R.Mengi for President?

Status
Not open for further replies.

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,989
22,521
Wakuu tumejadili sana kuhusu watu wenye kufaa kutuongoza wakati huu mgumu si tu nchini mwetu..Bali Barani mwetu Afrika na Duniani kwa ujumla!
Kuna Candidates wengi tu ambao wametajwa!
Is it right to mention R.Mengi for President?
 
thumbnail.aspx


Can this man lead this Nation towards a successfull way?
 
Halafu hapohapo unajifanya wewe siyo mkabila. Ukiambiwa ukabila ni moja ya natural predispositions za binadamu unapinga kwa nguvu zote: sasa sema kwa nini umtaje exactly Mengi kati ya wafanyabiashara wote maarafu na wasafi wa kizawa? Aende akaongoze Region/Province/State/Kingdom ya Kilimanjaro.
 
thumbnail.aspx


Can this man lead this Nation towards a successfull way?

Duuh! Na picha yake unatubandikia kabisa (for good effect probably, and not least in order to drive your point home) utadhani hatujawahi kuona sura la Mangi mwenzio. :D
 
Halafu hapohapo unajifanya wewe siyo mkabila. Ukiambiwa ukabila ni moja ya natural predispositions za binadamu unapinga kwa nguvu zote: sasa sema kwa nini umtaje exactly Mengi kati ya wafanyabiashara wote maarafu na wasafi wa kizawa? Aende akaongoze Region/Province/State/Kingdom ya Kilimanjaro.

Naomba tuendelee na mjadala kistaarabu ili na wale wenye uwoga wa wanyama hatari kama wewe wapate wasaa wa kuchangia!
Na pia ni swali!
Kwahiyo uchagga ndio kigezo gani?
Wewe unataka kuigawa nchi?
Hivi unajua nafasi ya Mengi Tanzania ama ni ile roho kutu ya ubaguzi na chuki imekujaa!?
 
Naomba tuendelee na mjadala kistaarabu ili na wale wenye uwoga wa wanyama hatari kama wewe wapate wasaa wa kuchangia!
Na pia ni swali!
Kwahiyo uchagga ndio kigezo gani?
Wewe unataka kuigawa nchi?
Hivi unajua nafasi ya Mengi Tanzania ama ni ile roho kutu ya ubaguzi na chuki imekujaa!?

Haya tuelimishe kinagaubaga hiyo nafasi "spesheli" unayodai Mengi kuwa nayo Tanzania?
 
Haya tuelimishe kinagaubaga hiyo nafasi "spesheli" unayodai Mengi kuwa nayo Tanzania?

Huyu jamaa amekuwa akipingana na mfisadi toka kitambo!
Na hata ikafikia mahali akaanza kupewa ulinzi!
Tatizo kubwa lilikuwa likimkabili na ambalo bado linamkabili ni "uchagga"
Ila ana nia nzuri!
Hana njaa!
Amesaidia watanzania wengi bila kujali dini,kabila etc! Na bila kujali malipo!
Ni mtu wa watu!
Amechangia maendelo ya wazawa kwa kiasi kikubwa sana, pia amekuwa akipewa majukumu makubwa sana tu na serikali zote zilizopita!
Na pia ana sauti Afrika!
So kwanini tusimjadili mtu kama huyu with honesty bila chuki?
 
Issue kwamba mimi ni mchagga haina maana kuwa sasa aliyofanya R.Mengi hayana maana!
Wala haina maana ya sisi kuwa waoga wa kujadili watu kwasababu tutafikiriwa vingine!
Honesty matters a lot kwenye siasa zetu za sasa!
 
Upinzani vurugu mingi..CCM ufisadi!
Sasa kuna watu ambao nao wamechoshwa na siasa!
Wanataka watu wenye vitendo!
Na Mkapa kweli naona akisikia hii issue anaweza pata presha ghafla!
Watu wanaopingana kiukweli na mafisadi ndio wanaotufaa!
Halafu aligundua Mkapa alivyokuwa akiiuza nchi na ndio maana wakafungua MKOMBOZI WA MALI ZA WATANZANIA...NICO!
Halafu kweli myama hatari unasema huyu bwana yeye ni mchagga tu na wala si Mtanzania mwenzetu mzalendo?
 
Hivi unajua NICO ni nini na ni watanzania wangapi wenye kuhodhi mali za Taifa lao through NICO?
 
