Progressive People's Party of Tanzania

Bado anapata ushauri kutoka kwa Makamba. Akikamilisha tu ajenda yake na CCM natumaini atakuwa na matamanio ya kujiunga nasi. Vipi wewe... kwanini usijiunge nasi bob?!

SteveD na Rev.
Salaam za Heri,
NAOMBA NAMBA WAKUU
 
Rev Kishoka;

Amani iwe juu yako. Mimi kadi yangu ni namba tatu, wewe, Steve na yangu. Unajua namna ya kunipata.

Chama lazima na muhimu kiwe na jina la kiswahili, kumbuka wanachama wetu wengi tunawategemea kutoka vijijini. Vijiji ndo itakuwa ngome kuu, vijiji ndo vinachagua rais na wabunge. Mijini longolongo hawapigi kura, wanashinda tu hapa JF

Kwahiyo basi nashauri kyama kyetu kiwe na jina la Chama cha Maendeleo Ya wananchi Tanzania, au Chama Cha maendeleo Tanzania, au Chama cha Kuwaendeleza wananchi Wa Tanzania -CKWT. Fikiria hilo ila ni muhimu.

Nimependa mrengo wa kati kwasababu tutaweza ku moderate wenye mrengo wa kushoto na kulia.

Main base yetu iwe vijijini na focus ielemee huko.

Tutahitaji fedha kwa ajili ya Kwenda vijijini, inabidi tukae mimi wewe na SteveD tulifanyie kazi hilo.

Watu wenye Migogoro au waliotimuliwa kwenye vyama vyenye migogoro kutokana na migogoro hatuwataki. Kama mtu au kiongozi ana tu join aje akiwa ameachana na chama chake kwa AMANI.

Inabidi tuanzishe vyombo vya habari ambavyo vitalenga zaidi vijijini, namna na ufadhili niachieni nisije kumwaga kuku kwenye mtama wengi bureeeeee!, kwanini pia naomba nisiulizwe.

Kyama kyetu kisiteuwe au kuwapigia kura wakurugenzi wake..... nina sababu na nitaziongelea kwenye kujadili RASIMU ya KATIBA ya chama.

Tunahitaji fedha..... hilo nalo pembeni.

Naomba kuwakilisha maombi na maoni yangu. Ni mategemeo yangu kuwa maombi yangu ya uwanachama yatakubaliwa.

Ndimi mwanachama mtarajiwa namba tatu

FP
 
Hili jina si geni masikioni mwangu.........! humu sio mule alipokuwepo somebody ABUBAKAR? na kile cha MWAKITWANGE kilikuwa kinaitwaje?
naomba kujuzwa...!
Kipo chama kinaitwa PPT-Maendeleo, kinaongozwa na jamaa anaitwa Peter Kuga Mzirai. Ndicho kilisimamisha mgombea mwanamke kwenye nafasi ya uarais uchaguzi mkuu uliopita na ndiye ambaye amerejea CCM hivi majuzi
 
Rev Kishoka;

Amani iwe juu yako. Mimi kadi yangu ni namba tatu, wewe, Steve na yangu. Unajua namna ya kunipata.

Chama lazima na muhimu kiwe na jina la kiswahili, kumbuka wanachama wetu wengi tunawategemea kutoka vijijini. Vijiji ndo itakuwa ngome kuu, vijiji ndo vinachagua rais na wabunge. Mijini longolongo hawapigi kura, wanashinda tu hapa JF

Kwahiyo basi nashauri kyama kyetu kiwe na jina la Chama cha Maendeleo Ya wananchi Tanzania, au Chama Cha maendeleo Tanzania, au Chama cha Kuwaendeleza wananchi Wa Tanzania -CKWT. Fikiria hilo ila ni muhimu.

Nimependa mrengo wa kati kwasababu tutaweza ku moderate wenye mrengo wa kushoto na kulia.

Main base yetu iwe vijijini na focus ielemee huko.

Tutahitaji fedha kwa ajili ya Kwenda vijijini, inabidi tukae mimi wewe na SteveD tulifanyie kazi hilo.

