Profesa Jay akamatwa na polisi

Lucchese DeCavalcante

JF-Expert Member
Jan 10, 2009
5,471
733
jj.jpg
Msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo fleva), Joseph Haule maarufu kama Profesa Jay amekamatwa na jeshi la polisi saa 5:30 usiku juzi Jumapili, na kufikishwa katika kituo cha Polisi cha Kijitonyama Mabatini, wilaya ya Kinondoni, kwa tuhuma za kutaka kumnyang’anya silaha Mkuu wa Kituo Kidogo cha Polisi cha Alimaua Kisiwani, jijini Dar es Salaam.

Chanzo chetu cha habari kilieleza kwamba msanii huyo anayeheshimika na wapenzi wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini, alikamatwa na askari akiwa na mdogo wake aitwaye Wilfred Haule na rafiki yao aitwaye Robert Mugisha wakati wakiwa njiani kuelekea Kijitonyama, nyumbani kwa msanii mwingine wa Bongo fleva aitwaye Hamis Mwinjuma au maarufu kama Mwana FA.

Imedaiwa kuwa Profesa J na wenzake wakiwa ndani ya gari lenye namba za usajili CA 196-748, aina ya BMW, waliligonga gari jingine ambalo namba zake hazikuweza kupatikana mara moja wakati wakiwa njiani kuelekea Kijitonyama na baada ya kusababisha ajali hiyo, polisi waliwaona na kutaka kuwaweka chini ya ulinzi, lakini Profesa J na wenzake walikataa kutii amri na kuanza kucharuka, hali iliyowalazimu polisi kutumia nguvu.

Habari zinadai katika purukushani hiyo ya aina yake, Profesa J na wenzake walionekana kutaka kuwazidi nguvu polisi na kutaka kumnyang’anya mkuu wa kituo silaha, hali iliyowalazimu polisi kufyatua risasi hewani. Licha ya kuwatisha kwa kufyatua risasi, lakini bado walikataa kusalimu amri na kukataa kuwekwa chini ya ulinzi, ndipo polisi walipopiga simu kwa wenzao kuomba msaada.

Muda mfupi baadaye gari la polisi ‘Defender’ liliwasili eneo la tukio likiwa na askari wengine, na kufanikiwa kuwakamata Profesa J na wenzake kisha kuwapeleka hadi Kituo cha Polisi cha Kijitonyama, ambapo walifunguliwa jalada la lenye namba KJN/2257/2010, kwa kosa la kujaribu kunyang’anya silaha.Hadi tunakwenda mitamboni msanii huyo alikuwa korokoroni.

Source: Globalpublisherstz.com
 


Jamani jamani hii avatar inanifanya nishindwe kusoma hii habari, nikifungua hapa ofsn inabidi nijifiche kidogo, INANIKWAZA JAMANI
 


Jamani jamani hii avatar inanifanya nishindwe kusoma hii habari, nikifungua hapa ofsn inabidi nijifiche kidogo, INANIKWAZA JAMANI

Mods please you need to try and control these Avatars maana sasa mdogo mdogo tutaanza kuweka viungo nyeti vya uzazi. Sio wote tuna ofisi zetu peke yetu. Zifute hizi za utata mods maana nashindwa hata kuangalia JF at home ni nooooooooooooooooooooooooooooma
 
Naona masuperstar wetu wameanza kuhisi wako America... And that they could be above the LAW...
 
Niliona jina la Prof. J angeperform jana kwenye Kongamano/Tamasha la Mwalimu pale UD, ila jana sikuuliza kama aliperform au la. Kwa source ni Global, as usual huwa wana sensenalize ili wauze magazeti, kwa Prof. ninayemjua mimi, hawezi kutaka kunyang'anya silaha polis,

Ila polisi nao wana yao, niliwahi kukamatwa usiku wa kawaida tuu toka kwenye starehe zangu, nikaulizwa kitambulisho, nikasema sina, nikaulizwa ninafanya wapi kazi, nikasema sifanyi kazi popote, wakaniambia niko chini ya ulinzi, nikawauliza kwa kosa gani?, wakasema kwa nini huna kitambulisho, kwa nini huna kazi, nikawauliza hivi kukosa kitambulisho ni kosa?, au kokosa kazi ni kosa?, jamaa wakakasirika, wakasemezana, hiri rijamaa rinatuuriza maswali sisi polisi, risweke ndani lirajiereza mbele ya safari. Nikaamriwa kukaa chini, mikono kichwani, ilinibidi nitii tuu.

Jamaa wakaita defender, kwa redio, wakati wakiripoti, wakasema kuna rijambazi wamerikamata rikiwa kwenye harakati za kwenda kutenda uhalirifu. Nilipelekwa kituoni O/Bay kama majira ya Saa Nne usiku. Thanks God, ile kufikishwa kituoni, Mkuu wa Kituo Afande Kalinga, akauliza huyu jamaa amefanya nini, jamaa wakadai, huyu jamaa tumemhoji akatutukana. Afande Kalinga akaniuliza mbele yao, wewe umewatukana vijana wangu?, mimi nikamjibu Sitamtukana mtu Afande, nikamwambia labda wasema nimewatukana nini, kabla hawajajibu, afande akawaambia wanipeleke chumba cha pili kuchukua maelezo yangu, huku nyuma wakasemezana, Afande Kalinga akaja akamwambia askari anayechukua maelezo, aache, akaniambia ondoka yamekwisha. Mimi nikamwambia afande kumbe huu ndio utendaji wa vijana wake, hivi ni wanachi wangapi wa kawaida wanatendewa isivyo na polisi?.

