RAGE awanyang'anya vifaa vya muziki bendi ya Sensema Malunde

Dec 21, 2011
71
75
Mbunge wa jimbo la Tabora mjini Ismail Aden Rage amechukua vyombo vya muziki vilivyokuwa vikitumiwa na bendi ya sensema malunde ya mkoani humo hali iliyopelekea bendi hiyo kusitisha kufanya maonesho kwa wiki tatu sasa.

Wakizungumza na gazeti hili viongozi wa bendi hiyo kwa sharti la kutotajwa majina walisema hatua hiyo ya Rage imewasikitisha sana na ina lengo la kuivuruga na kuiua bendi yao.

Walisema mapema mwaka jana kabla ya uchaguzi mkuu uliohusisha wabunge,madiwani na rais,Rage aliufuata uongozi wa bendi ya Sensema Malunde akawaeleza kuwa atanunua na kuleta vyombo vya muziki vipya kwa ajili kufanya matamasha pamoja na kushiriki katika kampeni za uchaguzi za chama cha mapinduzi.

Aidha walieleza kuwa mbali na makubaliano hayo pia walikubaliana baada ya vyombo hivyo kuanza kutumika asilimia 80 ya mapato yatakwenda kwa mmiliki ambaye ni Rage na asilimia 20 itabaki kwa viongozi.

Walisema makubaliano mengine ni pamoja na kulipa mishahara ya wanamuziki na vyombo vya bendi vya zamani viwekwe ndani.

Wameongeza kuwa baada ya vyombo hivyo kuwasili,kazi ilianza mara moja ikiwemo upigaji katika kumbi mbalimbali za burudani katika mji wa Tabora na vitongoji vyake.

Aidha wamebainisha zaidi kuwa pamoja muziki kupigwa kwenye kumbi mbalimbali za burudani pia bendi hiyo ilikuwa ikifanya kampeni zake za ubunge.

Wanasema hali ilianza kuwa mbaya mwanzoni mwa mwaka huu,ambapo hadi kufikia mwezi machi mwaka huu wanamuziki walianza kusotea mishahara yao na ndiyo ukawa mwisho wa na mparaganyiko wa bendi.

Walisema Rage alichukua vyombo vyake vya muziki,na kuvifungia ndani na baadhi ya wanamuziki amewahamishia jijini Da-es-Salaam kutokana na tetesi kuwa anataka kuanzisha bendi yake huko.

Mwisho-
 
Mijitu mingine bwana! Hivi walitegemea nini kutoka kwa wanasiasa wa aina ya jamaa. Au niwaulize kivingine, hivi kondomu ikishatumika huwa inafanywaje? Siasa za kimagamba ndivyo zilivyo. Next time watie adabu badala ya kudangaywa kama mitoto midogo kwa njaa zao.
 
Mijitu mingine bwana! Hivi walitegemea nini kutoka kwa wanasiasa wa aina ya jamaa. Au niwaulize kivingine, hivi kondomu ikishatumika huwa inafanywaje? Siasa za kimagamba ndivyo zilivyo. Next time watie adabu badala ya kudangaywa kama mitoto midogo kwa njaa zao.


Naunga mkono hoja!
 
Mbunge wa jimbo la Tabora mjini Ismail Aden Rage amechukua vyombo vya muziki vilivyokuwa vikitumiwa na bendi ya sensema malunde ya mkoani humo hali iliyopelekea bendi hiyo kusitisha kufanya maonesho kwa wiki tatu sasa.

Wakizungumza na gazeti hili viongozi wa bendi hiyo kwa sharti la kutotajwa majina walisema hatua hiyo ya Rage imewasikitisha sana na ina lengo la kuivuruga na kuiua bendi yao.

Walisema mapema mwaka jana kabla ya uchaguzi mkuu uliohusisha wabunge,madiwani na rais,Rage aliufuata uongozi wa bendi ya Sensema Malunde akawaeleza kuwa atanunua na kuleta vyombo vya muziki vipya kwa ajili kufanya matamasha pamoja na kushiriki katika kampeni za uchaguzi za chama cha mapinduzi.

Aidha walieleza kuwa mbali na makubaliano hayo pia walikubaliana baada ya vyombo hivyo kuanza kutumika asilimia 80 ya mapato yatakwenda kwa mmiliki ambaye ni Rage na asilimia 20 itabaki kwa viongozi.

Walisema makubaliano mengine ni pamoja na kulipa mishahara ya wanamuziki na vyombo vya bendi vya zamani viwekwe ndani.

Wameongeza kuwa baada ya vyombo hivyo kuwasili,kazi ilianza mara moja ikiwemo upigaji katika kumbi mbalimbali za burudani katika mji wa Tabora na vitongoji vyake.

Aidha wamebainisha zaidi kuwa pamoja muziki kupigwa kwenye kumbi mbalimbali za burudani pia bendi hiyo ilikuwa ikifanya kampeni zake za ubunge.

Wanasema hali ilianza kuwa mbaya mwanzoni mwa mwaka huu,ambapo hadi kufikia mwezi machi mwaka huu wanamuziki walianza kusotea mishahara yao na ndiyo ukawa mwisho wa na mparaganyiko wa bendi.

Walisema Rage alichukua vyombo vyake vya muziki,na kuvifungia ndani na baadhi ya wanamuziki amewahamishia jijini Da-es-Salaam kutokana na tetesi kuwa anataka kuanzisha bendi yake huko.

Mwisho-

Ati huyu anawakilisha Umma..Jizi nyonyaji kubwa hili
Hata hivyo Matatizo yanayotokana na Ujinga ,Huelimisha!
 
Akisimama jukwaani anasema ataleta maendeleo na kutengeneza fursa za ajira kwa wanajimbo lake!!lol!!aibu sana!ataibuka na kusema walikuwa hawampi pesa zake....
 
wajinga hao, kwanini hawakuandikiana mkataba? haya ni mambo ya kawaida sana kwenye biashara, partners wanafarakana na kampuni huvunjika. cha msingi ni makubaliano ya mkataba kabla ya kuanza biashara ambayo hupelekwa mahakamani na kila upande kupewa haki yake. "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa" asema BWANA
 
  • Thanks
Reactions: mka
Wasubirie 2015 watakapoitwa kwa sasa kibarua kimeota majani waende wakafyeke nyasi huko Dar. Msomali Rage amepata alichokuwa anakitafuta. 2015 watume cv zao mapema kwa Magamba :lol:
 
Hakuna mbunge wa Tabora mjini anayekaa zaidi ya muhula mmoja; hivyo jamaa[ Al shabab] anajua 2015 hatarudi mjengoni ndio maana anawafanyizia hao wanamuziki!
 
wajinga ndio waliwao... 2015 march atawarudishia, watamvika na uchifu, 2016 machi atawanyanganya watatuma mtu tena jf, 2020 april atafanya tena

siwaonei huruma waliomuamini mtu ambaye alishawahi kufungwa jela kwa masuala ya kukosa uaminifu
 
Back
Top Bottom