Propaganda za uongo: Elimu bure, CHADEMA ikishinda

Wewe binti Ngoda hizi data zako walakini kabisa:

Mkoa wa Kilimanjaro unaongoza Tanzania nzima kwa kuwa na shule za Sekondari nyingi kuliko mikoa yote ya Tanzania. Una sekondari 288 wakati hata Dar es salaam ina sekondari 252 tu (Chanzo: www.moe.go.tz/NectaResuls). Wakazi wa kilimanjaro ni 1441000 ukilinganisha na Dar es salaam ambao ni takriban 2,809,000 (Chanzo: Tanzania: Regions, Major Cities & Urban Localities - Statistics & Maps on City Population).

Hizi shule ni za kata ama ni zipi? halafu la muhimu ni idadi ya shule au iadadi ya wanafunzi? je hujuwi kuwa kutokana na shida za usafiri wazazi wengi watoto wao wanasoma mikoani hasa huo mkoa wa kilimanjaro?

Pato la kodi la mkoa wa Kilimanjaro (Rombo, Hai, Mwanga, Same, Mosho mjini na Moshi vijijini) ni 14,236.4 Milioni (Tzsh) wakati lile la Dar es salaam ni 441,000.5 Milioni (Tzsh) (Chanzo:
Tanzania Revenue Authority - Kigoma). Kigoma na Kilimanjaro wapi na wapi?

Kabla sijaandika zaidi naomba huyu waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA akisaidiana na wapambe wake hapa JF wanieleze ni vipi watazigawanya hizo14,236.4 milioni Tzsh katika huduma za matibabu (hospitali, zahanati na elimu ya afya), Polisi, utawala mkoa na wilayani, pembejeo, na Elimu(mishahara ya walimu, ukarabati na stationaries).

Ni nani aliyekwambiakuwa pato la mkoa hutumika kwa maendeleo ya mkoa? ULISHAWAHI KUSIKIA MKOA UPI UKIPITISHA BAJETI YAKE ? Je hujui kuwa hilo pato la mkoa wa Dar es Salaam linajumuisha wakaazi wa mko wa Kilimanjaro pia?

Mkishindwa kufanya hivyo maana yake ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE NI PROPAGANDA YA UONGO. Vinginevyo mlitaka kutumia pesa ya walipa kodi wa mikoa mingine kuendeleza mkoa wenu maana kiuchumi haiwezekani Kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe na shule kupita Dar es salaam yenye wakazi 2,809,000.

Sasa wewe mwenyewe umekiri kuwa mkoa wa Kilimanjaro umeendelea kwa kuwa na shule nyingio kuliko Darisalama yako. Hiyo peas ingepelekwa wapi tena? Msuya alipojenga kule kwao Mwanga(Kilimanjaro hiyohiyo) alikuwa Chadema? Kikwete anavyojenga Bagamoyo yuko Chadema?


CAMARADERIE acha Jazba. Kwanza hizo data za kodi ni za Kilimanjaro- ila nilipokopi chanzo nilikuwa nimepele kambele ukurasa. pato la Kigoma ni dogo zaidi.

Shule za kata, walimu hulipwa mishahara na nani? Tafadhali jibu swali hili ni muhimu sana katka kuendeleza mjadala

Bajeti ya taifa hutokana na kodi zikusanywazo mikoani na sio kuwa zinatoka mbinguni. Hivyo unapopiga bajeti yako (japo ni centralised) lakini ili kuwa mhalisia ni vyema uangalie kuwa umeingiza ngapi na umetumia ngapi. Ni lazima ujue na lazima uzingatie sana kuwa hizi pesa zinatoka kwanza mikoani kwenda makao makuu. Hivyo kama wewe ni mchumi mzuri ni vyema kuelewa kuwa ulipopewa pesa toka makao makuu umepata zaidi ya ulichoingiza au chini ya ulichoingiza. Pili, matumizi yako ni zaidi ya ulichoingiza au ni chini ya ulichoingiza. Hivyo ndivyo uchumi unavyokwenda.

