ndie aliye lisajili Tanzania Daima mbona katika maoni yake hasemi kama Mbowe alimtuma asajili Tanzania Daima??
 
Sasa ishaanza kuwa ni Tanzania Daima vs Rai... Nawashauri wayaongelee pembeni na kumalizana na wakubaliane kuwa siasa za kubeba 'watu flani' hazitotupeleka popote. Mwisho wa umaarufu wao utafika lakini ujuzi wenu kama waandishi utabaki, fedheha itawekwa wapi?

Taifa mbele!

Invisible na ushindwe kabisa. Yaani unataka kutuondolea uhondo wa mellenia sasa. Bahati kama hizi za kufuatilia mpambano wa wazi kati ya waandishi wa habari wenye kuju mengi kuhusu usafi na uozo wa nchi yetu ni baraka kubwa kwa raia wema wanaopitwa na wengi. Vilevilemwisho wa mpambano kama huu ni kujuana kwa undani zidi miongoni mwetu na pengine hata kuweza kupata UANDISHI uliokomaa. Hii ni kafara inayohitajika kuondoa makubaliano ya gizani kati ya waandishi na waandishi na vyombo vya habari na vyombo vya habari ambayo kwa miaka mingi imepelekea kukua kwa ufisadi mkubwa katika sekta hiyo. Wacha wapambane sisi tupate uhondo...
 
Waandishi wa habari wamekuwa vibaraka wa wanasiasa!wanashindwa kuandika ubaya wanaofanya wamiliki wao!gazeti la TZ daima kamwe halisemi mabaya ya mbowe!hivyo hivyo gazeti la RAI halisemi mabaya ya RA!haijalishi ubaya wa nani ni mkubwa zaidi!Ufisadi hadi kwenye elimu za watu!Waandishi wa habari kataeni taaluma zenu kununuliwa na Mafisadi!
au ndo mambo ya pesa kwanza taaluma baadae!
msg sent!
 
"Mafahari wawili wakigombana zinazoumia ni nyasi tu"

Endeleeni kujadili bila ya kujua 'what is next?'
 
Sawa lakini rudi soma kwa mantiki hoja walizo andika wahariri wote kisha pembua kwa uyakinifu utaona mapungufu....wewe umecrash kote sasa tunashindwa kukuelewa wakati vitu vipo clear ....Kumbuka Balile ndie aliye lisajili Tanzania Daima mbona katika maoni yake hasemi kama Mbowe alimtuma asajili Tanzania Daima??

Kumbe wewe unaangalia nakala iliyooandikwa na Rai na walivyojibu TZ daima!ok mimi naangalia mwenendo mzima wa haya magazeti na habari ambazo huwa zinaandikwa!Haya bwana unafikiri kwa nini CCM hawauoni ufisadi unaofanywa na wanachama wao?ukipata jibu basi ndo maana wewe huuoni ukanjanja wa TZ daima kwa kutumiwa na MBOWE!
 
Nimesoma Rai jana nikashangaa sana hasa pale Walipoilaumu CHADEMA kuwa ndiyo waliosababisha kujiuzulu kwa Lowasa! Yaani hawa Rai wanataka tuyamini kuwa Kamati ya Bunge ni CHADEMA! Shame on them! Hili gazeti siku hizi hata halieweki Udaku si Udaku, Uchambuzi hakuna kitu yaani liko ovyoovyo tu na naamini muda si mrefu Mmiliki wake atashindwa kuendelea kulichapisha, hata kama ni Bilionea!
 
Ballile amejitakia, hawezi kutukana gazeti ambalo amelianzisha yeye na pia katika tahariri yake ameandika makosa ya Tanzania Daima mwaka 2005, kipindi ambacho yeye alikuwa mhariri mkuu wake na ndiye aliyeandika tahariri nyingi kuelezea jinsi gazeti hilo lilivyo huru. KAma angetaka kusema angewaomba radhi kwanza Watanzania kwa kuwadanganya wakati huo na sasa ndipo asema anayotaka kusema tena kwa ushahidi na si maneno ya hisia. Ballile ana taaluma lakini kwa bahati mbaya haitumii kabisa


Lakini yawezekana wakati anaandika hayo Tzdaima lilikua huru Lakini saizi limenunuliwa wewe unaonaje?

CCM ya Nyerere ilichukukia Mafisadi na CCM ya saizi inakumbatia mafisadi Je kunauhalali wa kumhoji Nyerere kua alitutaganya ya kua CCM inachukia ufisadi?

Utakua nawakati mgumu sana hapa duniani to work with past experience
 
Waandishi kama hao ndo wanaofadhiliwa na mafisadi. Kwa mambo yao kama haya yatupe hasira na ari ili tuikomboe nchi yetu
Tanzania ni yetu na sisi ndo tunauchungu tuzidishe mapigano ili inchi yetu ipone na huu ukwasi
Jf idumu na iendelee kudumu mpaka kieleweke.
Mungu ibariki Tanzania
 
Waandishi wa habari wamekuwa vibaraka wa wanasiasa!wanashindwa kuandika ubaya wanaofanya wamiliki wao!gazeti la TZ daima kamwe halisemi mabaya ya mbowe!hivyo hivyo gazeti la RAI halisemi mabaya ya RA!haijalishi ubaya wa nani ni mkubwa zaidi!Ufisadi hadi kwenye elimu za watu!Waandishi wa habari kataeni taaluma zenu kununuliwa na Mafisadi!
au ndo mambo ya pesa kwanza taaluma baadae!
msg sent!

