MAKOLE
JF-Expert Member
- Feb 5, 2012
- 618
- 280
Nimesikia asubuhi ya leo katika kipindi cha mapitio ya magazeti ahadi ya Waziri wa Nishati na Madini Mh Prof. Sospeter kuwa mgao wa Umeme haupo na Hautakuwepo katika Tanzania hii.
Kwanza atambue kuwa ahadi hiyo tayari watangulizi wake walishaitoa na waliishia kuaibika.
La pili ni kwamba takribani kwa kipindi cha wiki moja sasa nipo katika wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga, kwa kipindi hicho chote nilichokaa hapa nimeshuhudia Tatizo klubwa sana la kukatika kwa umeme, Karibu kila siku iendayo zake umeme unakatika. Kwa siku ya jana pekee, tar 20/10 umeme ulikatika mara 5. Leo tarehe 21/10, mara tu baada ya kipindi hicho cha mapitio ya magazeti umeme mahali hapa tayari umekatika. Naandika post hii saa 1 na nusu asubuhi hakuna umeme. Kwa hili profesa wangu umetokota vibaya.
Kwanza atambue kuwa ahadi hiyo tayari watangulizi wake walishaitoa na waliishia kuaibika.
La pili ni kwamba takribani kwa kipindi cha wiki moja sasa nipo katika wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga, kwa kipindi hicho chote nilichokaa hapa nimeshuhudia Tatizo klubwa sana la kukatika kwa umeme, Karibu kila siku iendayo zake umeme unakatika. Kwa siku ya jana pekee, tar 20/10 umeme ulikatika mara 5. Leo tarehe 21/10, mara tu baada ya kipindi hicho cha mapitio ya magazeti umeme mahali hapa tayari umekatika. Naandika post hii saa 1 na nusu asubuhi hakuna umeme. Kwa hili profesa wangu umetokota vibaya.