Huyu jamaa amekuwa akipingana na mfisadi toka kitambo!
Na hata ikafikia mahali akaanza kupewa ulinzi!
Tatizo kubwa lilikuwa likimkabili na ambalo bado linamkabili ni "uchagga"
Ila ana nia nzuri!
Hana njaa!
Amesaidia watanzania wengi bila kujali dini,kabila etc! Na bila kujali malipo!
Ni mtu wa watu!
Amechangia maendelo ya wazawa kwa kiasi kikubwa sana, pia amekuwa akipewa majukumu makubwa sana tu na serikali zote zilizopita!
Na pia ana sauti Afrika!
So kwanini tusimjadili mtu kama huyu with honesty bila chuki?

ni mtu mzuri kwa kumjua kwa nje. Anao uzoefu wowote katika mambo ya siasa? maana kufanikiwa kibiashara sio kufanikikiwa kisiasa. Pia je una dataz zaidi kuhusu biashara zake zinazoweza kuonyesha yuko honest kiasi gani hadi aaminiwe kupewa nchi? Je unaweza kumcompare na kucontrast uwezo wake katika siasa na wanasiasa wengine wanaodhaniwa wanaweza kugombea urais 2010 kama kina slaa, SAS, mwandosya, mbowe n.k?
 
Huyu jamaa amekuwa akipingana na mfisadi toka kitambo!
Na hata ikafikia mahali akaanza kupewa ulinzi!
Tatizo kubwa lilikuwa likimkabili na ambalo bado linamkabili ni "uchagga"
Ila ana nia nzuri!
Hana njaa!
Amesaidia watanzania wengi bila kujali dini,kabila etc! Na bila kujali malipo!
Ni mtu wa watu!
Amechangia maendelo ya wazawa kwa kiasi kikubwa sana, pia amekuwa akipewa majukumu makubwa sana tu na serikali zote zilizopita!
Na pia ana sauti Afrika!
So kwanini tusimjadili mtu kama huyu with honesty bila chuki?

Unataka kuleta mambo ya Berlusconi Tanzania sio? Bepari aliyekubuhu kama Mengi mwenye kuhodhi vyombo karibia vyote vikuu vya habari (na labda pia uhuru wa habari) njaa itoke wapi? Na hizo pesa "anazochangia" kwa maendeleo ya Wazawa ni moja ya obligations zake kwa jamii ya Tanzania, kwani ukumbuke ni jamii hiyohiyo iliyodumaa kwa umasikini ndiyo imemletea utajiri wake wote. Mwenye pesa siku zote huwa anao uwezo wa kununua heshima inayofaa hadhi anayoitafuta, kwa hiyo si ajabu kwa serikali, vyombo na taasisi mbalimbali kumtunukia vyeo, medali na vikolombwezo vinginevo vinavyoendana na hadhi yake kiuchumi. Mengi ni bepari, and therefore its safe to say akiwa kama mabepari wengine wote atakuwa na mentality ya economic opportunism siku zote ili a-manipulate environment in order to make a buck.
 
Upinzani vurugu mingi..CCM ufisadi!
Sasa kuna watu ambao nao wamechoshwa na siasa!
Wanataka watu wenye vitendo!
Na Mkapa kweli naona akisikia hii issue anaweza pata presha ghafla!
Watu wanaopingana kiukweli na mafisadi ndio wanaotufaa!
Halafu aligundua Mkapa alivyokuwa akiiuza nchi na ndio maana wakafungua MKOMBOZI WA MALI ZA WATANZANIA...NICO!
Halafu kweli myama hatari unasema huyu bwana yeye ni mchagga tu na wala si Mtanzania mwenzetu mzalendo?

Nilidhani angekuwa mzalendo na kuibua hadharani hatari ya kuuzwa nchi na Mkapa, akanyamaza na kuanzisha NICO. Je tukimpa urais ataweza kuwakemea mafisadi kama alidiriki kumnyamazia fisadi Mkapa ilihali alimshamgundua kama ulivyosema? Je katika NICO ameianzisha mwenyewe?
 
Unataka kuleta mambo ya Berlusconi Tanzania sio? Bepari aliyekubuhu kama Mengi mwenye kuhodhi vyombo karibia vyote vikuu vya habari (na labda pia uhuru wa habari) njaa itoke wapi? Na hizo pesa "anazochangia" kwa maendeleo ya Wazawa ni moja ya obligations zake kwa jamii ya Tanzania, kwani ukumbuke ni jamii hiyohiyo iliyodumaa kwa masikini ndiyo imemletea utajiri wake wote. Mwenye pesa siku zote huwa anao uwezo wa kununua heshima inayofaa hadhi anayoitafuta, kwa hiyo si ajabu kwa serikali, vyombo na taasisi mbalimbali kumtunukia vyeo, medali na vikolombwezo vinginevo vinavyoendana na hadhi yake kiuchumi.

Hujanijibu kuhusu NICO!
Hivi Mkapa angekuwa na roho kama ya Mengi si tungekuwa mbali sana?
NICO ni mkombozi wa rasilimali zetu kuwekwa mikononi mwetu!
Vipi Kiwira?
Richmond?
Niendelee?
 
