Prof Tibaijuka lazima ajiuzulu

My Take:

Kwa kosa alilolifanya kupeleka ombi Un Pasi na kupata baraka za baraza la wawakilishi Znz wakti anajua fika suala la ardhi sio suala la muungano ni utovu mkubwa sana wa nidhamu na kutaka kufanya ubabe na kuvunja katiba ya Muungano na ile ya Zanzibar. Kiungwana anatakiwa ajiuzuru.[/FONT][/COLOR]

Prof. Tibajuka wala hahusiki na jambo hilo kiasi cha kulazimishwa kujiuzulu. Wazanzibari wamwulize Amani Karume na Dk. Shein kuhusu jambo hilo kwani kwa nafasi zao za uongozi kule Zanzibar walihusishwa kikamilifu kwenye mchakato wote.

Kiutaratibu jambo hilo lilifikishwa kwenye Baraza la Mawaziri kwa nyakati tofauti (Karume na Shein (pamoja na Nahodha na Bilal) wakiwa sehemu ya Baraza hilo) na kujadiliwa kwa kina kabla ya kuridhiwa na kupelekwa UN. Kama kulikuwa na ulazima wa suala hilo kujadiliwa na BLW (kwa maoni yangu hakukuwepo ulazima wowote), Rais wa Zanzibar wa kipindi husika alipaswa kuelekeza hivyo.

Tuache kukariri!.
 
Je unaijua bahari kuu weye?
Utawezaje kuizungumzia bahari kuu kwa Tanganyika bila kuihusisha Zanzibar?
Je ongezeka hilo Znz itafaidikaje nalo? kama watafanikiwa ombi lao huko UN, Znz itaongezewa au kupunguziwa eneo lake la bahari kwa kiasi gani?
Kwanini Braza la wawakilishi alikuhusishwa katika mchakato mzima?
kuna siri gani hapo wakti kitu hichi hakimo katika mkataba wa muungano wa Tanganyika na Znz?:eyebrows:nafikiri

hayo ni masuala yanayotakiwa kuulizwa katika kadhia nzima na kufanya Tibaijuka na Shamuhuna lazima wajiuzuru.


alaa- na shamhuna nae! basi badilisha heading yako ili twende sawa.
 
Hilo aliwezekani hata kidogo. Kwani Tanganyika na Znz zimeungana KIMKATABA na sio KIKATIBA. Kuna mambo apo nje ya mkataba wa Muungano likiwemo hili la ardhi na makazi.

Sasa unapozungumzia maslahi ya eneo la milki ya arrdhi ni lazima uziusishe pande zote mbili kwani hili si suala la muungano. Alichofanya Tibaijuka ni ubabe kitu ambacho hakikubaliki. Ni mawili tu yanatakiwa hapo ima a withdraw hayo maombi na kuanza mchakato mpya kama nchi zote mbili zitakubaliana au kuanisha kila nchi itanufaika vipi in terms of eneo hilo.

kama OIC ilizimwa na Muungano kwanini na hili lisizimwe.

Tibaijuka amechamke lazima ajiuzuru tu hakuna mjadala.


Hizi chuki za kijinga zinaonyesha kuwa kuna Wazanzibari hawapendi kuendelea na muungano. Hapo serikali ya JMT imekosea nini? Hakuna kilichoharibika hata kama eneo likiongezwa na muungano ukavunjika sheria za kimataifa zitafanya kazi ya kugawanya eneo. Tanzania kama nchi inayopakana na bahari ina haki ya kuongezewa eneo na hakuna sheria yoyote ile inayoizuia kufanya hivyo.

Azimio la Baraza la Wawakilishi si sheria ya nchi yetu wala halikuzungumzia suala la kuongezewa eneo katika bahari kuu. Hoja za Juisi Jusa zinatokana na chuki yake juu ya muungano na lengo la kujipatia umaarufu wa mtaani.

