nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
na Asha Bani
MHADHIRI mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustine, Profesa Mwesiga Baregu, na wanaharakati wengine wamemjia juu Rais Jakaya Kikwete wakimtaka kujiuzulu kutokana na kushindwa kusimamia utendaji wa serikali yake.
Kauli ya wanaharakati hao imekuja siku moja baada ya Kikwete kuwashukia Mawaziri, Makatibu wakuu wa wizara na watendaji wa serikali kutotumia nafasi zao vibaya kwa kujishirikisha katika vitendo vya rushwa na ubabe wakati wa semina elekezi ya siku nne inayofanyika mkoani Dodoma.
Akizungumza kwa njia ya simu na Tanzania Daima Jumatano jana, Profesa Baregu alisemakauli ya rais Kikwete, inashangaza kwa sababu watendaji anaowashutumu aliwachagua mwenyewe hivyo badala ya kuwataka kuachia ngazi aanze kujiondoa yeye ili ufanyike uchaguzi mkuu mwingine.
Profesa Baregu ambaye ni Mjumbe Kamati Kuu Taifa ya Chama cha Demekorasia na Maendeleo (CHADEMA) alisema maneno hayo ni dalili ya kushindwa kuongoza nchi kutokana na kuwa na watendaji wabovu hivyo kujitokeza kwake kwenye vyombo vya habari na kuwashukia ni kutaka aonewe huruma na wananchi.
"Kutokana na hili sitomuunga mkono hata kidogo na namshauri kuvunja baraza la mawaziri kama halifanyi vyema au mwenyewe kujiuzulu kwa kuwa ana kila dalili ya kushindwa kuwaongoza watendaji wake," alisema Profesa Baregu.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Julius Mtatiro, alisema ikiwa Kikwete anaona watendaji wake hawafanyi kazi awaengue na kuwachagua wengine atakaoona ni wachapakazi. Alisema maneno ya rais Kikwete yanaonyesha kutaka kujikosha kwa wananchi kwa kuwa tayari ana ombwe la uongozi kwa kuwa wananchi wana matatizo mengi ikiwemo ukosefu wa huduma ya afya, maji na mengine. Naye mwananchi Sylivester Nyamuhanga alisema kuwa kwa sasa Rais hakutakiwa kufanya semina hiyo elekezi kwa kuwa alishakagua wizara na kilichobakia ni mawaziri kufanya utekelezaji.
MHADHIRI mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustine, Profesa Mwesiga Baregu, na wanaharakati wengine wamemjia juu Rais Jakaya Kikwete wakimtaka kujiuzulu kutokana na kushindwa kusimamia utendaji wa serikali yake.
Kauli ya wanaharakati hao imekuja siku moja baada ya Kikwete kuwashukia Mawaziri, Makatibu wakuu wa wizara na watendaji wa serikali kutotumia nafasi zao vibaya kwa kujishirikisha katika vitendo vya rushwa na ubabe wakati wa semina elekezi ya siku nne inayofanyika mkoani Dodoma.
Akizungumza kwa njia ya simu na Tanzania Daima Jumatano jana, Profesa Baregu alisemakauli ya rais Kikwete, inashangaza kwa sababu watendaji anaowashutumu aliwachagua mwenyewe hivyo badala ya kuwataka kuachia ngazi aanze kujiondoa yeye ili ufanyike uchaguzi mkuu mwingine.
Profesa Baregu ambaye ni Mjumbe Kamati Kuu Taifa ya Chama cha Demekorasia na Maendeleo (CHADEMA) alisema maneno hayo ni dalili ya kushindwa kuongoza nchi kutokana na kuwa na watendaji wabovu hivyo kujitokeza kwake kwenye vyombo vya habari na kuwashukia ni kutaka aonewe huruma na wananchi.
"Kutokana na hili sitomuunga mkono hata kidogo na namshauri kuvunja baraza la mawaziri kama halifanyi vyema au mwenyewe kujiuzulu kwa kuwa ana kila dalili ya kushindwa kuwaongoza watendaji wake," alisema Profesa Baregu.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Julius Mtatiro, alisema ikiwa Kikwete anaona watendaji wake hawafanyi kazi awaengue na kuwachagua wengine atakaoona ni wachapakazi. Alisema maneno ya rais Kikwete yanaonyesha kutaka kujikosha kwa wananchi kwa kuwa tayari ana ombwe la uongozi kwa kuwa wananchi wana matatizo mengi ikiwemo ukosefu wa huduma ya afya, maji na mengine. Naye mwananchi Sylivester Nyamuhanga alisema kuwa kwa sasa Rais hakutakiwa kufanya semina hiyo elekezi kwa kuwa alishakagua wizara na kilichobakia ni mawaziri kufanya utekelezaji.