Samahani hoja yako ya mwisho sijaielewa mantiki yake hivyo sitaijibu.
 
Mwalimu NYerere alitoa elimu bure, matokeo yake baada ya miaka 20 nchi ilitembelea magoti. CHADEMA (Mh Slaa) japo ya kujua hilo bado ilisisitiza kutoa Elimu bure kwa watanzania wote ili ishinde uchaguzi 2010, lakini ikaanguka. Hii ni kutokana na ueleo mkubwa wa watanzania na kuelewa kuwa hizo ni PROPAGANDA ZA UONGO.

Wiki iliyopita nilipoandika Thread "CHADEMA NI CHAMA CHA PROPAGANDA" wengi walidai nilete ushahidi au vyanzo vya taarifa hizo. Sikufanya hivyo kwa kuogopa Mod kuifuta habari hiyo. Leo nimeamua kuandika ushahidi wa Propaganda hizo za uongo tukianzia kwenye kipengele cha ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE.

Ili twende hatua kwa hatua naona vyema tuanzie na mkoa wa Kilimanjaro ambako ndio Ngome ya CHADEMA ilikojikita. Naomba waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA aeleze kinaga ubaga ni vipi kwa kutumia kodi ya mkoa wa Kilimanjaro itamudu kutoa elimu bure kwa wananchi wa mkoa huo kabla hatujazungumzia Tanzania nzima.

Mkoa wa Kilimanjaro unaongoza Tanzania nzima kwa kuwa na shule za Sekondari nyingi kuliko mikoa yote ya Tanzania. Una sekondari 288 wakati hata Dar es salaam ina sekondari 252 tu (Chanzo: www.moe.go.tz/NectaResuls). Wakazi wa kilimanjaro ni 1441000 ukilinganisha na Dar es salaam ambao ni takriban 2,809,000 (Chanzo: Tanzania: Regions, Major Cities & Urban Localities - Statistics & Maps on City Population). Pato la kodi la mkoa wa Kilimanjaro (Rombo, Hai, Mwanga, Same, Mosho mjini na Moshi vijijini) ni 14,236.4 Milioni (Tzsh) wakati lile la Dar es salaam ni 441,000.5 Milioni (Tzsh) (Chanzo: Tanzania Revenue Authority - Kigoma).

Kabla sijaandika zaidi naomba huyu waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA akisaidiana na wapambe wake hapa JF wanieleze ni vipi watazigawanya hizo 14,236.4 milioni Tzsh katika huduma za matibabu (hospitali, zahanati na elimu ya afya), Polisi, utawala mkoa na wilayani, pembejeo, na Elimu (mishahara ya walimu, ukarabati na stationaries).

Mkishindwa kufanya hivyo maana yake ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE NI PROPAGANDA YA UONGO. Vinginevyo mlitaka kutumia pesa ya walipa kodi wa mikoa mingine kuendeleza mkoa wenu maana kiuchumi haiwezekani Kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe na shule kupita Dar es salaam yenye wakazi 2,809,000.

Nasubiri majibu yenu kabla sijaendelea na sekta nyingine.

Ninyi kila kitu hakiwezekani tu. Umeme Shida, maji Mgao, Barabarani foleni kuiondoa nayo haiwezekani. kila kitu hakuna mmekalia kudandia hoja za CHADEMA tu ndio maana mmeanza kushona hata kombati

Ukishakuwa na akili mgando huwezi kuwaza nje ya sanduku. (Thinking out of the Box). Ninyi CCM mkishadanganyana kuwa Elimu bure haiwezekani mnaona kweli.

Hili taifa limenufaika vipi na rasilimali zake? Ukianza na Soko (yaani watu). Tuna watu wengi lakini tunawanufaisha wachina kwa sababu hatuzalishi. Hata tooth pick tuna import, ujinga gani huu.