Watu wenye Migogoro au waliotimuliwa kwenye vyama vyenye migogoro kutokana na migogoro hatuwataki. Kama mtu au kiongozi ana tu join aje akiwa ameachana na chama chake kwa AMANI.

Inabidi tuanzishe vyombo vya habari ambavyo vitalenga zaidi vijijini, namna na ufadhili niachieni nisije kumwaga kuku kwenye mtama wengi bureeeeee!, kwanini pia naomba nisiulizwe.

Kyama kyetu kisiteuwe au kuwapigia kura wakurugenzi wake..... nina sababu na nitaziongelea kwenye kujadili RASIMU ya KATIBA ya chama.

Tunahitaji fedha..... hilo nalo pembeni.

Naomba kuwakilisha maombi na maoni yangu. Ni mategemeo yangu kuwa maombi yangu ya uwanachama yatakubaliwa.

Ndimi mwanachama mtarajiwa namba tatu

FP


Sikuwahi kufikiria kuwa mwanachama wa chama chochote lakini kwa chama hiki nitakuchukua kadi...!!! Best wishes
 
Waungwana,

Maboksi yamenishinda, narudi nyumbani na narudi kuanzisha chama. John Tendwa naomba ajiandae kwa ujio wa Mchungaji.

Chama changu kinalenga kuleta maendeleo kwa Mtanzania na si kwa kauli tuu bali kwa vitendo.

Nimejifunza mengi kutoka kwa TANU, CCM, CUF, CHADEMA, TLP na hata katika kubeba maboksi.

Lengo kuu la kwanza ni kuelimisha Mtanzania ajue haki yake ya kiraia na kikatiba.

Pili ni kumpa Mtanzania si tegemeo au tarajio tuu kuwa anaweza siku moja kupata ngekewa na kuneemeka, bali ni kumfundisha njia bora za kujineemesha kwa kumpa uimara wa moyo, roho na kisha wa kufanya kazi atambue kuwa hakuna lisilowezekana.

Tatu, katika kumjenga Mtanzania huyu upya, Chama changu kitalenga kumjenga Mtanzania anayejitegemea kwa kutumia nyenzo na mazingira aliyomo.

Nne, Chama cha PPPT kitahakikisha kuwa Watanzania wanapewa kipaumbele katika shughuli zote za uzalishaji kwa kutoa elimu ya nadharia na vitendo kuelewa mifumo ya Uchumi iliyoko Tanzania na manufaa yake kwa jamii na maisha yao.

Tano, PPPT lengo lake la muda mrefu ni kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa si nchi yenye kuishi katika ndoto za Amani, Utulivu na Mshikamano, bali ni kwa vitendo ambavyo vitadhihirika kwa kumjenga Mtanzania aondokane na Umasikini, Ujinga na Maradhi. Katika lengo hili, PPPT itahakikisha kuwa inashirikiana na Wananchi wa Tanzania kuujenga mfumo mzuri na bora ambao ni adilifu wa uzalishaji mali na uchumi na kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2035, Tanzania itakuwa inazalisha na kulisha nchi zaidi ya 10 inazopakana nazo.

Sita, Maendeleo ya jamii, yatatokana na mfumo bora wa Elimu na Afya ambao ni chimbuko na msingi mkuu wa Ajira na Uzalishaji mali. Mfumo wa elimu na Afya utapewa kipaumbele ili kujenga Taifa la Watu walioelimika kwa dhati na wenye uwezo wa kufanyia kazi elimu na ujuzi wao kwa kuajiriwa au kujitegemea na Taifa lenye watu walio na afya bora inayoandamana na lishe.

