Profesa achambua kwa kina jinsi Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulivyodhoofishwa mwaka hadi Mwaka

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,285
24,158


Video kwa hisani ya Sirallymasoud wa Youtube

SOMO ZURI KWA WADAU WA JAMIIFORUM KISIMA CHA ELIMU ENDELEVU

Historia ya dhana ya Muungano uliofikiriwa na Zanzibar kabla ya Zanzibar kupata uhuru mwaka 1963 na pia baada ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar 1964 hadi sasa mwaka 2012.

Pia Profesa anatoa uchambuzi wa kina kabisa jinsi masuala ya Muungano wa Tanzania jinsi ulivyokuwa ukibadilishwa toka mwaka 1968, mwaka 1976 AFRO SHIRAZI KUMEZWA NAKUWA CCM 1977, mfano kumuondoa Raisi wa Serikali ya Mapinduzi toka ktk cheo cha Makamu wa Raisi wa serikali ya Muungano wa Tanzania na kumfanya Rais wa Zanzibar kuwa Waziri Maalumu ktk Bazara la mawairi wa serikali ya Muungano na CCM kushika hatamu kama nchi ya chama kimoja.

Sikiliza jinsi maamuzi mengi yaliyofanywa mwaka hadi mwaka toka mwaka 1964 kuudhoofisha Muungano wa Kishirikisho na kufanya Muungano usio na uwiano kati ya nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar.
 
Last edited by a moderator:


Video kwa hisani ya Sirallymasoud wa Youtube

SOMO ZURI KWA WADAU WA JAMIIFORUM KISIMA CHA ELIMU ENDELEVU

Historia ya dhana ya Muungano uliofikiriwa na Zanzibar kabla ya Zanzibar kupata uhuru mwaka 1963 na pia baada ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar 1964 hadi sasa mwaka 2012.

Pia Profesa anatoa uchambuzi wa kina kabisa jinsi masuala ya Muungano wa Tanzania jinsi ulivyokuwa ukibadilishwa toka mwaka 1968, mwaka 1976 AFRO SHIRAZI KUMEZWA NAKUWA CCM 1977, mfano kumuondoa Raisi wa Serikali ya Mapinduzi toka ktk cheo cha Makamu wa Raisi wa serikali ya Muungano wa Tanzania na kumfanya Rais wa Zanzibar kuwa Waziri Maalumu ktk Bazara la mawairi wa serikali ya Muungano na CCM kushika hatamu kama nchi ya chama kimoja.

Sikiliza jinsi maamuzi mengi yaliyofanywa mwaka hadi mwaka toka mwaka 1964 kuudhoofisha Muungano wa Kishirikisho na kufanya Muungano usio na uwiano kati ya nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar.


Kuondolewa kwa na nafasi ya Rais wa Zanzibar kwenye umakamu wa kwanza wa Rais kulitokana na ukweli kuwa ilikubalika kuwa Rais wa Tanzania anaweza kutoka popote katika eneo la jamhuri ya Muungano, tofauti kabisa na makubaliano ya Karume na Nyerere kuwa Nyerere angekuwa Rais wa Muungano na Karume angekuwa Makamu wake. Ile kufungulia mlango kuwa hata Mwinyi anaweza kuwa Rais wa Tanzania ndiyo maana umuhimu wa Makamu wa Rais kutoka Zanzibar ukatolewa kwa sababu za wazi kabisa. Unfortunately baada ya Mwinyi, hakujatokea mtu mwingine kutoka Zanzibar kuwa Rais; wakati Ahmed Salim alipokuwa akiwania nafasi hiyo, ni wazenj hao hao walioshiriki katika kumchafua na hivyo kuongeza mbara mwingine kwenye nafasi hiyo. Sasa baada ya siasa vya vyama vingi ndiyo mambo yamekuwa magumu zaidi kwani inawezekana kabisa Rais wa Zanzibar akatoka Cuf, na Rais wa Muungano akatoka TLP. Ndiyo maana kulikuwa na haja ya kufanya mabadiliko ya kuondoa umuhimu huo.

Ninajua hapa swala madaraka wakati wa utawala wa Karume (jr) katika awamu ya Kikwete lilichangia sana kuwasha moto huu kwa vile Karume hakutaka awe chini ya Kikwete; inawezekana alikuwa na sababu kwa vile sote tunaujua utawala wa Kikwete.
 
Last edited by a moderator:
Baada ya Zanzibari na Tanzania Bara tujiandae kwa Pemba kujiatangazia uhuru wake
 
Back
Top Bottom