Nilidhani angekuwa mzalendo na kuibua hadharani hatari ya kuuzwa nchi na Mkapa, akanyamaza na kuanzisha NICO. Je tukimpa urais ataweza kuwakemea mafisadi kama alidiriki kumnyamazia fisadi Mkapa ilihali alimshamgundua kama ulivyosema? Je katika NICO ameianzisha mwenyewe?

Mama huyu jamaa anawapandishia mawaziri wazembe bila kujali!
Mkapa alikuwa Rais lakini haikumfanya asijitahidi kuokoa kile kitakachowezekana na kukirudisha mikononi mwa wananchi!
Hivi unafikiri hizi kashfa zote bila yeye tungezijua?
We unafikiri kwanini Mkapa hataki ata kusikia jina lake?
We unafikiri kwanini aliletewa gari lenye vioo vya bullet proof na kupewa ulinzi mkubwa?
Huyu ni rafiki wa fisadi kwa maoni yako?

Na kuhusu NICO no hajaianzisha mwenyewe..Kama vile ambavyo atahitaji msaada kwenye kuongoza!
 
Mama huyu jamaa anawapandishia mawaziri wazembe bila kujali!
Hivi unafikiri hizi kashfa zote bila yeye tungezijua?
We unafikiri kwanini Mkapa hataki ata kusikia jina lake?
We unafikiri kwanini aliletewa gari lenye vioo vya bullet proof na kupewa ulinzi mkubwa?
Huyu ni rafiki wa fisadi kwa maoni yako?

Na kuhusu NICO no hajaianzisha mwenyewe..Kama vile ambavyo atahitaji msaada kwenye kuongoza!

Haya yote uliyoyasema hapa juu naweza nikayakubali ama lah, do you have any supporting data? it will be good to let me know a lot about Mengi kabla sijaamua kupa kura if he will be deserving! Morever, what is his contribution to CCM? isn't he a member of Chama cha Mafisadi?
 
Mimi naona tuendeshe nchi yetu ki-ubia tu. Since tunaweza kusaini contract mbovu kwani tusiwaachie kabisa aidha makaburu au wazungu halafu sisi tufanye kazi kama punda. Maana kujiongoza tumeshindwa, kujiendeleza tumeshindwa. Na hizi contract tunazowapatia viongozi wetu waongoze miaka mitano mitano mpka ije kuisha tunajikuta tuko palepale au nyuma zaidi kila baada ya miaka mitano.....I mean, uongozi wa nchi sio sehemu ya kupatia work experience. Kwanini tusiwape wenye experience kabisa??
Dont kill me. Just a suggestion. Eti Ngabu we unaonaje ngosha?
 
Haya yote uliyoyasema hapa juu naweza nikayakubali ama lah, do you have any supporting data? it will be good to let me know a lot about Mengi kabla sijaamua kupa kura if he will be deserving! Morever, what is his contribution to CCM? isn't he a member of Chama cha Mafisadi?

Mimi nimeanzisha mjadala tu.
Yeye mwenyewe hajawahi kusema kuwa atagombea urais!
Ni wazo tu ambalo nataka tulijadili and maybe tum convince kama tukikubaliana ili tu muendorse!
Cha muhimu tumpe fair,honest and respecting discussion kwasababu hata yeye ameturespect na kutufanyia mengi wananchi na huku hata yeye akiwa si kiongozi!
Sasa tukiondoa tofauti zetu na kumpa uongozi kwanini asifanye makubwa zaidi kama akipewa ushirikiano?

Kuhusu yeye kuwa CCM hilo siwezi kumsemea.

Kuhusu supporting data nitajitahidi,ila ujue kuwa almost everybody knows what he has done to the community nationwide!
 
Mimi naona tuendeshe nchi yetu ki-ubia tu. Since tunaweza kusaini contract mbovu kwani tusiwaachie kabisa aidha makaburu au wazungu halafu sisi tufanye kazi kama punda. Maana kujiongoza tumeshindwa, kujiendeleza tumeshindwa. Na hizi contract tunazowapatia viongozi wetu waongoze miaka mitano mitano mpka ije kuisha tunajikuta tuko palepale au nyuma zaidi kila baada ya miaka mitano.....I mean, uongozi wa nchi sio sehemu ya kupatia work experience. Kwanini tusiwape wenye experience kabisa??
Dont kill me. Just a suggestion. Eti Ngabu we unaonaje ngosha?

Ni kweli kwasababu sijui hata ni vigezo gani tumekuwa tukivitumia kwenye kuchagua Rais!
Ila Mengi alijitahidi sana kuona kuwa baadhi ya rasilimali za taifa zinabaki mikononi mwa wananchi.
Unajua utaratibu wetu wa kuchagua rais hautupatii viongozi tunaowahitaji kwenye dunia ya sasa kwasababu siasa zinawaharibu!
Na kwenye historia ya dunia marais ambao wamekuwa na vipaji vingine tofauti na siasa wametokea kuwa wachapakazi hodari na honest!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom