Mnamo Saa Saba na Dakika 21, leo tarehe 6 Januari 2011, nimepokea ujumbe mfupi (SMS) toka Radio One Breaking News ukisema:
"Hatimaye serikali yatangaza majina ya wamiliki wa Dowans na kutoa ufafanuzi wa fedha wanazostahili kulipwa. RADIO1 STEREO"
Mtaniwia radhi kwani habari hii inaonekana ina mapungufu kwani hawajaweka majina. Hata hivyo nimeona ni vyema kuwashirikisha. Mod, tupa kapuni kama inajirudia.
Wamiliki wa dowans watakotajwa sio wale watu wanaotegemea kuwasikia.
Msitegemee jina la Rostam wala Lowasa. Tegemeeni majina tofautia ambayo yote ni ya wageni na mmoja wao akiwa ni yule jamaa wa oman kama sijakosea yule afisa wa jeshi
fedha za kulipwa tunajua! hata majina yao tunayajua! ni kampuni ya Cyprus ya Waingereza! mambo mengine haya yote ni kiini macho tu na kutoa watu kwenye hot issue ya sasa, watu kuuliwa na polisi Arusha!
Kama ni serikali ndo imewataja basi inaonekana inapata mrahaba kutoka kwa wamiliki hao ambao imeonyesha inakubaliana na kila pendekezo La hao wahuni, tujibiwe madeni inayodaiwa serikali na watu binafsi au kampuni imeyalipa yote kiasi cha kutaka kuwalipa wahuni wa dowans.
Tanesco inadaiwa na wadeni wengi tu, uharaka wa kutaka kulipa fedha ambazo tunaweza kuzijengea barabara km 198 kwa kiwango cha lami tutakuwa tunapeperusha bendera ya majuha huku tukishangilia.watanzania hatutaki kuilipa dowans, dumu daima haitakuwa halali kuilipa dowans. Kwa hili tunatakiwa kudhihirisha uhuru na jamuhuri yetu kwamba tunajitala angalau kwa taathira kiduchu.
Hatimae serikali yatangaza wamiliki wa Dowans na kutoa ufafanuzi wa fedha wanazostaili.
Sorce:Radio one sterio
MY TAKE
Serikali ya CCM iko determined kujilipa izi hela licha ya kerere zote hizi on a serious note hii serikali imectuchoka
Redio one wanamaana gani kusema majina yametajwa halafu wao wasiyataje? wanataja kutuharubia consetration ya kufuatilia kinachitokea Arusha. waambie hivi hatudanganyiki,
Hakuna Jipya Nadhani watataja yale yale yaliyotajwa na Gazeti Moja a week ago..... Yule Mwarabu, Mkenya na Jamaa wengine... wahusika wenyewe sio wajinga hadi kuwa wamiliki directly kwahiyo hii news am sure haitakuwa na majina tunayotegemea sisi
Hii Inchi inaendeshwa kihuni sijawahi kuona. Sioni haja ya serikali kuanza kuhaha kujiosha na kuhalalisha wizi wakati kila mtu anafahamu mwanzo hadi mwisho. Cha msingi, ni kujipanga barabarani kila wakipita tuwazomeee na kuwapiga inapobidi viongozi wowote wenye mawazo mgando.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.