Saba, PPPT ni chama chenye mrengo wa kati, kitajenga kwa kuchagua mfumo bora wa Uchumi unaowafaa Watanzania, kukiwa na nia ya kujenga nchi ambayo Serikali yake si kubwa na yenye kunenepa kwa utapiamlo, bali ni Serikali iliyo imara na yenye afya bora (lean and healthy) ambayo itapunguzwa ukubwa wake kwa asilimia 50 katika kipindi cha miaka 10 baada ya PPPT kuingia katika mfumo wa kisiasa kuanzia ngazi za Mtaa, Kijiji, Kata, Tarafa, Wilaya na hata Taifa.

Nane, kwa kuwa Tanzania iko njia panda kuelewa mfumo bora na sahihi kwa wakati (nyakati) na mazingira yetu kiuchumi, PPPT italenga kuelimisha na kutoa msukumo wa Ujasiriamali na kujitegemea kama mfumo mpya wa kiuchumi ambao utakuwa na vibwagizo (element) kutoka kwenye mfumo wa Kibepari, Kikabaila na hata kijamaa katika kuijenga upya Tanzania.

Tisa, PPPT itahakikisha kuwa inashirikiana na kwa ridhaa ya wananchi na dhamana kutoka kwa Wananchi kuwa shughuli za uzalishaji kutoka kwa wawezekaji wa nje, zinawanufaisha Watanzania kwa zaidi ya Asilimia 3 tunazopata leo hii. Lengo litakuwa ni kuhamasisha Watanzania kushirikiana na Wageni wawekezaji na kuwa washiriki na wabia katika shughuli za Uzalishaji mali na hivyo pato la Taifa kuongezeka kupitia viwango vipya vya kodi na ushuru ambavyo asilimia 50 ya mapato hayo yataelekezwa moja kwa moja kwa wananchi na sehemu husika zilizozalisha mali hizo na kujishughulisha kiuchumi.

Kumi, PPPT kina dhamira ya kurudisha heshima ya Mtanzania na Utu wa Mtanzania awe wa upande wowote ule wa Muungano, dini, kabila, umri, jinsia, kiwango cha elimu au aina ya Ajira. Kwa Tanzania kuwa nchi yenye uimara wa kiuchumi ambao ndio msingi mkuu wa kuhakikisha kuna Amani, Mshikamano na Utulivu wa kweli, kila Mtanzania atarudishiwa haki yake ya Kikatiba na aliyopewa na muumba kwa kuthaminiwa nafasi yake katika Taifa na zaidi, dhamana yake kupitia sanduku la kura.

Kumi na Moja, PPPT itahakikisha kuwa Demokrasia inajengwa upya, kwa kuwa na mfumo shirikishi wa Kiutawala, Kikatiba na Kiserikali ambao utatoa nafasi sawa kwa kila Mtanzania bila ubaguzi au kujali maslahi ya kundi fulani. Mfumo huu utatoa nafasi sawa kwa kila mtu kushiriki katika uzalishaji mali, kushiriki katika siasa na uwakilishi bila kuegemea kutoa upendeleo kwa kikundi kimoja au kwa chama kimoja chenye nguvu.

Mwisho, nawaomba mjiunge nami katika safari hii mpya na wote mnakaribishwa kujiunga mlete mawazo mapya ya kimapinduzi ikiwa tu, mtakuwa tayari kumtumikia Mtanzania na si kutumikiwa na Watanzania!

Akhsanteni,

Good luck :lakini kwa bahati mbaya hukubahatika kujifunza kwa ASP.
 
Jina la chama: Progressive People's Party of Tanzania
Kwa kiswahili: Chama cha Maendeleo Endelevu ya Wananchi
Kwa kifupi: "Wananchi na Maendeleo"

Ushauri;
kwenye makabrasha ya chama twende na hayo majina ya kithungu, lakini mitaani twende na
" Wananchi na Maendeleo"

Ushauri tu!
 
kama jina ni refu basi kifupi chake PIPIPI TI, PIPIPITI au PIPI PITI, hakuna mtanzania atayeshindwa mbona wanatamka majina ya ajabu tu ya wajukuu wao, ( ashley, precious, joylyn,xenia ) wanaowaona mara moja kwa miaka mitatu na hawasahau sembuse chama ambacho kitawaleltea maendeleo ya kweli na watakuwa nacho 24/7???.

lol, this is some classy humor!! :)
 
Rev Kishoka;

Amani iwe juu yako. Mimi kadi yangu ni namba tatu, wewe, Steve na yangu. Unajua namna ya kunipata.