Hatuwezi kuongozwa na watu wenye chuki na hila, na kama Mtanzania nasema wakati wa kuvumilia upuuzi kama huu umekwisha tutapambana na watu wapuuzi na wapotoshaji kama Jusa bila kurudi nyuma.

Tanzania bara haiwezi kuyumbishwa na sisimizi kama Jusa na kelele zake haziwezi kuzuia sisi kupata haki yetu katika bahari kuu.
 
Jussa ndio awe wa kwanza kujiuzulu kutokana na undumilakuwili wake. Ni mnafiki hatari sana yule. Jussa alisema kuwa cuf ilianzishwa mwaka 1992 (yeye hata haijulikani alikuwa wapi) kwa lengo la kuikomboa zanzibar.

Leo tumesikia kupitia Zitto kwa Jussa alishiriki kukihujumu chama cha cuf katika uchaguzi wa 2010 kwa kutowasilisha baadhi ya nyaraka kwa muda.

Kadhalika kushiriki kumhonga Maalim kukubali kushindwa uchaguzi uliopita (rejea hotuba fupi ya maalim baada ya kutangazwa mshindi wa urais). Muda mwingi na siku za karibuni huyu mjinga Jussa amekuwa aakiikoromea sana bara kwa maslahi anayoyajua yeye.

Jussa ni mnafiki
 
  • Thanks
Reactions: ral
Wewe na Jussa wote ni waarabu, waacheni waafrika wenye eneo waongee. Kumbuka Zanzibar haiko Arabuni Barubaru, mate yatawatoka mpaka niku ya kiama Zanzibar will never fall in the hands of Oman again.
 
Yaghee mbona nyie wachoyo vya bara mwataka kula ila vyakwenu wilaya ya pemba na unguja mkoani zanzibar mwataka mle wenyewe! c vizuri hivyo tutavila tu c mwajua siye wa wabara hatujui kuremba. Mtubanie kuoa Dada zenu hadi kwenye bahari hamtaki?
 
Katika msafara wa kwenda UN walikuwepo waziri Shamhuna na katibu mkuu wa wizara yake, kwahiyo ni dhahiri kwamba SUK Zanzibar ilishirikishwa. Sasa hizi propaganda za ccmB kuwaambia wapemba wawe tayari kufa wakati walikufa 2001 na wengine wamekuwa wakimbizi hadi leo bila msaada wowote, pamoja na cuf kuingia serikalini bado imeshindwa kuwasaidia waathirika wa mauaji ya jan.2001, sasa tena anataka kuwadanganya nini wapemba??

UN ikikubali na kuiongezea JMT eneo hilo kama lilivyoombwa, then SUK Znz kama watakuwa hawajaridhika na kipande walichogawiwa wanaweza kuendelea kuzungumza na wenzao wa JMT, lakini kushauri kwamba zoezi lisistishwe, ama kusema ccmB watakwenda UN kuitaka isituongezee hilo eneo lililoombwa huo utakuwa ni ufinyu wa mawazo.

Mwisho, Barubaru wewe ni msaliti wa wazenjiberi wenzako, leo unajifanya kuwa na huruma nao, kama bado unaipenda zenji si urudishe uraia wa omani na kuomba kurudi nyumbani? kwanini kila siku kuongelea mambo ya Tanganyika wakati ulishaamua kujilipua na sasa wewe ni mwarabu wa omani?
Wakati unaposhauri Prof. Tibaijuka kwa kupigania maslahi ya JMT ungeutumia vizuri muda huo kumshauri mwanaccB mwenzako, waziri wa miundombinu wa zenji ajiuzulu kwa uzembe wa kuisimamia wizara yake hadi kuruhusu meli chakavu kubeba wapemba wenzako na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 1300. Kama huna uchungu na wale wapemba wenzako zaidi ya 1300 basi wewe ni zaidi ya mnafiki.
 
Umeshatuambia kuwa muungano huu hauna katiba sasa unasimamiaje katiba ambayo haipo? Kajipange tena, muongo wewe!