Hii ndio nchi yetu na hawa ndio polisi wetu.
 
Kuhusu ugomvi may be yes may be no. But kujaribu kunyang'anya silaha nahisi ni a big NO manake hawa kina Marwa wanatabia ya kubambikia kesi wakiona kesi msingi haina ushahidi au hauna uzito!
 
Niliona jina la Prof. J angeperform jana kwenye Kongamano/Tamasha la Mwalimu pale UD, ila jana sikuuliza kama aliperform au la. Kwa source ni Global, as usual huwa wana sensenalize ili wauze magazeti, kwa Prof. ninayemjua mimi, hawezi kutaka kunyang'anya silaha polis,

Ila polisi nao wana yao, niliwahi kukamatwa usiku wa kawaida tuu toka kwenye starehe zangu, nikaulizwa kitambulisho, nikasema sina, nikaulizwa ninafanya wapi kazi, nikasema sifanyi kazi popote, wakaniambia niko chini ya ulinzi, nikawauliza kwa kosa gani?, wakasema kwa nini huna kitambulisho, kwa nini huna kazi, nikawauliza hivi kukosa kitambulisho ni kosa?, au kokosa kazi ni kosa?, jamaa wakakasirika, wakasemezana, hiri rijamaa rinatuuriza maswali sisi polisi, risweke ndani lirajiereza mbele ya safari. Nikaamriwa kukaa chini, mikono kichwani, ilinibidi nitii tuu.

Jamaa wakaita defender, kwa redio, wakati wakiripoti, wakasema kuna rijambazi wamerikamata rikiwa kwenye harakati za kwenda kutenda uhalirifu. Nilipelekwa kituoni O/Bay kama majira ya Saa Nne usiku. Thanks God, ile kufikishwa kituoni, Mkuu wa Kituo Afande Kalinga, akauliza huyu jamaa amefanya nini, jamaa wakadai, huyu jamaa tumemhoji akatutukana. Afande Kalinga akaniuliza mbele yao, wewe umewatukana vijana wangu?, mimi nikamjibu Sitamtukana mtu Afande, nikamwambia labda wasema nimewatukana nini, kabla hawajajibu, afande akawaambia wanipeleke chumba cha pili kuchukua maelezo yangu, huku nyuma wakasemezana, Afande Kalinga akaja akamwambia askari anayechukua maelezo, aache, akaniambia ondoka yamekwisha. Mimi nikamwambia afande kumbe huu ndio utendaji wa vijana wake, hivi ni wanachi wangapi wa kawaida wanatendewa isivyo na polisi?.

Hii ndio nchi yetu na hawa ndio polisi wetu.

Pasco kwanza nimechekeshwa na majibu yako na maswali ya hao 'mapoyoyo'

halafu nikakarahishwa na waliyokufanyia na nahisi baada ya kugundua walikuwa 'wanadili' na nani ndo wakakuacha maana they sensed trouble in paradise!!!

Poor wananchi wasio kuwa na A wala B....wanaishia kufungwa kwa kesi za kupakaziwa!!
 
pole prof Jay..

mie sipendagi mapolisi wa TZ jamanii,natamanigi kukiwa na purukushani kati yao na raia,wao washindwe!!jambo ambalo ni ndoto!LOLZ!
 
Ukisababisha ajali barabarani unawekwa chini ya Ulinzi? Hii nimeisoma leo hapa!

BTW: Gari lililogongwa ni la mkuu wa kituo? Ni mara chache ku-reinforce usalama eneo la ajali ya magari madogo mawili! Defender!
 
polisi bongo njaa kali sana sio siri,niliwahi kukamatwa na polisi kutaka nimpe hongo mpaka alinisindikiza nikakope hela nimuhonge ili aniachie.
 
Police wetu nao wanaboa sana ..wanaweza kukusababishia ufanye jambo ambalo sio .. wanaweza kuwa hata wamemsingizia kijana wa watu
 
Mie niliwahi kupewa lift na kaka mmoja nikiwa mmoja wa abiria ..kijana wa watu akawa bado hajabandika ile Docs ya week ya nenda kwa usalama kasimamishwa ..kijana kajaribu kumwambia police kapitiwa tu ataibandika jamaa haelewi mbaya police mwenyewe ananuka pombe tupu ..kwa nini asimkamatwe na kupelekwa kituoni kufika huko police huyo anawaambia wenzie eti jamaa alitishia kumpiga ..
police wakamwanzishia songombigo la ajabu .Salama yake kumbe aliwahi kumpa OCD offer ya bia wakiwa bar hahaha kilichoendelea mnakijua raia wema wa TZ
 
Back
Top Bottom