Rungu
JF-Expert Member
- Feb 23, 2007
- 3,932
- 1,726
Mwanamuziki mpiga Bass wa DDC Mlimani Park Orchestra, ambaye alijulikana kwa jina maarufu la Ngosha atazikwa kesho saa 10 Magomeni. Ngosha alijiunga na DDC Mlimani Park miaka ya mwanzoni ya 90, akiwa anajulikana kama Charles John Ngosha, baadae alibadili dini na Kuslim na kupewa jina la Mustafa.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa Amana Hospital Ilala, na msiba utakuwa Magomeni katika maeneo ya kituo cha Bi Nyau, karibu na ukumbi wa DDC Magomeni.
Source: Wanamuziki wa Tanzania blog