Kuna Ardhi, mito, maziwa, Madini, wanyama pori na wa kufuga. Hivi vyote vingechangia katika pato la Taifa, pia tukawa na uzalishaji wa ndani wa viwanda kutosheleza angalau 80% ya soko la ndani, unadhani ELIMU BURE HAIWEZEKANI japo kwa msingi na sekondari ambapo watoto wanalipa ada ya 20,000 to 40,000.

Acha ujinga Bhana... ala, JF sio mabwegwe ni Home of great thinkers.
 
Bado unajaribu kutumia akili ya Upinzani kuuliza swali. Chadema hata wakikupa maelezo yao maadam wewe unapoingana na sera zao huwezi kuona inawezekana! lazima utaona mapungufu upande wa pili kwa sababu sera zako ni pinzani.
Kwa mfano Chadema wakisema, watapunguza mishahara ya wanasiasa haswa rais, Mawaziri, Wabunge, Kuondoa kabisa manunuzi ya mashangingi na posho za vikao vya bunge, kupunguza gharama za safari na misafara ya rais na mawazirii zisokuwa lazima na kadhalika..Je, utaweza kuelewa na kutoshelezwa?

Hivi vyote, bado hutaelewa kitu kwa sababu huelkewi ni kiasi gani kitakusanywa kutokana na hayo, halafu utaanzisha Ubishi ktk sera ambazo hukubaliani na baadhi ya maamuzi kutokana na mtazamo wako. Halafu, tuacha kuwa wana Chadema au CCM, binafsi naamini kabisa inawezekana kama tukianza na kurekebisha sehemu muhimu za ukusanyaji wa kodi. TRA ifanyiwe marekebisho makubwa sana ktk utendaji kazi wake, iwezeshwe kwa vifaa vya kimataifa. Kila mwananchi awe na TIN namba yake - iwe lazima na ndicho kitambulisho.. Kodi ikishushwa na kuwa asilimia 10 hadi 15. KIla mapato yalipiwe kodi ktk transaction zote zenye kurekodiwa..Nina hakika wananchi na wafanyabiashara wengi watalipa kodi halali kuliko sasa hivi wanapotozwa kodi kubwa sana hivyo hupitia mlango wa nyuma. Kwa kutoza asilimia 10 serikali itaweza kukusanya zaidi pato la taifa kuliko leo hii bila ongezeko la uzalishaji. Licha ya hivyo less than 3 millioni ya wananchi ndio wanalipa kodi hata ukichukua hesabu ya watu wote waliojiandikisha kupiga kura - Hii ni aibu kwa nchi!

Moja ya sababu kubwa za Udini nchini zimetokana na mfumo tenge wa ELIMU..Mtazungumza yoote mnayoweza kuyasema lakini kwa mfumo wa ELIMU uliopo leo hii nchini, Udini utazidi kupata nguvu kubwa sana na pengine hata itakuja tokea vita. Nawasoma watu wote wanavyoandika hapa JF wenye jazba na majigambo, wengine matusi mazito mazito kwa sababu hakuna tsababu ya ujenzi wa chuki baina ya Muislaam na Mkristu isipokuwa kupitia Elimu..

JK sio sababu ya Udini nchini, yeye anatumia Udini uliopo kwa manufaa yake. Kwa wananchi wasiokuwa na Udini, JK hawezi kuwachonganisha atachekesha.. Hivyo nitawakumbusha tena Udini nchini Tanzania unatokana na mfumo wa elimu duni uliopo unatuathiri sote wazawa Waislaam kwa wakristu wakati wageni wanachukua nafasi hizi kutawala uchumi wetu..

