Profesa J : Kila la Kheri Yanga..!

KIM KARDASH

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
5,139
1,139
MSANII wa muziki wa bongo fleva nchini Joseph Haule 'Prof J', amewataka Watanzania kuweka utaifa mbele kwa kuishangilia Yanga katika mchezo wake na Zamelek utakaopigwa Februari leo jioni.
J alisema siku hiyo Watanzania wanapaswa kujitokeza kwa wingi huku wakiungana kwa pamoja kutoa sapoti kwa wachezaji wa Yanga kwa kuwa wanaiwakilisha Taifa.
"Mimi ni mmoja wa mashabiki wa Simba lakini siku hiyo nitatoa sapoti kwa timu ya nyumbani Yanga kwani utaifa ni muhimu kuliko kitu kingine"alisema Prof J
Prof. J alisema kwa kufanya hivyo itakuwa ni hatua moja mbele katika kufanya mapinduzi ya maendeleo ya mchezo huo unaopendwa na wengi hapa nchini.
Alisema ushabiki wa kuzizomea timu za hapa nyumbani zinapocheza na wageni hausaidii kuinua kiwango cha soka na kuliletea Taifa mafanikio bali unazindi kurudisha nyuma mafanikio yanayotarajiwa.
Prof J alisema Watanzania ni muhimu wakaweka utaifa mbele kwa kuzishangilia timu zao kwa kuwa kila timu inaposhinda ni taifa ndilo linalopata heshima na kutambulika katika mchezo huo duniani.
 
MSANII wa muziki wa bongo fleva nchini Joseph Haule 'Prof J', amewataka Watanzania kuweka utaifa mbele kwa kuishangilia Yanga katika mchezo wake na Zamelek utakaopigwa Februari leo jioni.
J alisema siku hiyo Watanzania wanapaswa kujitokeza kwa wingi huku wakiungana kwa pamoja kutoa sapoti kwa wachezaji wa Yanga kwa kuwa wanaiwakilisha Taifa.
“Mimi ni mmoja wa mashabiki wa Simba lakini siku hiyo nitatoa sapoti kwa timu ya nyumbani Yanga kwani utaifa ni muhimu kuliko kitu kingine”alisema Prof J
Prof. J alisema kwa kufanya hivyo itakuwa ni hatua moja mbele katika kufanya mapinduzi ya maendeleo ya mchezo huo unaopendwa na wengi hapa nchini.
Alisema ushabiki wa kuzizomea timu za hapa nyumbani zinapocheza na wageni hausaidii kuinua kiwango cha soka na kuliletea Taifa mafanikio bali unazindi kurudisha nyuma mafanikio yanayotarajiwa.
Prof J alisema Watanzania ni muhimu wakaweka utaifa mbele kwa kuzishangilia timu zao kwa kuwa kila timu inaposhinda ni taifa ndilo linalopata heshima na kutambulika katika mchezo huo duniani.

hapa hakuna haja ya utaifa sababu hivi ni vilabu na sio timu za taifa zinacheza..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom