CULCULUS
JF-Expert Member
- Nov 17, 2011
- 316
- 619
Mimi ni Mwanafunzi wa Mwaka wa Tatu hapa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kampasi ya Mlimani. Kwa muda wangu wote hapa chuoni nimekuwa nikisikitika sana jinsi mambo yanavyoendeshwa. Na kwa mgeni anaetoka nje hawezi amini kuwa haya yanatokea katika Taasisi inayojikita katika Elimu (Academic), Utafiti (Resarch) na Ushauri (Consultancy).
Imefika wakati Tawala za Vyuo vikuu (UDSM hususani) viamke ni vitambue wajibu wao. Haya ni baadhi tu ya duku duku langu hapa Chuoni:-
I) Vyoo vingi hapa Kampasi havina Taa (Bulb). Nyakati za usiku wanafunzi tunaingia vyooni kwa kutumia uzoefu kwamba choo hiki nikienda hatua tatu nitakuwa nimefika sehemu ya kukojolea. Then ukifika unakojoa. Matokeo yake vyoo vingi vimejaa maji maji (mikojo) kwenye kordo. Kwenye Jengo la UDBS ambalo halina hata miaka 3 sasa hivi Vyoo havina taa. Mikojo inachuruzika kama chemchem!
II) Njia muhimu za chuo, mfano kutoka Cafeteria kupitia darajani hadi Seminar Rooms (SR) hakuna taa za barabarani. Taa zilizopo haziwaki, imebaki milingoti kama urembo.
III) Electricity Socket za Seminar Rooms (SR) hazitoi umeme tangu nimeingia mwaka wa kwanza na sasa nakaribia kumaliza. Sasa sijui ziliwekwa za nini
IV) Kumekuwepo na ongezeko wa wimbi la wizi wa laptop hususan kwenye Parking za Magari ya pale Hill Park. Magari yanavunjwa vioo na kupekuliwa wakati Auxilliary Police ipo. Wanafunzi wengi wa Masters wamekuwa wahanga wa janga hili
V) Kordo za mabweni hazina taa na maji ya vyoo yamekuwa yakivujia kwenye makordo na pengine kuingia hadi kwenye vyumba vya wanafunzi kwa wale walio karibu na vyoo husika.
VI) Maji yakikatika inakuwa ni kama janga chuoni. Wanafunzi wanajisadia kwenye vyoo vya maji (Vyoo vya kuflash) bila kuwa na maji matokeo yake kinyesi kinajazana kwenye sinki la shoo utadhani kimeziba. Hii kitu tunaiita ‘deposit' kwa kweli ni kero kwa sababu harufu hutanda mabwenini na pia si salama kiafya
VII) Bweni la Hall 2 limechoka hata ukiliangalia kwa nje ingawa wenyewe wanasema life expectancy yake bado. Sasa sijui wanataka wanafunzi walitumie hadi end of life expectancy na hatimae wadondoke nalo. Kwanza sewerage system yake imechoka na kuna baadhi ya floor maji yanandokeo kwenye kordo hadi kwenye ngazi za kutembea waenda kwa miguu.
VIII) Kubebana bebana kwenye vitanda imekuwa tabia ya kuzoeleka. Ingawa ni fault ya wanafunzi wenyewe lakini Utawala wa Chuo nao umezembea kwa sababu hawafanyi inspection kukagua wakazi wa mabwenini. Mfano vyumba vya Hall 6, awali vilijengwa kwa ajili ya kuishi mwanafunzi mmoja moja (kwa jinsi ninavyosikia). Baadae wanafunzi walipozidi kuongezeka Chuo utawala ukaongeza kitanda kimoja kimoja kwa kila chumba na hivyo vikawa viwili viwili viwili na kwa msingi huo wanaopaswa kuishi kwenye chumba hicho ni Wanafunzi wawili tu.
Kwa sasa inashangaza sana kila kitanda wanafunzi wanabebana na bado unakuta kuna Wanafunzi wengine wanakaribishwa wanaingiza godoro wanakuwa wanalala chini. Na huyu anaelala chini nae anambeba mwenzie. Kwa hiyo chumba kilichokuwa designed kwa kuishi Mwanafunzi mmoja, wanaishi Wanafunzi sita! Uongozi unajua lakini hauwajibiki!
IX) Licha ya kuwa na Library kubwa na ya kisasa, haina vitabu vya kisasa. Vitabu vingi ni vya miaka ya tisini kurudi nyuma. Vitabu vya miaka ya elfu mbili ni vichache sasa(Sisemi kwamba vitabu vya zamani si vizuri). Kwa mantiki hii Wanafunzi wanakosa maarifa ya mapya na ya kisasa. Tatizo hilo ndilo limechangia Wanafunzi wengi kuamini katika matumizi ya Mitandao hususani Google katika kutafuta material ya kujisomea.
X) Wanazuoni wengi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (na vyuo vingine pia) wamegeuka kuwa brush ya utawala uliopo madarakani. Sasa hivi hakuna tena ile dhana kwamba Sauti ya Wanazuoni ni sehemu ya Sauti ya Wananchi. Pale Watawala wapovurunda, tawala nyingi za Vyuo vikuu licha ya kuwa na Wasomi waliobobea wamekuwa kimya bila kutoa matamko. Mengi ya Matamko yao ni ya kuisafisha na kuisifia serikali iliyopo Madarakani hata pale inapopaswa ionye. Dk Benson Bana, Rwekaza Mkandala, n.k ni mifano ya wanazuoni waliogeuza Taaluma zao kuwa Brush la Watawala.