Tz Daima- nitafutieni sehemu ilipo mpinga Mbowe na CHADEMA.

Ndiyo RAI ni ya RA na LOWASA na TZ Daima ni ya MBOWE na CHADEMA huo ndio ukweli.

Ukipenda CHONGO ni KENGEZA.

Ukweli ni wote hao RAI na TZ daima wanawatumikia mabwana wao ama MABEBERU wao.
 
Tz Daima- nitafutieni sehemu ilipo mpinga Mbowe na CHADEMA.

Ndiyo RAI ni ya RA na LOWASA na TZ Daima ni ya MBOWE na CHADEMA huo ndio ukweli.

Ukipenda CHONGO ni KENGEZA.

Ukweli ni wote hao RAI na TZ daima wanawatumikia mabwana wao ama MABEBERU wao.

Wengi wetu tumeingia mkenge wa ushabiki pasi na kuangalia kwa kina ni nini kilichopelekea mzozo kama huu.

Leo hii hawa wakubwa wawili wanaomiliki vyombo hivi vya habari vya Tanzania Daima na Rai hawako kwenye terms nzuri baina yao, na wanawatumia wananchi wa kawaida katika kufanikisha mambo yao, ikiwa ni pamoja na vita ya maneno. Tumegeuka kuwa midomo yao bila ya sisi wenyewe kuchukua muda na kutafakari.

Freeman na Rostam ni wanasiasa, isitoshe ni wafanya biashara pia. Kwa hiyo basi migongano ya kimaslahi kama wafanyibiashara inawezekana ni sababu tosha ya mmoja wao kumwonea wivu mwingine, hii ni kawaida ya binadamu haikwepeki.

Ninashauri mashabiki chukueni muda kutafakari zaidi na mjiulize maswali lukuki, itakuwaje siku ya siku hawa wafanyabiashara wawili wakipatana na hata kufikia Rostam kununua Tanzania Daima au Freeman kununua Rai? Je, mtakuwa katika nafasi gani siku Freeman akiamua kumpa ajira tena Balile?

Tuna matatizo mengi ya kijamii yanayohitaji attention yetu na sio kuwapigia debe wenye nazo.
 
Wengi wetu tumeingia mkenge wa ushabiki pasi na kuangalia kwa kina ni nini kilichopelekea mzozo kama huu.

Leo hii hawa wakubwa wawili wanaomiliki vyombo hivi vya habari vya Tanzania Daima na Rai hawako kwenye terms nzuri baina yao, na wanawatumia wananchi wa kawaida katika kufanikisha mambo yao, ikiwa ni pamoja na vita ya maneno. Tumegeuka kuwa midomo yao bila ya sisi wenyewe kuchukua muda na kutafakari.

Freeman na Rostam ni wanasiasa, isitoshe ni wafanya biashara pia. Kwa hiyo basi migongano ya kimaslahi kama wafanyibiashara inawezekana ni sababu tosha ya mmoja wao kumwonea wivu mwingine, hii ni kawaida ya binadamu haikwepeki.

Ninashauri mashabiki chukueni muda kutafakari zaidi na mjiulize maswali lukuki, itakuwaje siku ya siku hawa wafanyabiashara wawili wakipatana na hata kufikia Rostam kununua Tanzania Daima au Freeman kununua Rai? Je, mtakuwa katika nafasi gani siku Freeman akiamua kumpa ajira tena Balile?

Tuna matatizo mengi ya kijamii yanayohitaji attention yetu na sio kuwapigia debe wenye nazo.

Ukweli ni huo ndg yangu na umenena
Sisi tunaingizwa mkenge kirahisi sana na tunakua kama mashabiki wa mpira .
 
Balile pole sana kaka. naona njaa yako inakusumbua sana. Afadhali ungeenda pale TIRDO kwa Mkono ukajustify kwa nini wakupeleke Hull kuliko kupokea fadhila kama kuna ukweli.

Kama walikupeleka nahisi target ni kuwa kutumia ujuzi na knowledge from there kulenga mbali ambapo sasa unaanza kulenga miguuni mwako. unatofauti na mimi ambae hata TIMES sijui ipo mtaa gani pale jijini?

Tumia taaluma yako kumpeleka "BWANA" wako kule alikotegemea sio kuanguko. Chombo utakipeleka wapi? CV yako utaandika nini kaka? Elimu cheti ndo hii sasa.

Asanteni
 
Wengi wetu tumeingia mkenge wa ushabiki pasi na kuangalia kwa kina ni nini kilichopelekea mzozo kama huu.

