RAI: CCM yaijibu CHADEMA; Nape amtahadharisha Freeman Mbowe

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
[h=2][/h] Jumatatu, Mei 07, 2012 05:00 Na Gabriel Mushi, Dar es Salaam




nape.jpg
Nape Nnauye

* Yakana taarifa za wabunge wake kuhama
* Nape amtahadharisha Freeman Mbowe

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, ameibuka na kukana taarifa zilizotolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, kwamba kuna wabunge 70 wa CCM wanataka kuhamia Chadema.

Aidha, amemtaka Mbowe kuwa makini kutokana na nyadhifa alizonazo ndani ya chama hicho cha upinzani.

Akizungumza na MTANZANIA kwa simu jana, Nape alisema amesikitishwa na kauli ya Mbowe kwa kuwa ameitoa bila kufanya utafiti.

“Mbowe anatakiwa kumwachia Dk. Slaa (Katibu Mkuu wa Chadema), azungumze masuala hayo ya kisiasa kwa ajili ya kuleta picha nzuri ndani ya jamii.

“Mbowe asisahau kuwa yeye ni Mwenyekiti wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, pia ni kiongozi mkubwa wa chama hicho, asizungumze masuala kama hayo yasiyokuwa na tija mbele ya jamii.

“Anachokisema Mbowe ni sawa na mtu ambaye anapigana halafu anapigwa huku akipiga kelele kwamba, njooni mnitoe nitamuua huyu wakati yeye ndiye anayepigwa. Au ni sawa na mtu anayetaka kujiua halafu anakuja kuniambia kuwa sasa nataka kujiua, huyu anataka nikamwokoe hana maana yoyote.

“Kwa hiyo, kauli ya Mbowe imenisikitisha sana kwa sababu naona kama amekurupuka, kwa hiyo, ninachotaka kumshauri ni kwamba, ajiheshimu kwa kauli zake, kulingana na nafasi zake za kiungozi alizonazo katika chama na jamii kwa ujumla,” alisema Nape.

Juzi, Mbowe alipokuwa jijini Arusha alihutubia mkutano wa hadhara na kusema miongoni mwa walioomba kujiunga na CHADEMA ni mawaziri walioteuliwa na Rais Jakaya Kikwete.

Akiwahutubia wananchi na makada wa chama hicho waliofika katika mkutano wa uzinduzi wa Operesheni Vua Gamba, Vaa Gwanda, uliofanyika mkoani Arusha, Mbowe alisema kuna wimbi kubwa la wanachama watakaohamia CHADEMA.

Akinukuliwa na vyombo vya habari, Mbowe alisema “Kwanza namtahadharisha Rais Kikwete katika Baraza la Mawaziri alilolitangaza jana.

“Wapo mawaziri tisa ambao wameniomba nafasi CHADEMA, kwa nyie mlioingia leo karibuni CHADEMA, huku hakuna rushwa wala ufisadi, unapiga gwanda, unapiga kazi tu.

“Wana CHADEMA msiwe na hofu na wale wanaojiunga na chama kutokea CCM, kwa kuwa kuna wengi walitoka huko na ni wapigania haki wazuri. Kwa mfano, Katibu Mkuu, Dk. Willbrod Slaa, Mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje na Makamu Mwenyekiti wetu, Said Amour Arfi, ambaye alikuwa TLP kabla ya kujiunga CHADEMA,” alisema Mbowe.
 
Kwanini Nape Nnauye anakana? Yeye alipokuwa anampango wa kuhama CCM; nani alimpingia? CCM iache kuwalinda wanachama wake kama wakati wa Ucomunist; it is free now they can choose where to go; what party to Join.

Nape, hajui Mawazo ya binadamu yoyote...
 
[h=2][/h] Jumatatu, Mei 07, 2012 05:00 Na Gabriel Mushi, Dar es Salaam




nape.jpg
Nape Nnauye

* Yakana taarifa za wabunge wake kuhama
* Nape amtahadharisha Freeman Mbowe

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, ameibuka na kukana taarifa zilizotolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, kwamba kuna wabunge 70 wa CCM wanataka kuhamia Chadema.