Chama lazima na muhimu kiwe na jina la kiswahili, kumbuka wanachama wetu wengi tunawategemea kutoka vijijini. Vijiji ndo itakuwa ngome kuu, vijiji ndo vinachagua rais na wabunge. Mijini longolongo hawapigi kura, wanashinda tu hapa JF

Kwahiyo basi nashauri kyama kyetu kiwe na jina la Chama cha Maendeleo Ya wananchi Tanzania, au Chama Cha maendeleo Tanzania, au Chama cha Kuwaendeleza wananchi Wa Tanzania -CKWT. Fikiria hilo ila ni muhimu.

Nimependa mrengo wa kati kwasababu tutaweza ku moderate wenye mrengo wa kushoto na kulia.

Main base yetu iwe vijijini na focus ielemee huko.

Tutahitaji fedha kwa ajili ya Kwenda vijijini, inabidi tukae mimi wewe na SteveD tulifanyie kazi hilo.

Watu wenye Migogoro au waliotimuliwa kwenye vyama vyenye migogoro kutokana na migogoro hatuwataki. Kama mtu au kiongozi ana tu join aje akiwa ameachana na chama chake kwa AMANI.

Inabidi tuanzishe vyombo vya habari ambavyo vitalenga zaidi vijijini, namna na ufadhili niachieni nisije kumwaga kuku kwenye mtama wengi bureeeeee!, kwanini pia naomba nisiulizwe.

Kyama kyetu kisiteuwe au kuwapigia kura wakurugenzi wake..... nina sababu na nitaziongelea kwenye kujadili RASIMU ya KATIBA ya chama.

Tunahitaji fedha..... hilo nalo pembeni.

Naomba kuwakilisha maombi na maoni yangu. Ni mategemeo yangu kuwa maombi yangu ya uwanachama yatakubaliwa.

Ndimi mwanachama mtarajiwa namba tatu

FP
That's good point to note. Tatizo mojawapo kubwa la upinzani Tanzania limekuwa ni influence kutoka kwa waasisi wa vyama ambao wengi wao ni x-CCM. Hii imesababisha vyama vingi kuwa na sera na katiba zinazofanana na zile za CCM kwa namna fulani hivyo kupoteza maana halisi ya chama cha upinzani. It's about time we have a really opposition party.
Kadi namba nne please!
 
Ushauri;

Core Values;
"-We believe and recognize that every party has played significant role in our national development"

However, we are not satisfied with the result and pace of development, this is the reason why we introduce another party to serve the people of Tanzania.


Hatupo kubeza yale yaliyofanywa na wengine, bali kujenga juu ya yale mazuri na kwa speed ya light.
 
Ushauri;

Core Values;
"-We believe and recognize that every party has played significant role in our national development"

However, we are not satisfied with the result and pace of development, this is the reason why we introduce another party to serve the people of Tanzania.


Hatupo kubeza yale yaliyofanywa na wengine, bali kujenga juu ya yale mazuri na kwa speed ya light.

Philosophically, hili sidhani kama ni sahihi sana. Kukubali kutosahihisha yale unayoona mabaya, na ambayo yamekufanya uchukue uamuzi wa kuanzisha chama na harakati zako mpya, si kuuma na kupuliza tu, bali ni kujaribu kuficha maovu ya wale waliopita na kuharibu au kusababisha hayo maovu.

Na pale unapokubali kujenga juu ya mazuri ya hao unaotaka kupingana nao (maana katika siasa hakuna neutrality), swali linaloibuka ni kuwa- kwanini usijiunge huko huko na kuendeleza hayo mazuri kuliko kujifanya unapaka rangi na kujenga partition ndani ya nyumba wakati ukiwa umesimama nje?!!

