Pump za maji kwa ajili ya umwagiliaji.

Red Giant

JF-Expert Member
Mar 9, 2012
15,658
20,885
Wakuu naomba mtu mwenye ujuzi nazo anisaidie. Nataka kujua pump yenye uwezo wa kuvuta maji kina cha mita 10 na kumwagilia ekari mbili inaweza kugharimu kiasi gani? Pia nilitaka kujua kama kilimo kwanza wanauza na hizi pump. Natanguliza shukrani.
 
Wakuu naomba mtu mwenye ujuzi nazo anisaidie. Nataka kujua pump yenye uwezo wa kuvuta maji kina cha mita 10 na kumwagilia ekari mbili inaweza kugharimu kiasi gani? Pia nilitaka kujua kama kilimo kwanza wanauza na hizi pump. Natanguliza shukrani.

Kuna pump inatumia mafuta (petroli) yenye uwezo wa ku-pump lita 500 kwa dakika.
Ina uwezo wa kupeleka maji mita 30 (horizontal), na kupandisha maji juu (max. head) mita 20.
Ni pump ya kichina inauzwa sh.300,000. Ina connection ya bomba la inch 2.
Kama uko Dar es Salaam, kuna duka liko karibu na stesheni, karibu kabisa na ofisi za TRA stesheni.
Maelezo zaidi utayapata kwa jamaa webnyewe wanaoziuza hapo dukani.

Pump yenyewe inafanana na hii hapa (lakini sio hii).
product1_2397.jpg
 
Hapa kuna taarifa muhimu zinakosekana. Unalima zao gani- Kila zao lina mahitaji tofauti ya maji. Na utamwagilia kwa njia ipi? Kama ni kwa mirija au kwa mifereji. Na shamba lako liko umpali gani toka chazo cha maji (je kuna mlima? Ukijibu haya itakuwa rahisi kukushauri aina ya pampu.
 
Kama vipi nenda TUNAKOPESHA Ltd (kama bado wapo hewani) siku zote huwa wanakopesha pump. Wanazo pump imara sana aina ya JD.
 
Kuna pump inatumia mafuta (petroli) yenye uwezo wa ku-pump lita 500 kwa dakika.
Ina uwezo wa kupeleka maji mita 30 (horizontal), na kupandisha maji juu (max. head) mita 20.
Mkuu nataka kuamini kuwa ulikusudia kuandika/kusema mita 300!
 
Mkuu nataka kuamini kuwa ulikusudia kuandika/kusema mita 300!

Hapana, hii pump ni ndogo ndio maana bei yake ni ndogo, hivyo inapeleka maji mita 30 tu (horizontal).
Pum hizi ndogo jamaa wanazitumia kutolea maji mtoni ili kuyapandisha na kuyafikisha shambani. Baada ya hapo, maji yanasambaa shambani kwa mifereji ya umwagiliaji.
Kuna pump nyingine kubwa zinapeleka maji mita 100 (horizontal) na kupandisha maji juu (max. head) mita 50.
 
Hapana, hii pump ni ndogo ndio maana bei yake ni ndogo, hivyo inapeleka maji mita 30 tu (horizontal).
Pum hizi ndogo jamaa wanazitumia kutolea maji mtoni ili kuyapandisha na kuyafikisha shambani. Baada ya hapo, maji yanasambaa shambani kwa mifereji ya umwagiliaji.
Kuna pump nyingine kubwa zinapeleka maji mita 100 (horizontal) na kupandisha maji juu (max. head) mita 50.

Hivi kuna kikomo cha kusukuma maji "horizontally"? au hii ni kama unasukuma maji "horizonally" na "vertically"?
 
Hivi kuna kikomo cha kusukuma maji "horizontally"? au hii ni kama unasukuma maji "horizonally" na "vertically"?