Hapana, sitakataa ukinieleza mipango yenu. Namba hazidanganyi hata siku moja. Ukinieleza kuwa utakusanya jumla ya sh 100 hapa na pale, na utatumia sh 90 hapo sina ubishi, na haya ndio mahesabu ninayoyaomba hapa JF. Lakini ukasema kuwa utakusanya sh 100 na utatumia sh 110, hapo tutahitilafiana. Ninachohitaji ni kujua jinsi CHADEMA walivyojipanga kupata mapato na matumizi yake katika mahesabu ya karibu ya mwananchi.

Ukisema tutapunguza mishahara ya wabunge na viongozi wa serikali, ok. Lakini ninachohitaji kujua mimi ni NAMBA kuwa katika mapunguzo hayo utakusanya sh ngapi. Ninachotaka kuepuka ni kuzungumzia kuserve sh mil 100 wakati matumizi tunayoyazungumzia ni sh mil 200.

Mategemeo yangu ni kwamba mjadala ungekuwa wa kiuchumi zaidi kuliko wa kisiasa, pamoja na kuwa maamuzi ya kisiasa ndio yataongoza mfumo husika.

Kifupi bado sijapata kile nilichokitegemea huenda baadae kidogo.
 
hayo mapato ya kilimanjaro ni makusanyo ya mafisadi ccm,mapato ya chadema ni mara tano ya hayo .
halafu piga hesabu ya wanafunzi wanaonyanyasika na elfu ishirini za kata uone kama serikali ikilipa itatumia sh ngapi?
kuhusu kilimanjaro kuwa na shule nyingi waulize ccm ndio waliioongoza nchi kwa kipindi hicho chote.

kuhusu nyerere na uganda kila kitu kinajulikana alitumia rasilimali za nchi kumwokoa rafiki yake obote na hayo ndiyo chadema wanalalamikia sasa wewe na akili yako ndogo ukafikiri alishindwa kuongoza kwa sababu ya kulipia elimu bure\?sikulaumu kwani ndio vijana wa green guard na akili zenu za kuua watu.
hata hapa nafikiri unatafuta watu wa kuuwa ila nikupe pole wachangiaji wote hapa ni watoto wa mjini hamuwezi kuuuwa hata mmoja na mafunzo yenu ya singida misigiri.


Hayo mapato ya CHADEMA ndio ninayoyahitaji. Nakupongeza, kwani hakuna mjinga atayekata pato lake kuongezeka mara TANO, VIZURI.

Ninachokuomba lete data kivuli ili tujaribu kuona uhakika wake. Poteza muda kidogoulete hesabu makini zaidi, kuliko kusema tu mara 5.

Hata mzee Mapesa, japo ya kuahidi mapesa lakini urais hakuupata kwa sababu watanzania si wajinga hivyooooooo.
 
Sikutegemea mjadala makini kama huyu asitokee hata mtu mmoja kuja na data mahsusi zinavyoonyesha jinsi elimu ingetolewa bure. Nimesikitishwa sana kwa vile baada ya kuangalia vigezo halisi wengi wameumizwa na kuitaja Kilimanjaro na wengine wameenda mbali zaidi na kuiita THread kama ina mlengo wa kiudini. Nashukuru kwa vile wengi hawakuliunga mkono hili la udini kwa vile thread haipo huko kabisa.

Pengine ni vyema nieleze kwanini nimeuchagua mkoa wa Kilimanjaro. Sababu ya kwanza ni kuwa huu ni mkoa wa kwanza kuongoza kwa shule nyingi za sekondari. Hivyo kuweka sawa ni vipi elimu itatolewa bure katika mkoa huu ingekuwa ni kipimo. Pili ndiko ngome ya CHADEMA ILIKO hivyo wakereketwa wataweza kujibu hoja husika kwa data nzuri.

Kwa nini mkoa wa Dar, Ni kitovu cha mkusanyiko wa watu wengi (wakazi). Pili ni ya pili kwa sekondari nyingi baada ya Kilimanjaro. Tatu inaongoza kwa ulipaji kodi.

