R.I.P. Dr. Remmy Ongara

Mungu hahusiki jamani, hebu someni vizuri kitabu cha Ayub mtaelewa alisema maneno hayo bila ujuzi bila kufahamu kilichokuwa kikiendelea kati ya Mungu na Shetani na isitoshe katika Ayub sura za 42 alitengua usemi huo na yale yote akidhani Mungu ndiye alikuwa akimtendea. Wachungaji walitudanganya, tukafikiri Mungu anahusika katika vifo vinavyotokea. Wengine wanasema "Tulimpenda marehemu lakini Mungu kampenda sana au Mungu anavuna alichopanda. Lakini unaweza kuangalia matokeo ya vifo kwa mfano. Unaaenda kutembeza umalaya unakumbana na virus vya ukimwi baada ya muda unakufa, Mungu ndiye aliyekutuma ufanye umalaya??? si alisema mzinzi hataurithi ufalme wa Mungu sasa atakutumaje. Jambo tunapaswa kujifunza ni kwamba Mungu karuhusu kifo cha mwanadamu lakini hasababishi kifo hicho, kuna tofauti kati ya kurusu na kusababisha. Ukitaka maelezo zaidi soma kitabu cha Mhubiri.

Hivyo usemi huo tunaendelea kuutumia kimakosa. Mimi namuomba Mungu aipe nguvu za familia ya mzee Remmy kukabiliana na msiba huu kwani ni kipindi kigumu kwao cha kumpoteza mpendwa wao. Na aiangalie familia hiyo ili iendelee kupata mahitaji yake ya kila siku. Amen.

ndugu muacici, nina neno kidogo na ile comment ya kitabu cha ayubu. tafadhari zingatia kuwa kitabu cha ayubu si cha historia au mambo ya nyakati (matukio/chronicles).......... ni kitabu cha utenzi kinachokusudia kuibua asili, sifa na tabia ya Mungu.......... simulizi la shetani kama ulivyolinukuu liko katika prologe ya hicho kitabu (3-42:6). ........ na kibwagizo chake kiko kwenye epilogue yake (42:7 hadi mwisho)............ ila maudhui ya kitabu chenyewe yako sura za 3-42:6 na yameandikwa katika mtindo wa utenzi unawahusu ayubu na marafiki zake watatu (elifaaz, zofari na bildad) mwishonimwishoni anaibuka kijana mmoja mdogo lakini mwenye hekkima kubwa (elihu) kushinda hata ya ayubu na rafiki zake wote. anaongea mambo yanayokaribia kufanana na ya Mungu mwenyewe na hatimaye anasababisha ayubu akiri alipopotoka na kutubu.......... tafadhari soma taratibu na Mungu akusaidie kuelewa nasema nini na kama utapata tatizo, nitafurahi kukusaidia........... unaweza kutumia PM........... ubarikiwe..........

RIP Dr Remmy..............
 
mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi si nyingi, nazo zimejaa tabu na shida,
mwanga wa milele umuangazie eee Bwana, apumzike kwa amani, ameeeen,
 
Usiku wa kuamkia leo majira ya saa 8 usiku mwimbaji mkongwe hapa nchini ambaye kwa sasa alikuwa kaokoka na kuimba nyimbo za kwaya, dr.remmy ongalla amefariki dunia. Kwa hiyo hatunaye kwa sasa. Kama una laptop weka song lake hapo ofini kwako uanze kuomboleza.

Waitu mwikalege, omukama ababele, obahe omugisha gwe.
 
hapa nakula vibao vyake taratibuuuu kama Dole, maisha, mwanza,fadhili ni Utumwa n.k
 
remmy.jpg
 
Oooohhhh Maskini Ongalla, Mungu ailaze mahali pema roho ya marehemu amen

Bwn alitwaa na bwn ametwaa, jina lake lihimidiwe.
 
Usiku wa kuamkia leo majira ya saa 8 usiku mwimbaji mkongwe hapa nchini ambaye kwa sasa alikuwa kaokoka na kuimba nyimbo za kwaya, dr.remmy ongalla amefariki dunia. Kwa hiyo hatunaye kwa sasa. Kama una laptop weka song lake hapo ofini kwako uanze kuomboleza.

Waitu mwikalege, omukama ababele, obahe omugisha gwe.

Baada ya kuokoka , aliwahi kushuhudia kwamba alikuwa anatumia mizimu kupata nyota na mara kadhaa alikuwa akinywa damu ya binadamu.
Hata hivyo, hajawahi kusema damu hiyo alikuwa anaipata wapi.
Tatizo la damu za siku hizi , ukute alikunywa yenye virusi....
Anyway, RIP Ongala, nyimbo zako nilikuwa nazipenda sana, kama vile Mola nalilia mtoto, Narudi Songea, Nakulilia Mola wangu nk.......
 
Baada ya kuokoka , aliwahi kushuhudia kwamba alikuwa anatumia mizimu kupata nyota na mara kadhaa alikuwa akinywa damu ya binadamu.
Hata hivyo, hajawahi kusema damu hiyo alikuwa anaipata wapi.
Tatizo la damu za siku hizi , ukute alikunywa yenye virusi....
Anyway, RIP Ongala, nyimbo zako nilikuwa nazipenda sana, kama vile Mola nalilia mtoto, Narudi Songea, Nakulilia Mola wangu nk.......

Tusihukumu, sote tuko safarini dr. Remmy Ongala pamoja na mapungufu yake yote yeye ndio kautangaza Muziki wa TZ kuliko mwanamuziki yeyote yule. Amefariki kutokana na matatizo ya figo yaliosababishwa na ugonjwa wa kisukari na sio kunywa damu za watu
 
Back
Top Bottom