Kipimo cha kusukuma maji horizontally kipo. Jinsi umbali (horizontal distance) unavyoongezeka, ndio inahitaji pump yenye nguvu zaidi kusukuma maji.
Maji yakiwa kwenye bomba ambalo liko horizontal yanahitaji nguvu ya kuyapeleka mbele, hivyo umbali unavyoongezeka ndio mzigo wa maji unapokuwa mkubwa ndani ya bomba, na hivyo kuhutaji nguvu kubwa zaidi kutoka kwenye pump.
 
nashukuru wadau kwa kutujuza taarifa hizi za muhimu. MIMI NINAHITAJI KUJUA KAMA NINAWEZA PATA PUMP YENYE UWEZO WA KUVUTA MAJI KILOMETA KAMA MOJA NA NUSU KUTOKA KWENYE CHANZO CHA MAJI. GHARAMA KWA UJUMLA PAMOJA NA PIPE NDEFU KIASI HICHO NI SHILINGI NGAPI? NATANGULIZA SHUKURANI.
 
Jamani mmi nina shamba liko maeneo ya hai masama rundugai, shamba hili linataka pamp ili uweze kupandisha maji kutoka mtoni hadi shambani na mto huo haukauki maji. Naomba mweye uwezo wa kuapata pamp na mipira ya nch 4 tuwasiliane kwa mob: Tukalime tujikwamue na umasikini
 
Guys, somo zuri sana. Nawafuatilia kwa makini kwani na mimi napata somo. Thanks for your valuable inputs.
 
Jamani mmi nina shamba liko maeneo ya hai masama rundugai, shamba hili linataka pamp ili uweze kupandisha maji kutoka mtoni hadi shambani na mto huo haukauki maji. Naomba mweye uwezo wa kuapata pamp na mipira ya nch 4 tuwasiliane kwa mob: Tukalime tujikwamue na umasikini

Rundugai ndo wapi?
 
Hongereni sana kwa wale mnaotaka kujiunga na Kilimo cha umwagiliaji....Mimi sina utaalam sana ila naweza nikachangia kitu kwenye hii mada...jaribu kupitia hizi pump below..ni nzuri sana
1.WT40XK3C...Honda trash pump kama shamba lako ni kubwa...4inch
2.Honda WT30XK4C...3inch
3.Honda WH20X high pressure water pump...2inch
4. Honda WB30...3inch
hizo pump kuna ya 4m hadi ya 1m..hizo ndo pump nzuri kwa mashamba ya kuanzia ekari tano..Mashamba yanamwagiliwa kwa mifereji..yaani unakuwa na point moja(center) ambapo utakuwa unapump hayo maji, afu from there unayasafirisha kwa mfereji..hiyo point jitahidi iwe katikati au sehemu yenye muinuko zaidi katika shamba lako..
Unaweza kuzipata hizo pump kwenye duka la Honda lililopo kariakoo, lipo karibu na zilipokuwa ofisi za scandnavia..
Kumbuka, kama unataka kufanya kilimo cha umwagiliaji kitu cha kwanza muhimu ni ubora wa pump..nakushauri achana na pump za kichina kama pesa yako ni yakuunga unga maana zinahitaji maintenance za mara kwa mara...they look cheap but they r expensive...
Ukiweza pata pump za Diesel ni much better
 
nashukuru wadau kwa kutujuza taarifa hizi za muhimu. MIMI NINAHITAJI KUJUA KAMA NINAWEZA PATA PUMP YENYE UWEZO WA KUVUTA MAJI KILOMETA KAMA MOJA NA NUSU KUTOKA KWENYE CHANZO CHA MAJI. GHARAMA KWA UJUMLA PAMOJA NA PIPE NDEFU KIASI HICHO NI SHILINGI NGAPI? NATANGULIZA SHUKURANI.