Naomba niweke wazi mipaka na nchi yetu kama ilivyoainishwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano, 1977.

1. Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.

1) Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni
pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo.

Na kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibari ya Mwaka 1984 kama ilivyorekebishwa mwaka 2009:

1. "Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la Visiwa
vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka na bahari
yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar"

DgJePCKeSQAAAABJRU5ErkJggg==

Kwa tafsiri ya kisheria ni kuwa eneo la Zanzibar ni kama lile lililokuwepo kabla ya kuungana (1964), yaani maili 12 za majini kutoka ufukweni mwake. Na kwamba haina haki ya bahari kuu na eneo la EEZ maili 200 kutoka ufukweni, kwani mataifa yanayopakana na bahari yameipata mwaka 1982 wakati Makubaliano ya Sheria za Bahari yalipofikiwa.

Ni vizuri watu kama wakina Jussa wafikirie vizuri kabla ya kuzungumza masuala kama hayo. Ni lazima ikumbukwe kuwa kwa mujibu wa sheria za kimataifa Zanzibar si nchi kwani nchi hiyo hii ndani ya JMT ambaye ni mwananchama wa Umoja wa Mataifa na mwenye haki ya kuomba haki na upendeleo wa Makubaliano ya Sheria za Bahari ya Mwaka 1982.
 
Tanzania ni nchi moja na ni jamhuri ya muungano (sheria ya 1984 Na. 15 )...Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar,na ni pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo (sheria ya 1992 Na. 4 Ib. 3)...Tibaijuka ni waziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,what wrong with claim alopeleka UN?
 
Muungano ni issue sensitive

je kulikuwa kuna ubaya gani ikafanyika public consultation juu ya hili ?

Je wananchi wamehusishwa vipi ?

serikali zote za CCM zinaweza zikawa ziko right lakini wanavyoifanya hii issue ni kui mishandle kama walivyofanya juu ya Kigamboni na uvumi juu ya kambi ya jeshi ya USA
Hivi kuongezewa eneo kwa ajiri ya uchumi wa nchi na kuimarisha ulinzi halikuwa swala kufanya mjadala wa kitaifa kwanza ndio tuchukue uamuzi, Mama Prof. Timaijuka kafanya kwa usahihi kabisa kufanya alivyo fanya. Au ulitaka pesa za walipa kodi zipotee tena kwa ajili ya kuratibu maoni ya raia juu ya kuomba kuongezewa eneo nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
 
Na vile vile Tibaijuka alitakiwa aende na faili la Tanganyika sio Tanzania. Kwani Tanzania ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Je unalijua hilo?

Kwani madaraka ya Tibaijuka mwisho msasani wala hayafiki Znz. Kwa kuwa amejivika kilemba cha Tanzania ndipo tunapomuhoji alipewa na nani madaraka ya kuiwakilisha kwenye jambo lisilo la muungano? Je aliowawakilisha wanalijua hilo?

Kwa vyovyote lazima kiungwana ajiuzuru.


Tibaijuka alipeleka azimio lilopitishwa na baraza la mawaziri la JMT, ambalo Dr shein ni mjumbe. Aliambatana na wabunge wa Jmt ambalo wazanzibari ni wajumbe. Ushiriki gani unautaka? Tukichukua mjumbe wa BLW, Tanganyika itawakilishwa na nani?
 
Hakika Jusa wewe ni shujaa sana kwa kuliona hili kwani kuna dhulma kubwa sana ilitaka kufanyika hapa. Ikiwemo ile ya kumega eneo la bahari kwa Znz na kuitumbukiza katika Muungano.

Lazima kieleweke na Prof lazima aondolewe hapo. Kwani ubabe hauna nafasi kwenye sheria. lazima sheria zifuatwe.

