Mungu hahusiki jamani, hebu someni vizuri kitabu cha Ayub mtaelewa alisema maneno hayo bila ujuzi bila kufahamu kilichokuwa kikiendelea kati ya Mungu na Shetani na isitoshe katika Ayub sura za 42 alitengua usemi huo na yale yote akidhani Mungu ndiye alikuwa akimtendea. Wachungaji walitudanganya, tukafikiri Mungu anahusika katika vifo vinavyotokea. Wengine wanasema "Tulimpenda marehemu lakini Mungu kampenda sana au Mungu anavuna alichopanda. Lakini unaweza kuangalia matokeo ya vifo kwa mfano. Unaaenda kutembeza umalaya unakumbana na virus vya ukimwi baada ya muda unakufa, Mungu ndiye aliyekutuma ufanye umalaya??? si alisema mzinzi hataurithi ufalme wa Mungu sasa atakutumaje. Jambo tunapaswa kujifunza ni kwamba Mungu karuhusu kifo cha mwanadamu lakini hasababishi kifo hicho, kuna tofauti kati ya kurusu na kusababisha. Ukitaka maelezo zaidi soma kitabu cha Mhubiri.
Hivyo usemi huo tunaendelea kuutumia kimakosa. Mimi namuomba Mungu aipe nguvu za familia ya mzee Remmy kukabiliana na msiba huu kwani ni kipindi kigumu kwao cha kumpoteza mpendwa wao. Na aiangalie familia hiyo ili iendelee kupata mahitaji yake ya kila siku. Amen.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.