Leo hii hawa wakubwa wawili wanaomiliki vyombo hivi vya habari vya Tanzania Daima na Rai hawako kwenye terms nzuri baina yao, na wanawatumia wananchi wa kawaida katika kufanikisha mambo yao, ikiwa ni pamoja na vita ya maneno. Tumegeuka kuwa midomo yao bila ya sisi wenyewe kuchukua muda na kutafakari.

Freeman na Rostam ni wanasiasa, isitoshe ni wafanya biashara pia. Kwa hiyo basi migongano ya kimaslahi kama wafanyibiashara inawezekana ni sababu tosha ya mmoja wao kumwonea wivu mwingine, hii ni kawaida ya binadamu haikwepeki.

Ninashauri mashabiki chukueni muda kutafakari zaidi na mjiulize maswali lukuki, itakuwaje siku ya siku hawa wafanyabiashara wawili wakipatana na hata kufikia Rostam kununua Tanzania Daima au Freeman kununua Rai? Je, mtakuwa katika nafasi gani siku Freeman akiamua kumpa ajira tena Balile?

Tuna matatizo mengi ya kijamii yanayohitaji attention yetu na sio kuwapigia debe wenye nazo.

Pundamilia07,

Naona hapa umepotoka kidogo. mimi namjua mbowe kama m/kiti wa chadema. sijui mimi kama anamiliki t/daima. namjua rostam kama mbunge wa igunga. na ndio mwanzo na connection hii inapoanzia. ukisema vingine utakuwa unapoteza mweleko.

Wakiwa wamiliki wa hizo biashara then wanatoa policy tu sasa ni kazi ya wataalam kuwork on it. ukitaka kutupeleka huko tutafanya kazi za akina balile na kibanda na tutachanganyikiwa kama balile. Hata wewe haya ni maoni yako based on politics, je nikisema unasema hivi kutokana na mazingira yako kwa sasa utanielewa?

asante
 
Tz Daima- nitafutieni sehemu ilipo mpinga Mbowe na CHADEMA.

Ndiyo RAI ni ya RA na LOWASA na TZ Daima ni ya MBOWE na CHADEMA huo ndio ukweli.

Ukipenda CHONGO ni KENGEZA.

Ukweli ni wote hao RAI na TZ daima wanawatumikia mabwana wao ama MABEBERU wao.

Mkamap,

unaishi sayari ipi? sitegemei hata sikumoja rai kumpinga RA na EL ila nategemea kukaa kimya pale penye ukweli. Hata Mengi alishasema kuwa wao wanatoa tu policy kwenye Kulikoni na Thisday na sio kuandika. Kama wewe utakuwa umeajiri mtu then akaanza na wewe kutakuwa na tatizo na huyo mwajiriwa wako anatakiwa aachane na wewe then ndo aanze kudiffer na wewe. Ukishaweka policy unaweza kwenda mbali zaidi na kuwa na guidelines na standard to meet your committments. unaishia hapo. ukienda mpaka kwenye day2day mtaalam hapo anatakiwa aondoke. kama balile anatakiwa aondoke na kibanda habari ndio hio.

thank you and idios
 
Hii imetoka kwenye RAI la tarehe 18-24 Septemba 2008, toleo namba 782.

I remain speechless!

attachment.php


HIVI HUYU BALILE..HUKO NYUMA ANA MATATIZO ,,,,,,,,,,,,???..INAKUWAJE ASEME KUWA CHADEMA NDIO WAASISI WA SIASA ZA KUCHAFUANA TANGU MWAKA 2005...........WAKATI SIASA ZA KUCHAFUANA NCHI HII MWASISI WAKE ANAJULIKANA KUWA NI MTANDAO[KIKWETE,LOWASSA,ROSTAM,MEMBE...]...WALIOANZA NA KUWACHAFUA CCM..KINA DR HASSY KITINE,IDDI SIMBA,MALECELA,SUMAYE,DR SALIM ..na wengine waliokuwa tishio kwao..........????
 
Pundamilia07,

Naona hapa umepotoka kidogo. mimi namjua mbowe kama m/kiti wa chadema. sijui mimi kama anamiliki t/daima. namjua rostam kama mbunge wa igunga. na ndio mwanzo na connection hii inapoanzia. ukisema vingine utakuwa unapoteza mweleko.

Wakiwa wamiliki wa hizo biashara then wanatoa policy tu sasa ni kazi ya wataalam kuwork on it. ukitaka kutupeleka huko tutafanya kazi za akina balile na kibanda na tutachanganyikiwa kama balile. Hata wewe haya ni maoni yako based on politics, je nikisema unasema hivi kutokana na mazingira yako kwa sasa utanielewa?

asante

Kichwangumu,
Ahsante sana kwa mchango wako.
Lakini usijifanye kuwa umevaa miwani ya mbao na kuziba masikio. Kama kweli hujui kuwa Freeman Mbowe (Mwenyekiti wa Chadema) ndiye mmiliki wa Tanzania Daima, basi unaangukia kule kwa wahenga walikosema kuwa 'usilolijua litakusumbua' ... 'usilolijua ni sawa na usiku wa giza'
Kwahiyo kaa chini tafakari, fanya upembuzi then utapata mwelekeo!
 
Back
Top Bottom