Nimekatishwa tamaa sana na wana CHADEMA, kwasababu baada ya kujadili mada wamekuja na jazba na kutupilia mbali kabisa kiini cha mazungumzo. Sijui huko tuendako tutafika vipi.

Mkononi mwangu nina Thread 10 zonye vyanzo zinazoeleza Propaganda za CHADEMA za uongo, lakini swali ni vipi tutazijadili kwa kina na marefu ili wasomaji waelewe kile mlichokikusudia katika Propaganda hizo.

Hata hivyo sijakatishwa tamaa, kwani safari ijayo nitakuja na mada ya "PROPAGANDA ZA UWEKEZAJI NCHINI" ikifuatiwa na "MATUMIZI YA RUZUKU NDANI YA CHAMA". Nina nyaraka ya hizo zote na nafikiri mtapevuka katika kujadili. Si suala la siasa ni hali halisi.
 
SWALI KWA MLETA MADA: Unajua migodi ya Tz samax,buzwagi nk. inatoa madini kiasi gani kwa siku? je, sirikali inajua?
 
yaani na ukubwa wako na ndevu zote hizo hujui kwa nini Nyerere alienda kupigana na Uganda? hujafoji vyeti wewe kweli?
akili masaburi hii

I normally don't read official version of the story..

I am independent thinker

Not yet programmed as they did to you..

Think out of box, it will helpful for your brain
 
why sell shares and not this? - YouTube

Kwenye ilani CDM walisema posho pekee zingeweza ku-fund education. I agree
Kwenye bajeti yao kivuli hawakuzungumzia ufutwaji wa posho za wabunge na viongozi wa serikali (only sitting allowance ambayo haitatosheleza)
Mtaji wao, kama ilivyo CCM ni ujinga wa watanzania..... but time is running out.
 
SWALI KWA MLETA MADA: Unajua migodi ya Tz samax,buzwagi nk. inatoa madini kiasi gani kwa siku? je, sirikali inajua?

Tatizo la mikataba ya madini li wazi. Si wana CCM si vyama pinzani haviungi mkono. Tatizo lililopo ni kwamba kuvunja mikata hivyo watanzania tutalipa gharama kubwa sana kama tulivyofanywa Dowans. Na matatizo kama hayo yapo nchi zote za Afrika jaribu kufanya utafiti.

Hawa wenzetu wa nchi za ulaya ni wezi, kwa bahati mbaya wanaishi kwa mtindo huo. Hakuna kingine ni kuendeleza mapambano tu, hasa kipindi hiki wakati uchumi wao uko hatarini.
 
Baada ya kusoma hoja za wanachadema, nimefikia hitimisho kuwa Chama cha Upinzani Tanzania bado hakipo. Mtaji wa CHADEMA ni UJINGA WA WATANZANIA. Na ushindi wao unategemea sana Propaganda Za Uongo.

Ni vipi wanachadema siku nzima washindwe kuitolea hoja ya kiuchumi mpango wa Elimu Bure zaidi ya kusema tu unawezekana. Aliyekuja karibu sana ni yuyle aliyeeleza jumla ya michango kuwa ni 34 bil wakati gharama kamili ni 300 bil. Hongera kwa data hizo!

Lakini lengo la taifa ni kusaidiana na gharama za ada zitawekwa kutokana na uwezo wa wazazi- Huu ni mwanzo na kadiri uchumi kwa kila mwananchi utaongezeka na kiwango kitaongezeka. Hivyo nia si kurudi nyuma bali ni kusoga mbele ili mwananchi ahisi uchungu kidogo na aonyeshe jinsi anavyoweza kulisaidia Taifa hili. Kumbuka ni vyema kujiuliza ni vipi wewe umelisaidia Taifa na si kila mara kuuliza ni jinsi gani Taifa limekusaidia.