Aidha, amemtaka Mbowe kuwa makini kutokana na nyadhifa alizonazo ndani ya chama hicho cha upinzani.

Akizungumza na MTANZANIA kwa simu jana, Nape alisema amesikitishwa na kauli ya Mbowe kwa kuwa ameitoa bila kufanya utafiti.

“Mbowe anatakiwa kumwachia Dk. Slaa (Katibu Mkuu wa Chadema), azungumze masuala hayo ya kisiasa kwa ajili ya kuleta picha nzuri ndani ya jamii.

“Mbowe asisahau kuwa yeye ni Mwenyekiti wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, pia ni kiongozi mkubwa wa chama hicho, asizungumze masuala kama hayo yasiyokuwa na tija mbele ya jamii.

“Anachokisema Mbowe ni sawa na mtu ambaye anapigana halafu anapigwa huku akipiga kelele kwamba, njooni mnitoe nitamuua huyu wakati yeye ndiye anayepigwa. Au ni sawa na mtu anayetaka kujiua halafu anakuja kuniambia kuwa sasa nataka kujiua, huyu anataka nikamwokoe hana maana yoyote.

“Kwa hiyo, kauli ya Mbowe imenisikitisha sana kwa sababu naona kama amekurupuka, kwa hiyo, ninachotaka kumshauri ni kwamba, ajiheshimu kwa kauli zake, kulingana na nafasi zake za kiungozi alizonazo katika chama na jamii kwa ujumla,” alisema Nape.

Juzi, Mbowe alipokuwa jijini Arusha alihutubia mkutano wa hadhara na kusema miongoni mwa walioomba kujiunga na CHADEMA ni mawaziri walioteuliwa na Rais Jakaya Kikwete.

Akiwahutubia wananchi na makada wa chama hicho waliofika katika mkutano wa uzinduzi wa Operesheni Vua Gamba, Vaa Gwanda, uliofanyika mkoani Arusha, Mbowe alisema kuna wimbi kubwa la wanachama watakaohamia CHADEMA.

Akinukuliwa na vyombo vya habari, Mbowe alisema “Kwanza namtahadharisha Rais Kikwete katika Baraza la Mawaziri alilolitangaza jana.

“Wapo mawaziri tisa ambao wameniomba nafasi CHADEMA, kwa nyie mlioingia leo karibuni CHADEMA, huku hakuna rushwa wala ufisadi, unapiga gwanda, unapiga kazi tu.

“Wana CHADEMA msiwe na hofu na wale wanaojiunga na chama kutokea CCM, kwa kuwa kuna wengi walitoka huko na ni wapigania haki wazuri. Kwa mfano, Katibu Mkuu, Dk. Willbrod Slaa, Mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje na Makamu Mwenyekiti wetu, Said Amour Arfi, ambaye alikuwa TLP kabla ya kujiunga CHADEMA,” alisema Mbowe.

nadhan mbowe alijisahau
alidhan yupo pale ikulu kwake bilicanas
 
Kwa staili hii ya Nape aliyotumia kanusha, kunauwezekano mkubwa maneno ya Mh. Mbowe yakawa sahihi.
 
Nape hajui kama CCM yake ina matobo kama vyandaraua vya ''kwa msaada wa watu wa Marekani''

Inawezekana hata JK anataka kuhamia kwenye M4C ila nape hajui
 
Mimi naamini wengi wanasubiri tu posho, hata hivyo naamini kuna watakaohama kabla ya kumbaliza msimu kama alivyofanya mpendazoe. Litakapotokea naomba Nape uwe tayari kufuta usemi wako, kwani unawasemea watu ambao wana fikra tofauti na wewe, kuna waliotarajia uwaziri wameukosa sasa wana kinyongo ile mbaya.
 
Yeye ni Mbunge wa Vitu Maalum akihama kuhamia Chadema nani atampa Ulaji kama anaoupata kama Mbunge?

Wabunge wengi wezi tu hawawezi kuachia hivyo vyeo, anasema kinamuuma nadhani alitaka pia Uwaziri na hiyo Ph.D
 
Back
Top Bottom