Mkuu Kasheshe, kuna wakati huwa ni vyema kubomoa au kuanza na msingi. Naamini umeshafikia uamuzi kama huo mara kadhaa pale computer yako inapokuwa kero, badala ya kupatch, unafuta kila kitu na kuanza na OS installation. Katika hili, chukulia kuwa hii PPPT ni OS mpya iliyokuwa designed specifically kuwa very efficient, cheap to run and install kwa mashine inayozeeka na kuwa kero kwa mtumiaji. You get the gist!
 
Mchungaji
Una mikakati gani ya kuvutia wapiga kura?

Huku uswahilini mambo si mchezo ati. Chama chaweza kufa kabla ya kuzaliwa.
 
Waungwana,

Maboksi yamenishinda, narudi nyumbani na narudi kuanzisha chama. John Tendwa naomba ajiandae kwa ujio wa Mchungaji.

Chama changu kinalenga kuleta maendeleo kwa Mtanzania na si kwa kauli tuu bali kwa vitendo.

Akhsanteni,


Kishoka,

Mie wasiwasi wangu ni hapo kwenye maneno "chama changu". Kama kweli kutakuwa na Demokrasia, hivi akaja mtu mwengine mwenye nguvu zaidi ya kushawishi wapiga kura na kutaka kukiteka CHAMA CHAKO kama ambavyo Zitto alitaka kukiteka CHAMA CHA MTEI/Mbowe (CCM?) utakuwa tayari ku-step down na kusubiri kama jamaa ataboronga, basi wanachama wakurudishe tena kwa njia ya demokrasia au uwekwe pembeni milele na ukumbukwe tu kama mtu aliyeleta demokrasia ya kweli Tanzania?

Mie wasiwasi wangu siku zote ni hapo tu. Na miiko gani ya viongozi kama chama mtajiwekea 'in advance'. Hii miko ndiyo itakuwa kama mwanga wa nini kitatokea kama mtashinda uchaguzi. Mtu kama ni FISADI basi mapema kabisa ataambiwa achagua kuwe kiongozi au arudi akaendelee na kuganga njaa/kufanya biashara zake. Wadhamini wote lazima waandikwe na wawekwe wazi na chama kisikubali kupokea hela kubwa kubwa maana nidyo kujitundika kitanzi. Heri kupokea tuseme max. 10 mlns Tsh.

Mwisho kama nilivyosema hapo zamani, chama hiki kiwe chama cha kwanza kufanya mikutano yake hadi ONLINE ili hata wale Watanzania waliokwama kufika kwenye kikao, waweze kuhudhuria hata kama kwa siku hiyo watakuwa kwenye kuvua samaki bwawa la Igombe.

Kama hayo juu, hasa lile la kwanza na MIIKO ya viongozi likiwa limeandikwa na kuwekwa wazi, basi Mchungaji, mie ni MWANACHAMA.
 
Huo ndio ushujaa anayetembea usiku ni mwamba kwani wakati huo wengi wamelala. Kuimba sio tija ones presence must be felt and in other tribes inasaidia kufukuza vinyemelezi kwenye mji wako.Kushtuka mtu akiona ujani goes to the principle that do not trust anyone. Basing on the above therefore kelele zako zina maana sana sio za bure wala sio za woga.

Ama kweli wewe unajua kweli kunisoma...umeweza ku relate na maisha halisia ya Mkerewe.