Siasa za CHADEMA NI za kuwaweka watanzania kama viwete na kwamba CHADEMA watafanya yote watanzania walale tu. Huu ni uongo uliokithiri.
Watanzania wameamka, msipoangalia mtabezwa vibaya uchaguzi ujayo.
 
wana jf ogopeni sana udini utatupotezea dhamira ya ukombozi wa tz. We Zawadi ya ujinga ngoda kaanze darasa la kwanza kwani uwezo wako wa kufikilia unazidiwa kabisa na mtoto wangu ambaye haja anza masomo bado
 
Huhitaji shule! Hivi wewe uko makini?

Unajua itaigharimu kiasi gani Mkoa wa Kilimanjaro kutoa Elimu bure kwa shule 288. Kweli Waafrika uchumi hawaujui. Tafadhali jisahihishe. Kama mlikurupuka tu bila kutumia shule kupiga kampeni ya ELIMU BURE, basi kweli CHADEMA NI CHAMA CHA PROPAGANDA.
Mwanzoni niliamini kuwa unahoja ya msingi unataka tuijadili kama wasomi, kumbe nilikosea, kwani akili yako imeoza kuliko kawaida. Kujua au kutokujua uchumi kunauhusiano gani na rangi(race) ya mtu? Hao wana CCM kama wewe mnao ujua uchumi ni wazungu, wahindi au waarabu? Ebu tuondelee upumbavu wako hapa eboo!
 
Posho pekee zinaigharimu serikali 500bn, elimu inaweza kuwa funded. Je wapo tayari kukatwa posho at least 60%... ili tuwasomeshe wanetu?
 
Mwanzoni niliamini kuwa unahoja ya msingi unataka tuijadili kama wasomi, kumbe nilikosea, kwani akili yako imeoza kuliko kawaida. Kujua au kutokujua uchumi kunauhusiano gani na rangi(race) ya mtu? Hao wana CCM kama wewe mnao ujua uchumi ni wazungu, wahindi au waarabu? Ebu tuondelee upumbavu wako hapa eboo!

Sijakueleza kuwa CCM uchumi wanaujua, unaweza kusoma thread na hoja zangu zote. Ninachokieleza hapa ni kuwa Hoja zenu za ELIMU BURE HAMKUZIFANYIA UTAFITI- MLIKURUPUKA TU. Kwani hayo ndio wananchi walipenda kusikia, mlishindwa kuwaeleza kile wanachopashwa kusikia.
 
wana jf ogopeni sana udini utatupotezea dhamira ya ukombozi wa tz. We Zawadi ya ujinga ngoda kaanze darasa la kwanza kwani uwezo wako wa kufikilia unazidiwa kabisa na mtoto wangu ambaye haja anza masomo bado

Kama ulijua hivyo ungemketisha mtoto wako ilinihojiane naye. Inawezekana mtoto wako anaakili zaidi kuliko wewe. Mpe komputa aandike hoja.
 
Mwalimu NYerere alitoa elimu bure, matokeo yake baada ya miaka 20 nchi ilitembelea magoti. CHADEMA (Mh Slaa) japo ya kujua hilo bado ilisisitiza kutoa Elimu bure kwa watanzania wote ili ishinde uchaguzi 2010, lakini ikaanguka. Hii ni kutokana na ueleo mkubwa wa watanzania na kuelewa kuwa hizo ni PROPAGANDA ZA UONGO.

Wiki iliyopita nilipoandika Thread "CHADEMA NI CHAMA CHA PROPAGANDA" wengi walidai nilete ushahidi au vyanzo vya taarifa hizo. Sikufanya hivyo kwa kuogopa Mod kuifuta habari hiyo. Leo nimeamua kuandika ushahidi wa Propaganda hizo za uongo tukianzia kwenye kipengele cha ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE.

Ili twende hatua kwa hatua naona vyema tuanzie na mkoa wa Kilimanjaro ambako ndio Ngome ya CHADEMA ilikojikita. Naomba waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA aeleze kinaga ubaga ni vipi kwa kutumia kodi ya mkoa wa Kilimanjaro itamudu kutoa elimu bure kwa wananchi wa mkoa huo kabla hatujazungumzia Tanzania nzima.

