Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Profesa Kikula: Niko tayari kujiuzulu
Tuesday, 11 January 2011 20:42
Habel Chidawali, Dodoma
MAKAMU Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Profesa Idrisa Kikula, amesema kitendo cha wahadhiri wa chuo hicho na wanafunzi kuanzisha mgomo, huenda kuna ajenda ya siri nyuma yao.
Kufuati hatua hiyo, Profesa Kikula alisema msalaba alionao ni mkubwa, hivyo yupo tayari kumwachia mtu yeyote kama atapatikana ili naye aweze kujitwisha kama wahadhiri hao wataona inafaa kufanya hivyo.
Profesa Kikula alitoa kauli hiyo jana ikiwa ni siku moja baada ya wanafunzi wa chuo hicho Kitivo cha Elimu, kuanzisha maandamano hadi Ofisi ya Waziri Mkuu Mjini hapa.
Hata hivyo, kauli ya Profesa Kikula ingekuwa ni lulu kwa wanachuo na wahadhiri wao kama ingetolewa na Profesa Shaaban Mlacha, ambaye ni Mkuu Kitengo cha Fedha na Utawala, kwani wahadhiri na wanachuo wengi wamekuwa wakimlalamiki kuwa chanzo cha migogoro yote.
Akitoa ufafanuzi mbele ya waandishi wa habari jana, Profesa Kikula alisema mgomo baridi ulioanzishwa na wanachuo hao na wahadhiri, sio tatizo kubwa ambalo linaweza kumfanya amuite Rais Jakaya Kikwete kama wengi wanavyodai.
"Tatizo sio kubwa kama linavyochukuliwa na wengi, bali ni mambo ambayo tunaweza kuyamaliza ndani ya chuo sisi wenyewe, bila ya kumuita hata rais kama ambavyo watu wanataka," alisema.
Alisema wao kama uongozi wa chuo, watakaa na taasisi zinazohusika na masuala ya urekebishaji mishahara kwa upande wa wafanyakazi chuoni hapo, kama rais atahitaji taarifa uongozi utafanya hivyo, lakini syo lazima kwenda chuoni hapo.
Kuhusu suala la migogoro ya uongozi, Profesa Kikula alisema iwapo kutajitokeza watu na kudai hawana imani na yeye, basi hatasita kuitisha baraza la chuo waeleze wanayemtaka kuwaongoza.
Tuesday, 11 January 2011 20:42
Habel Chidawali, Dodoma
MAKAMU Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Profesa Idrisa Kikula, amesema kitendo cha wahadhiri wa chuo hicho na wanafunzi kuanzisha mgomo, huenda kuna ajenda ya siri nyuma yao.
Kufuati hatua hiyo, Profesa Kikula alisema msalaba alionao ni mkubwa, hivyo yupo tayari kumwachia mtu yeyote kama atapatikana ili naye aweze kujitwisha kama wahadhiri hao wataona inafaa kufanya hivyo.
Profesa Kikula alitoa kauli hiyo jana ikiwa ni siku moja baada ya wanafunzi wa chuo hicho Kitivo cha Elimu, kuanzisha maandamano hadi Ofisi ya Waziri Mkuu Mjini hapa.
Hata hivyo, kauli ya Profesa Kikula ingekuwa ni lulu kwa wanachuo na wahadhiri wao kama ingetolewa na Profesa Shaaban Mlacha, ambaye ni Mkuu Kitengo cha Fedha na Utawala, kwani wahadhiri na wanachuo wengi wamekuwa wakimlalamiki kuwa chanzo cha migogoro yote.
Akitoa ufafanuzi mbele ya waandishi wa habari jana, Profesa Kikula alisema mgomo baridi ulioanzishwa na wanachuo hao na wahadhiri, sio tatizo kubwa ambalo linaweza kumfanya amuite Rais Jakaya Kikwete kama wengi wanavyodai.
"Tatizo sio kubwa kama linavyochukuliwa na wengi, bali ni mambo ambayo tunaweza kuyamaliza ndani ya chuo sisi wenyewe, bila ya kumuita hata rais kama ambavyo watu wanataka," alisema.
Alisema wao kama uongozi wa chuo, watakaa na taasisi zinazohusika na masuala ya urekebishaji mishahara kwa upande wa wafanyakazi chuoni hapo, kama rais atahitaji taarifa uongozi utafanya hivyo, lakini syo lazima kwenda chuoni hapo.
Kuhusu suala la migogoro ya uongozi, Profesa Kikula alisema iwapo kutajitokeza watu na kudai hawana imani na yeye, basi hatasita kuitisha baraza la chuo waeleze wanayemtaka kuwaongoza.