Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,555
- 19,428
Taasisi nyingi za serikali ambazo asili ya majukumu yake ni kutumia mabavu zina tatizo la kuwa na professionals wachache sana. Taasisi kama vile TAKUKURU, POLISI, na MAGEREZA ni taasisi ambazo zinatakiwa kuwa na watendaji ambao ni professionals wa hali ya juu ili kuhakikisha kuwa haki inatendeka kila mara kwa kutomwonea mtu au kuzembea mbele ya mhalifu. Mbali ya mafunzo ya kutumia nguvu kama matumizi ya pingu, matumizi ya silaha, na namna ya kujilinda (self defense), watu hawa wanatakiwa wae na elimu ya juu ya kitaalamu katika nyanya nyingine kama ifuatavyo:
TAKUKURU na POLISI wanatakiwa wawe wamesomea nyanja kama Criminal Justice, Criminal psychology, Interrogation techniques, Human Rights Law, Crisis Management, The Law of Evidence, na Constitutional Rights Law. MAGEREZA wanatakiwe wawe pia wamesomea nyanja kama Criminal Psychology, Human Rights Law, Crisis Management, na Educational Psychology.
Mara nyingi sana tumesikia uchunguzi wa kipolisi au TAKUKURU umekamilika na kupelekwa na DPP, lakini ama uchunguzi huo hutupiliwa mbali, na au kesi inapofanyika serikali inashindwa ama kwa technicalities au kwa kukosa ushahidi imara. Hivi karibuni tumesikia wagombea wakihojiwa na TAKUKURU na baadaye kuachiwa lakini sina uhakika kama kweli hao TAKUKURU walikuwa wanawahoji wagombea hao kitaalamu kiasi cha kujiridhisha kuwa ama kuna kosa au hakuna lolote.
Ushauri wangu kwa serikali ijayo, ni kuimarisha muundo wa tasisisi hizi mbili ambazo zina jukumu kubwa sana la kulinda sheria ile ziwe na watu wenye ujuzi na kazi zao. Ninajua kuwa idara ya polisi ina wanasheria ila ni watu wakubwa sana ambao hupelekewa ripoti kutoka kwa watu ambao hawako trained katika sheria, na hivyo kufanya shughuli yote ya upelelezi iwe imejengwa kwenye msingi dhaifu.
Madai ya mama Sita hivi Karibuni kuwa TAKUKURU inawabambikiza kesi watu, yanatia doa sana kwenye kredibility ya TAKUKURU hasa itakagundulika kuwa interrogation ile haikufanyika professionally.
TAKUKURU na POLISI wanatakiwa wawe wamesomea nyanja kama Criminal Justice, Criminal psychology, Interrogation techniques, Human Rights Law, Crisis Management, The Law of Evidence, na Constitutional Rights Law. MAGEREZA wanatakiwe wawe pia wamesomea nyanja kama Criminal Psychology, Human Rights Law, Crisis Management, na Educational Psychology.
Mara nyingi sana tumesikia uchunguzi wa kipolisi au TAKUKURU umekamilika na kupelekwa na DPP, lakini ama uchunguzi huo hutupiliwa mbali, na au kesi inapofanyika serikali inashindwa ama kwa technicalities au kwa kukosa ushahidi imara. Hivi karibuni tumesikia wagombea wakihojiwa na TAKUKURU na baadaye kuachiwa lakini sina uhakika kama kweli hao TAKUKURU walikuwa wanawahoji wagombea hao kitaalamu kiasi cha kujiridhisha kuwa ama kuna kosa au hakuna lolote.
Ushauri wangu kwa serikali ijayo, ni kuimarisha muundo wa tasisisi hizi mbili ambazo zina jukumu kubwa sana la kulinda sheria ile ziwe na watu wenye ujuzi na kazi zao. Ninajua kuwa idara ya polisi ina wanasheria ila ni watu wakubwa sana ambao hupelekewa ripoti kutoka kwa watu ambao hawako trained katika sheria, na hivyo kufanya shughuli yote ya upelelezi iwe imejengwa kwenye msingi dhaifu.
Madai ya mama Sita hivi Karibuni kuwa TAKUKURU inawabambikiza kesi watu, yanatia doa sana kwenye kredibility ya TAKUKURU hasa itakagundulika kuwa interrogation ile haikufanyika professionally.