Sina uhakika w hayo maandishi kwenye red,maana kama Jussa ndio shujaa wa wazanzibar,basi hali ya znz ni tete kuliko ninavyo fikiria
 
Ajiuzulu kwa vipi?Eneo lililo ombwa ni miongoni mwa free zone areas;sasa ninyi kwa ujinga wenu mlidhani bahari ya hindi yote ni ya znz?
 
My Take:

Kwa kosa alilolifanya kupeleka ombi Un Pasi na kupata baraka za baraza la wawakilishi Znz wakti anajua fika suala la ardhi sio suala la muungano ni utovu mkubwa sana wa nidhamu na kutaka kufanya ubabe na kuvunja katiba ya Muungano na ile ya Zanzibar. Kiungwana anatakiwa ajiuzuru.
[/QUOTE]

Labda mie sielewi, lakini kama hilo eneo linaloombwa ni international waters iweje Jussa na wenzake wagombe? Yaani ni nongwa kwa mfano eneo hilo likawa ni lile linalotazamana na Mtwara?
 
Wanaojua kuwa Tanzania Zanzibar ni nchi kamili ni akina Jussa na wenzake wachache. Katika sheria za kimataifa hakuna nchi inayoitwa Zanzibar katika dunia hii. Na vile vile hakuna nchi inayoitwa Tanganyika katika hii dunia. Nchi inayotambuliwa duniani ni TANZANIA (Jumhuri ya Muungano wa Tanzania-JMT) na rais wake ni Jakaya Mrisho Kikwete. Kwa hiyo basi hakuna kosa lolote lililofanywa na Pro Ana Tibaijuka kupeleka maombi ya Tanzania umoja wa mataifa.

Pia napenda kumkumbusha Jussa pamoja na wenzake kuwa Tanzania Zanzibar kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano inawakilishwa katika maamuzi ya ngazi za juu kabisa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Rais wa Tanzania Zanzibar ni mjumbe wa baraza la mawaziri na pia kuna watu wengine wamepewa nafasi za uwaziri kwa sababu tu wametoka Tanzania Zanzibar. Mambo yote ya kupeleka maombi ya kuongeza eneo la bahari kuu nina uhakika kuwa yalizungumzwa ndani ya vikao vya baraza la mawaziri la JMT. Hivyo uamuzi ulifanyika kwenye vikao vya viongozi wa JMT kuwa jambo hilo ni jema na lipelekwe umoja wa mataifa kwa faida ya nchi ya Tanzania.

Hivyo basi hili jambo la kusema Prof Ana Tibaijuka ametumia ubabe naona sio sahihi hata kidogo, yeye anafanya kazi kama anavyoelekezwa na rais wa Tanzania na baraza lake la mawaziri ambamo watu kutoka Tanzania Zanzibar nao pia ni wajumbe.


Hii issue ya katiba nao iko sawa tu. KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 1977 kifungu namba 1 kinasema hivi

``Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano``

Kifungu cha 2 (1) kinasema hivi

``Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo``

Mimi naona ili ombi halijakiuka hivi vifungu kwa katiba ya JMT.

Najua kuna hoja ya Jussa kuwa hili jambo lisubiri katiba mpya. Sijui ana maana gani anaposema hivyo? Labda anahitajika kutoa ufafanuzi zaidi wa hoja yake.

Hii hoja inatuma ujumbe kuwa kuanzia sasa mambo yote ya JMT yasimame mpaka katiba mpya itakapopatikana? Mimi nadhani hili haliwezekani kufanyika. Zoezi la kuandika katiba mpya litaendelea na shughuli nyingine za serikali zitaendelea kama kawaida. Nchi haiwezi kusimama kusubiri katiba mpya kwani Tanzania tangu kuzaliwa kwake mwaka 1964 imendeshwa kwa katiba yake (pamoja na mabadiliko yake) mpaka leo hii bila kusimamisha shughuli za serikali. Sasa atasemaje leo shughuli za JMT zingoje katiba mpya? Asema anategemea nini kwenye hiyo katiba mpya?
 
Back
Top Bottom