Rev. Kishoka, Steve, Kasheshe, Fairplayer na wengineo nyote..
Nawapeni pongezi sana kwa maamuzi yenu lakini tafadhali nakuombeni kufikiria kitu moja tu..
Kwa nini nyote kwa pamoja msijiunge na Chadema kwanza mkajaribu kukibadilisha kuondoa udhaifu ili kiweze kukabiri vizuri uchjaguzi wa mwaka 2010.
Ninazo sababu muhimu sana ktk mawazo haya kwani wakuu zangu Wananchi wamechoka.. Taifa letu halina muda wa kusubiri Nabii kwa miaka 10 au 20 ijayo..Na kuanzishwa kwa chama hiki kipya hadi kufikia mahala kimesimama sawasawa itachukua muda huo. By then mtaikuta nchi kama Ethiopia ya 1982..
Pili, navyofahamu mimi Chadema inahitaji vijana kama nyie makini ili kuwawezesha kuchukua ushindi wilaya na mikoa ktk uchaguzi mkuu ujao 2010. Na ikiwa mtafanikiwa ni imani yangu kubwa kwamba UMOJA wenu vijana chini ya chama kimoja ndipo pekee mnaweza kuiangusha CCM, laasivyo kugawanyika kwenu ktk makundi hakuwezi kabisa kumwondoa CCM.
Binafsi naamini kwamba kisiasa Adui wa wananchi hivi sasa ni CCM - UONGOZI..nakubaliana na maneno ya mwalimu kimsingi kwamba nchi yetu ili ipate kuendelea inahitaji vitu vinne ARDHI WATU, SIASA SAFI na UONGOZI BORA..katika hayo chama chenu kimechukua uzito zaidi ktk Watu na Mazingira ambayo ni sehemu kubwa ya hekima ya mwalimu.
Lakini maadam tunakosa Siasa safi, siasa inayokana Ubwana na utumwa ndipo nyie mnapokuja na PPPT. Zote hizi ni nyenzo muhimu sana ktk MAHITAJI yetu ya maendeleo lakini kabla hatujafika huko kuna kitu Emergency hapa - Uongozi bora ni TATIZO kubwa, tatizo ambalo linahitaji kuziba Ufa huu kwanza laa sivyo itatubidi tujenge Ukuta mzima..
Matayarisho yenu yote hanakosa kutazama kiini cha TATIZO hili la UONGOZI BORA ambalo ndio sababu kubwa ya kuzaliwa kwa UFISADI... Na UFISADI ndio kilema cha maendeleo yetu kwa ujumla.
Kwa hiyo ningeshauri kuchukua maamuzi ya dharura kwanza, kuondoa hii shida kubwa ya Uongozi bora kwa kuziba nyufa zilizopo. Mkifanikiwa kuchukua majimbo mkiwa na azma moja tu ya kuziba ufa huu mkubwa uliopo ktk uongozi bora bila shaka Ufisadi utakosa nafasi pia na itakuwa rahisi kwenu ku practice kile mnacho preach.
Wakuu zangu DAWA ya Ufisadi ni Uongozi bora, tunahitaji tiba ya haraka na kuwaweka waathirika kwenye karantini ili maradhi haya yasisambae zaidi..kisha ndio pale tutaweza kusimamisha sheria (Vaccine) kwa kutumia Siasa safi ambayo kwa hivi sasa naweza sema bado ipo Lab ikifanyiwa majaribio.
Nawaombeni sana mfikirie hili kwa makini sana mkizingatia zaidi yale yaliyopo usoni mwetu. Ufisadi umekithiri nchini na sidhani kama kuundwa kwa chama kipya ndio Solution ya dharura hii isipokuwa ni ktk malengo ya muda mrefu (long term strategy).. hivi sasa tunahitaji Umeme, Chadema sii Dowans wala Richmond..ni mtambo wa wananchi uliopo na unafanya kazi chini ya kiwango chake, kinachotakiwa ni kufanyiwa ukarabati ambao kwa imani yangu nyie wakandarasi mnaweza kabisa kuwasha hizo Mw zilizopungua na kuiwezesha nchi nzima kutoka kizani for the time being!
 
Mkuu wangu kwanza mnabidi mfikirie Watanzania walio wengi.. Huyo mama yangu mkulima nikimwambia Progressive People's Party of Tanzania, atauliza eeeh ndio nini hiyo Pogolesivu!..kaazi mpya!
Wakuu wapo wengi sana, jaribuni pia kutumia jina la kiswahili amini maneno yangu mna deal na Wadanganyika!

I like that, wakikiita hivyo itakuwa sawa kabisa!
 
Back
Top Bottom