Raha ya kuwa na mbunge wa CCM katika jimbo

Kakke

JF-Expert Member
Dec 4, 2010
1,883
1,482
RAHA YA KUWA NA MBUNGE WA CCM KATIKA JIMBO LAKO HII HAPA

"Mheshimiwa Spika, kabla sijaingia kuchangia bajeti hii, nataka niseme kuwa naona upinzani wamefikia pabaya sana, wanaikashifu serikali sikivu ya CCM. Chama kimefanya mengi sana, maendeleo makubwa tumepata, shule za msingi, sekondari na vyuo viko vingi sana tofauti na zamani, barabara za lami, umeme nchi nzima mpaka vijijini, lakini wapinzani wanakebehi.

Naipongeza sana serikali ya Chama Cha Mapinduzi. Mheshimiwa Spika, bila kupoteza muda sasa niingie kwenye jimbo langu, naomba nielezee kwa kifupi matatizo ya jimbo langu. Kule hatuna shule za sekondari katika kata sita, maji ni ndoto, tunategemea mvua za msimu. Shule zilizopo hazina ubora wala walimu wa kutosha. Rais alikuja sasa ni miaka sita akatuahidi umeme lakini mpaka leo hakuna lolote. Barabara ni mbovu hazipitiki.

Nauliza ni lini serikali hii (ya CCM) itatusikia na kutuletea maendeleo?"(Wab unge Makofi) kwa! Kwa! Kwa!. Naombeni sana tena sana jimbo langu liangaliwe kwa jicho la Huruma. Baada ya kusema hayo Mheshimiwa Spika, naunga mkono bajeti kwa 100%
 
Ili ujue kua hakuna tofauti kati ya wabunge wa upinzani na wa ccm posho za vikao vyote vya bunge na mikopo ya Vx wabunge wa upinzani wanavipiga kama kawaida.
 
Haaa haaaa unadhani wabunge wa CCM wajinga ndio maana wanapinga TBC1 kuonyesha live mazingaumbwe yao.
 
RAHA YA KUWA NA MBUNGE WA CCM KATIKA JIMBO LAKO HII HAPA

"Mheshimiwa Spika, kabla sijaingia kuchangia bajeti hii, nataka niseme kuwa naona upinzani wamefikia pabaya sana, wanaikashifu serikali sikivu ya CCM. Chama kimefanya mengi sana, maendeleo makubwa tumepata, shule za msingi, sekondari na vyuo viko vingi sana tofauti na zamani, barabara za lami, umeme nchi nzima mpaka vijijini, lakini wapinzani wanakebehi.

Naipongeza sana serikali ya Chama Cha Mapinduzi. Mheshimiwa Spika, bila kupoteza muda sasa niingie kwenye jimbo langu, naomba nielezee kwa kifupi matatizo ya jimbo langu. Kule hatuna shule za sekondari katika kata sita, maji ni ndoto, tunategemea mvua za msimu. Shule zilizopo hazina ubora wala walimu wa kutosha. Rais alikuja sasa ni miaka sita akatuahidi umeme lakini mpaka leo hakuna lolote. Barabara ni mbovu hazipitiki.

Nauliza ni lini serikali hii (ya CCM) itatusikia na kutuletea maendeleo?"(Wab unge Makofi) kwa! Kwa! Kwa!. Naombeni sana tena sana jimbo langu liangaliwe kwa jicho la Huruma. Baada ya kusema hayo Mheshimiwa Spika, naunga mkono bajeti kwa 100%
RAHA YA KUWA NA MBUNGE MSOMI WA UKAWA
 
Ndio maana Dar wamechagua wabunge wengi wa upinzani na Hospitali barabara na mengineyo yanaboreshwa hata vitanda kutoka Hospitali ya Singida na CTScan+ MRI machine tumechukua kutoka Dodoma walikoichagua chama tawala kwa wingi..
 
Ili ujue kua hakuna tofauti kati ya wabunge wa upinzani na wa ccm posho za vikao vyote vya bunge na mikopo ya Vx wabunge wa upinzani wanavipiga kama kawaida.
Lakini bora wa upinzani maana kwa mbali wanaonyesha moyo wa kutujari japo kwa kutusemea
 
Kwan wale wa chadema wana kip cha maana, kutetea bunge kuoneshwa live pia kupinga kila kitu
 
Wabunge wa Ccm siyo wawakilishi wa wananchi bali ni wawakilishi na wasemaji wa serikali. Na hii inasababishwa na utaratibu mbovu unao tumika kuwapata kuanzia chamani. Kwanza ni lazima uwe mtu wa kujipendekeza ndani ya chama na serikali, pili lazima utumie rushwa kuipata hiyo nafasi ndani ya chama na tatu lazima uwe mwizi wa kura hasa linapokuja suala la uchaguzi mkuu.
Ukithubuti kuiponda serikali basi ujue wanakuhesabia siku tu kama sio miezi ili wakupige chini.
 
Ndio maana Dar wamechagua wabunge wengi wa upinzani na Hospitali barabara na mengineyo yanaboreshwa hata vitanda kutoka Hospitali ya Singida na CTScan+ MRI machine tumechukua kutoka Dodoma walikoichagua chama tawala kwa wingi..
Kweli ni raha kuwa na mbunge wa ccm Dar es Salaam tulipo chagua upinzani maendeleo kwanza Dodoma mkaisome namba
 
Back
Top Bottom