Ngaliba Dume
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,710
- 3,669
Nina rafiki yangu wa karibu sana...yeye ana mwanamke aliyemuoa mkewe kwa mda wa mwaka mmoja hivi,lakini wakati akiwa nae,huyo dada alikuwa na mpenzi mwingine.Katika kuishi na mkewe kiukweli jamaa yangu alikuwa mbabe,mara kadhaa amempiga shemeji yangu,amemnyanyasa na kumtesa..lakini wakaoana!huyu mpenzi wa nje hakuwa anajua kuwa "demu" wake ameolewa,na kwa vile alikuwa anampenda mwanamke,anamtreat vizuri na kumpetipeti..yule dada akazama kabisa kwa mpenz wa nje,huku wakiendelea kuweka mpango ya ndoa na kuish pamoja Imetokea jamaa akagundua kuwa mkewe ana mtu nje,akamtafuta wake "mwizi" akampata,jamaa akakili kuwa hakujua na alikuwa na malengo sana na mpenzi wake,na mwanamke alipoulizwa akampa makavu mumewe kuwa hampendi,bali anampenda "mpenzi" na yupo tayali kwa lolote,ndoa imekuwa na taharuki,mwanamke asikii wala haelewi,anajuta kuwa na mumewe,mana hajui kwanin alimpenda,mana anahs anamnyanyasa na hampendi..amezama kwa mpenzi mwingine!Je hapo jamaa yangu muoaji afanye nini?