Profesa Haroub Othman afariki dunia

Mhache

JF-Expert Member
Jun 20, 2008
345
24

Mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Haroub Othman amefariki dunia leo alfajiri. Hizi ni taarifa nilizozipata kwenye TBC One. Kifo hiki ni pigo kubwa kwa wanasiasa na wanafunzi wa chuo hicho. Kifo hiki kimenigusa kwani alikuwa mmoja wa walimu wangu wakati nikisoma chuoni hapo. Ninachoweza kusema ni kwamba tulimpenda sana Profesa Haroub Othman lakini Mungu alimpenda zaidi. Mungu ailaze roho ya Profesa Haroub Othman mahali pema peponi.
 
Mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Haroub Othman amefariki dunia leo alfajiri. Hizi ni taarifa nilizozipata kwenye TBC One. Kifo hiki ni pigo kubwa kwa wanasiasa na wanafunzi wa chuo hicho. Kifo hiki kimenigusa kwani alikuwa mmoja wa walimu wangu wakati nikisoma chuoni hapo. Ninachoweza kusema ni kwamba tulimpenda sana Profesa Haroub Othman lakini Mungu alimpenda zaidi. Mungu ailaze roho ya Profesa Haroub Othman mahali pema peponi.

Burian Professor Haroub Othman. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu Mahali Pema Peponi.
Utakumbukwa kwa mengi ndani na nje ya Tanzania na Zanzibar.
Ulikuwa msomi mahiri kutoka Tanzania Visiwani, ukiwa na mbongo zinazochemka.
Uliasisi harakati mbali mbali za kimapinduzi, bila woga wala hiana.
Ulikuwa mwana-mapinduzi mfuasi wa falsafa za Karl Marx usiyebadili msimamo, ukiwaunga mkono kamaradi Fedel Castrol, Che Gwivara na wanamapinduzi wengine.
Uliasisi Zanzibar Legal Services Centre; Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Zanzibar.
Ulifundisha watanzania wengi waliopitia Chuo Kiuu Cha Dar es salaam; utaendela kukumbukwa na wengi.
Ulikuwa nguzo, maktaba na hazina ya hekima ya Taasisi ya Taaluma ya Maendeleo (IDS) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Kwa heri Prof.
Kwa heri Haroub Othman
Kwa heri kipenzi cha wanamapinduzi wengi.
 
hiki kifo kimeniuma sana,Prof. Haroub alikuwa mtu muhimu sana katika nchi yetu,pengo ambalo halitazimika milele,rambirambi zangu za dhati ziende kwa ndugu na familia yake.
Bwana alitoa na ametwaa,hakuna tuwezalo kufanaya,amemaliza safari yake na sote tutafuata njia hiyo hiyo.
 
R.I.P Prof, kila nafsi itaonja umauti. Kama mmoja wa wanafunzi wa Prof. Haroub DS second year mlimani tutakuenzi kwa kuendeleza falsafa zako uhsusani ile ya kutokutaka kufungamana na upande wowote na kudadavua siasa za Zanzibar, Africa na Dunia.

Binafsi naona mwezi huu June 09 ni mbaya sana kwa UDSM alumni mwanzoni mwa mwezi huu pia tulimpoteza Prof. Baradiyana. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
 
Back
Top Bottom