PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,724
Jana nilimpeleka mgonjwa wangu Hospitali ya Mount Meru akiwa na shida inayohusiana na allergy.
Lakini nilikatishwa tamaa na mganga niliyemkuta kwenye chumba kimojawapo nilichoelekezwa!
Kwa ufupi mganga huyo ni kisichana kidogo kabisa(around 25) ambacho hakijui wala kujali maana ya mtu kuumwa au kuugua, mapozi meengi na maneno ya mkatomkato!
Nilipodadisi niliambiwa kuwa "HAWA NI KIZAZI KIPYA, wameajiriwa juzijuzi mwanzoni mwa mwaka, na wako wengi sana"
Tulisubiri takriban dakika tano akiwa anaongea na simu na mtu, ambapo ilionekana wazi ni mwandani wake, au mtu fulani wa nasaba yake aliyemuudhi sana katika jambo fulani huko mtaani kwake!
Kwa kuisoma tu hali aliyokuwa nayo huyo 'mganga' nilipata shaka kama angeweza kutoa tiba sahihi!
Sasa wanajamvi ninachotaka tujadili ni ishu ya mahusiano ya UMRI wa mganga na KAZI anayoifanya!
Je, kwa vile kidada kama kile kimemaliza shahada yake pale MUCHS, na kikafaulu vizuri kwenye makaratasi yake, basi kianze kazi, huku kikiwa na ma'frustration ya wachumba, na kinabipiwa kila dakika kikiwa kazini, au je labda umri wa daktari kuanza kazi uwe stipulated kwenye maadili ya uganga?
Lakini nilikatishwa tamaa na mganga niliyemkuta kwenye chumba kimojawapo nilichoelekezwa!
Kwa ufupi mganga huyo ni kisichana kidogo kabisa(around 25) ambacho hakijui wala kujali maana ya mtu kuumwa au kuugua, mapozi meengi na maneno ya mkatomkato!
Nilipodadisi niliambiwa kuwa "HAWA NI KIZAZI KIPYA, wameajiriwa juzijuzi mwanzoni mwa mwaka, na wako wengi sana"
Tulisubiri takriban dakika tano akiwa anaongea na simu na mtu, ambapo ilionekana wazi ni mwandani wake, au mtu fulani wa nasaba yake aliyemuudhi sana katika jambo fulani huko mtaani kwake!
Kwa kuisoma tu hali aliyokuwa nayo huyo 'mganga' nilipata shaka kama angeweza kutoa tiba sahihi!
Sasa wanajamvi ninachotaka tujadili ni ishu ya mahusiano ya UMRI wa mganga na KAZI anayoifanya!
Je, kwa vile kidada kama kile kimemaliza shahada yake pale MUCHS, na kikafaulu vizuri kwenye makaratasi yake, basi kianze kazi, huku kikiwa na ma'frustration ya wachumba, na kinabipiwa kila dakika kikiwa kazini, au je labda umri wa daktari kuanza kazi uwe stipulated kwenye maadili ya uganga?