MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,603
Vile vipindi vya Pwagu na Pwaguzi viliishia wapi?
Vilikuwa vinaburudisha na kufunza. Wale wazee walikuwa mahiri kweli.
Mimi nakumbuka kisa kimoja hiki:
"Pwagu alimshitaki Pwaguzi kuwa alimrembea rungu ikampasua kichwa. Katika kesi ili kuwa hivi:
HAKIMU: Bwana Pwaguzi, unasema Pwagu alikurembea rungu ukaumia kichwani ni kweli?
PWAGUZI: Muheshimiwa Bwana Hakimu ni kweli, ushahidi jeraha hili hapa.
HAKIMU: Pwagu una lipi la kusema?
PWAGU: Naomba kumhoji mdai, Bwana Hakimu, kwa ruhusa yako. [Hakimu anatoa ruhusa ya kuhoji].
PWAGU: Unasema nilikurembea rungu, uliniona?
PWAGUZI: Nilikuona.
PWAGU: Nilikuwa umbali gani?
PWAGUZI: Ulikuwa karibu sana, na ndio maana rungu ikatua juu ya kichwa changu.
PWAGU: Uliona kuwa nimekamata rungu mkononi?
PWAGUZI: Ndiyo!
PWAGU: Uliona jinsi nilivyokuwa ninajitayarisha kukurembea rungu hilo?
PWAGUZI: Ndio nilikuona, nilikuwa ninakuangalia shahidi macho yangu.
PWAGU: Nilipokurembea ulilikwepa?
PWAGUZI: Sikulikwepa!
PWAGU (Kwa Hakimu): Bwana Hakimu, mdai anasema aliniona nimekamata rungu mkononi, nikijitayarisha kulirembea, yeye ananitazama tu, nikamrembea nalo, yeye ananiangalia tu; Huoni Bwana Hakimu Pwaguzi alikuwa ananitega kwa makusudi nimrembee nalo?
HAKIMU: Pwaguzi, inaonesha ulikuwa unamtega mwenzako kwa makusudi. Kesi Dismiss.
Unakumbuka kisa gani cha Pwagu na Pwaguzi?
Vilikuwa vinaburudisha na kufunza. Wale wazee walikuwa mahiri kweli.
Mimi nakumbuka kisa kimoja hiki:
"Pwagu alimshitaki Pwaguzi kuwa alimrembea rungu ikampasua kichwa. Katika kesi ili kuwa hivi:
HAKIMU: Bwana Pwaguzi, unasema Pwagu alikurembea rungu ukaumia kichwani ni kweli?
PWAGUZI: Muheshimiwa Bwana Hakimu ni kweli, ushahidi jeraha hili hapa.
HAKIMU: Pwagu una lipi la kusema?
PWAGU: Naomba kumhoji mdai, Bwana Hakimu, kwa ruhusa yako. [Hakimu anatoa ruhusa ya kuhoji].
PWAGU: Unasema nilikurembea rungu, uliniona?
PWAGUZI: Nilikuona.
PWAGU: Nilikuwa umbali gani?
PWAGUZI: Ulikuwa karibu sana, na ndio maana rungu ikatua juu ya kichwa changu.
PWAGU: Uliona kuwa nimekamata rungu mkononi?
PWAGUZI: Ndiyo!
PWAGU: Uliona jinsi nilivyokuwa ninajitayarisha kukurembea rungu hilo?
PWAGUZI: Ndio nilikuona, nilikuwa ninakuangalia shahidi macho yangu.
PWAGU: Nilipokurembea ulilikwepa?
PWAGUZI: Sikulikwepa!
PWAGU (Kwa Hakimu): Bwana Hakimu, mdai anasema aliniona nimekamata rungu mkononi, nikijitayarisha kulirembea, yeye ananitazama tu, nikamrembea nalo, yeye ananiangalia tu; Huoni Bwana Hakimu Pwaguzi alikuwa ananitega kwa makusudi nimrembee nalo?
HAKIMU: Pwaguzi, inaonesha ulikuwa unamtega mwenzako kwa makusudi. Kesi Dismiss.
Unakumbuka kisa gani cha Pwagu na Pwaguzi?