Imefika wakati Tawala za Vyuo vikuu (UDSM hususani) viamke ni vitambue wajibu wao. Haya ni baadhi tu ya duku duku langu hapa Chuoni:-
I) Vyoo vingi hapa Kampasi havina Taa (Bulb). Nyakati za usiku wanafunzi tunaingia vyooni kwa kutumia uzoefu kwamba choo hiki nikienda hatua tatu nitakuwa nimefika sehemu ya kukojolea. Then ukifika unakojoa. Matokeo yake vyoo vingi vimejaa maji maji (mikojo) kwenye kordo. Kwenye Jengo la UDBS ambalo halina hata miaka 3 sasa hivi Vyoo havina taa. Mikojo inachuruzika kama chemchem!
II) Njia muhimu za chuo, mfano kutoka Cafeteria kupitia darajani hadi Seminar Rooms (SR) hakuna taa za barabarani. Taa zilizopo haziwaki, imebaki milingoti kama urembo.
III) Electricity Socket za Seminar Rooms (SR) hazitoi umeme tangu nimeingia mwaka wa kwanza na sasa nakaribia kumaliza. Sasa sijui ziliwekwa za nini
IV) Kumekuwepo na ongezeko wa wimbi la wizi wa laptop hususan kwenye Parking za Magari ya pale Hill Park. Magari yanavunjwa vioo na kupekuliwa wakati Auxilliary Police ipo. Wanafunzi wengi wa Masters wamekuwa wahanga wa janga hili
V) Kordo za mabweni hazina taa na maji ya vyoo yamekuwa yakivujia kwenye makordo na pengine kuingia hadi kwenye vyumba vya wanafunzi kwa wale walio karibu na vyoo husika.
VI) Maji yakikatika inakuwa ni kama janga chuoni. Wanafunzi wanajisadia kwenye vyoo vya maji (Vyoo vya kuflash) bila kuwa na maji matokeo yake kinyesi kinajazana kwenye sinki la shoo utadhani kimeziba. Hii kitu tunaiita ‘deposit' kwa kweli ni kero kwa sababu harufu hutanda mabwenini na pia si salama kiafya
VII) Bweni la Hall 2 limechoka hata ukiliangalia kwa nje ingawa wenyewe wanasema life expectancy yake bado. Sasa sijui wanataka wanafunzi walitumie hadi end of life expectancy na hatimae wadondoke nalo. Kwanza sewerage system yake imechoka na kuna baadhi ya floor maji yanandokeo kwenye kordo hadi kwenye ngazi za kutembea waenda kwa miguu.
VIII) Kubebana bebana kwenye vitanda imekuwa tabia ya kuzoeleka. Ingawa ni fault ya wanafunzi wenyewe lakini Utawala wa Chuo nao umezembea kwa sababu hawafanyi inspection kukagua wakazi wa mabwenini. Mfano vyumba vya Hall 6, awali vilijengwa kwa ajili ya kuishi mwanafunzi mmoja moja (kwa jinsi ninavyosikia). Baadae wanafunzi walipozidi kuongezeka Chuo utawala ukaongeza kitanda kimoja kimoja kwa kila chumba na hivyo vikawa viwili viwili viwili na kwa msingi huo wanaopaswa kuishi kwenye chumba hicho ni Wanafunzi wawili tu.
Kwa sasa inashangaza sana kila kitanda wanafunzi wanabebana na bado unakuta kuna Wanafunzi wengine wanakaribishwa wanaingiza godoro wanakuwa wanalala chini. Na huyu anaelala chini nae anambeba mwenzie. Kwa hiyo chumba kilichokuwa designed kwa kuishi Mwanafunzi mmoja, wanaishi Wanafunzi sita! Uongozi unajua lakini hauwajibiki!
IX) Licha ya kuwa na Library kubwa na ya kisasa, haina vitabu vya kisasa. Vitabu vingi ni vya miaka ya tisini kurudi nyuma. Vitabu vya miaka ya elfu mbili ni vichache sasa(Sisemi kwamba vitabu vya zamani si vizuri). Kwa mantiki hii Wanafunzi wanakosa maarifa ya mapya na ya kisasa. Tatizo hilo ndilo limechangia Wanafunzi wengi kuamini katika matumizi ya Mitandao hususani Google katika kutafuta material ya kujisomea.
X) Wanazuoni wengi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (na vyuo vingine pia) wamegeuka kuwa brush ya utawala uliopo madarakani. Sasa hivi hakuna tena ile dhana kwamba Sauti ya Wanazuoni ni sehemu ya Sauti ya Wananchi. Pale Watawala wapovurunda, tawala nyingi za Vyuo vikuu licha ya kuwa na Wasomi waliobobea wamekuwa kimya bila kutoa matamko. Mengi ya Matamko yao ni ya kuisafisha na kuisifia serikali iliyopo Madarakani hata pale inapopaswa ionye. Dk Benson Bana, Rwekaza Mkandala, n.k ni mifano ya wanazuoni waliogeuza Taaluma zao kuwa Brush la Watawala.