Mkoa wa Kilimanjaro unaongoza Tanzania nzima kwa kuwa na shule za Sekondari nyingi kuliko mikoa yote ya Tanzania. Una sekondari 288 wakati hata Dar es salaam ina sekondari 252 tu (Chanzo: www.moe.go.tz/NectaResuls). Wakazi wa kilimanjaro ni 1441000 ukilinganisha na Dar es salaam ambao ni takriban 2,809,000 (Chanzo: Tanzania: Regions, Major Cities & Urban Localities - Statistics & Maps on City Population). Pato la kodi la mkoa wa Kilimanjaro (Rombo, Hai, Mwanga, Same, Mosho mjini na Moshi vijijini) ni 14,236.4 Milioni (Tzsh) wakati lile la Dar es salaam ni 441,000.5 Milioni (Tzsh) (Chanzo: Tanzania Revenue Authority - Kigoma).

Kabla sijaandika zaidi naomba huyu waziri kivuli wa fedha wa CHADEMA akisaidiana na wapambe wake hapa JF wanieleze ni vipi watazigawanya hizo 14,236.4 milioni Tzsh katika huduma za matibabu (hospitali, zahanati na elimu ya afya), Polisi, utawala mkoa na wilayani, pembejeo, na Elimu (mishahara ya walimu, ukarabati na stationaries).

Mkishindwa kufanya hivyo maana yake ELIMU BURE KWA WATANZANIA WOTE NI PROPAGANDA YA UONGO. Vinginevyo mlitaka kutumia pesa ya walipa kodi wa mikoa mingine kuendeleza mkoa wenu maana kiuchumi haiwezekani Kilimanjaro yenye wakazi 1441000 iwe na shule kupita Dar es salaam yenye wakazi 2,809,000.

Nasubiri majibu yenu kabla sijaendelea na sekta nyingine.

umejitahidi sana kutafuta takwimu, nakupongeza kwa hilo. Umesahau tu jambo moja kuwa kilimanjaro sio nchi. Ni sehemu ya nchi. Katika hizo ongeza gawio zitokanazo na raslimali za taifa (Madini, Bandari, Bahari, Maziwa, n.k) uone kama inawezekana au la.
 
Thanks you, but you are mixing things

Mimi sina shida na christians wala israel as long as they do justice to others period!

As for accepting jesus, that is debatable..

Accepting as whom? (Messiah yes I do ) accept him as God (No I do not and I will not)
Nyie mnaotaka kwenda mbinguni kwanini msianzishe thread nyingine au muende kwenye jukwaa la dini kuliko kutuharibia mjadala wetu juu ya elimu ya bure?
 
Tatizo la mikataba ya madini li wazi. Si wana CCM si vyama pinzani haviungi mkono. Tatizo lililopo ni kwamba kuvunja mikata hivyo watanzania tutalipa gharama kubwa sana kama tulivyofanywa Dowans. Na matatizo kama hayo yapo nchi zote za Afrika jaribu kufanya utafiti.

Hawa wenzetu wa nchi za ulaya ni wezi, kwa bahati mbaya wanaishi kwa mtindo huo. Hakuna kingine ni kuendeleza mapambano tu, hasa kipindi hiki wakati uchumi wao uko hatarini.
Hapana. Mikataba inaweza kuvunjwa bila gharama yeyote. Hii imefanyika nchi nyingi tu kukiwemo na Zaire ya Kabila na Zambia. Hii dhana kwamba kuvunjwa kwa mikataba kutatuweka katika hali ya Dowans inaendelezwa na mafisadi kwa sababu wao ndio wanaoendelea kufaidika na mikataba hiyo. Tukishampata Sata wetu atafanya yale yanayotokea Zambia. We need regime change and we need change of direction.
 
Back
Top Bottom