Kwa umbali huo unaweza kupata pump hiyo maana hakuna lisilowezekana. Cha muhimu kuzingatia si umbali pekee bali kiasi cha mwinuko kilichopo toka kilipo chanzo cha maji! Kama ni mwinuko mkubwa utahitajika kuwa na pump yenye nguvu sana. Siyo rahisi kukadiria bei ya pump kwa vile inategemea na mwinuko. Kwa umbali huo na mwinuko huo jiweke kwenye makadirio ya Millioni 2 hadi 4 kwa kuzingatia figure za Mkuu Mateshi hapo juu. Kwa umbali huo unahitajika kuwa na Tsh Milioni 1.5 kwa kununua mpira wa 3". Au unaweza kutumia pump ndogo unajenga tanki kubwa kwenye chanzo cha maji, pump inalijaza tanki hilo na ule mkandamizo wa maji kwenye tanki unayasukuma maji kwenda shambani kwako. Pump ndogo kujaza tanki zinauzwa laki 3/4. Ila mziki uko kwenye kutengeneza tanki ambapo utajikuta umerudi kule kule sawa na kununua pump ya bei kubwa.
 
Hongereni sana kwa wale mnaotaka kujiunga na Kilimo cha umwagiliaji....Mimi sina utaalam sana ila naweza nikachangia kitu kwenye hii mada...jaribu kupitia hizi pump below..ni nzuri sana
1.WT40XK3C...Honda trash pump kama shamba lako ni kubwa...4inch
2.Honda WT30XK4C...3inch
3.Honda WH20X high pressure water pump...2inch
4. Honda WB30...3inch
hizo pump kuna ya 4m hadi ya 1m..hizo ndo pump nzuri kwa mashamba ya kuanzia ekari tano..Mashamba yanamwagiliwa kwa mifereji..yaani unakuwa na point moja(center) ambapo utakuwa unapump hayo maji, afu from there unayasafirisha kwa mfereji..hiyo point jitahidi iwe katikati au sehemu yenye muinuko zaidi katika shamba lako..
Unaweza kuzipata hizo pump kwenye duka la Honda lililopo kariakoo, lipo karibu na zilipokuwa ofisi za scandnavia..
Kumbuka, kama unataka kufanya kilimo cha umwagiliaji kitu cha kwanza muhimu ni ubora wa pump..nakushauri achana na pump za kichina kama pesa yako ni yakuunga unga maana zinahitaji maintenance za mara kwa mara...they look cheap but they r expensive...
Ukiweza pata pump za Diesel ni much better

Mkuu pump gani zinafaa kwa kisima cha chini kama 80m-100M? kwa ajili ya umwagiliaji?
 
Kwa umbali huo unaweza kupata pump hiyo maana hakuna lisilowezekana. Cha muhimu kuzingatia si umbali pekee bali kiasi cha mwinuko kilichopo toka kilipo chanzo cha maji! Kama ni mwinuko mkubwa utahitajika kuwa na pump yenye nguvu sana. Siyo rahisi kukadiria bei ya pump kwa vile inategemea na mwinuko. Kwa umbali huo na mwinuko huo jiweke kwenye makadirio ya Millioni 2 hadi 4 kwa kuzingatia figure za Mkuu Mateshi hapo juu. Kwa umbali huo unahitajika kuwa na Tsh Milioni 1.5 kwa kununua mpira wa 3". Au unaweza kutumia pump ndogo unajenga tanki kubwa kwenye chanzo cha maji, pump inalijaza tanki hilo na ule mkandamizo wa maji kwenye tanki unayasukuma maji kwenda shambani kwako. Pump ndogo kujaza tanki zinauzwa laki 3/4. Ila mziki uko kwenye kutengeneza tanki ambapo utajikuta umerudi kule kule sawa na kununua pump ya bei kubwa.

mkuu nashukuru sana maana ni kitambo nimekuwa nikisubiri feedback kama hizi. ngoja nikajaribukufanya detailed research then niangalie ni njia hipi ni sahhi zaidi katika kufanikisha hili.
ahsante. Maana nikikuwa nahofu juu ya bei ya mpira utakao range umbali ambao niiukadilia.
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom