Kachanchabuseta
JF-Expert Member
- Mar 8, 2010
- 7,269
- 675
Awali iliripotiwa kuwa Rais Jakaya Kikwete alitarajiwa kushiriki kwenye mazishi ya Mwaikusa, ambaye amefanya kazi ya uhadhiri mwandamizi wa Kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa muda mrefu.
Kutoonekana kwa viongozi wa serikali kwenye mazishi yake kumeshtua wengi, hasa baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani waliofika nyumbani kwa Profesa Mwaikusa kuhudhuria mazishi yake
Akizungumza na Tanzania Daima Jumapili, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, alisema ameshangazwa kwa hatua ya serikali kushindwa kuhudhuria mazishi ya Profesa Mwaikusa, kwani ameuawa akiwa bado mtumishi wa serikali.
Kwanza ukiangalia tukio zima, si rahisi kukwepa kuhudhuria mazishi ya Profesa Mwaikusa, pia alikuwa mfanyakazi wa serikali hadi mauti yalipomfika, iweje sasa hawa wenzetu wa serikali washindwe kuhudhuria shughuli hii muhimu? alihoji Profesa Lipumba.
Alisema umakini wa Profesa Mwaikusa katika utendaji kazi enzi za uhai wake, kumesaidia nchi kupiga hatua kwenye mambo mbalimbali, hivyo serikali kushidwa kuhudhuria mazishi yake ni jambo la kushangaza.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, alisema hakutarajia kutowaona viongozi wa serikali katika mazishi ya msomi huyo, kwani kwa namna moja au nyingine wanahusika na mauaji yake.
Hawawezi kuja hapa, yeye ndiye alishiriki katika kesi ya mgombea binafsi, na hawa ndio waliohusika na mauaji yake, alisema Mchungaji Mtikila bila kufafanua.
Mhadhiri Mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Issa Shivji, alisema haijawahi kutokea kwa serikali kushindwa kuleta hata mwakilishi wake kwa msiba wa aina hiyo, hasa ukizingatia kuwa Profesa Mwaikusa alikuwa mfanyakazi wa serikali.
Source: Tanzania Daima
Kutoonekana kwa viongozi wa serikali kwenye mazishi yake kumeshtua wengi, hasa baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani waliofika nyumbani kwa Profesa Mwaikusa kuhudhuria mazishi yake
Akizungumza na Tanzania Daima Jumapili, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, alisema ameshangazwa kwa hatua ya serikali kushindwa kuhudhuria mazishi ya Profesa Mwaikusa, kwani ameuawa akiwa bado mtumishi wa serikali.
Kwanza ukiangalia tukio zima, si rahisi kukwepa kuhudhuria mazishi ya Profesa Mwaikusa, pia alikuwa mfanyakazi wa serikali hadi mauti yalipomfika, iweje sasa hawa wenzetu wa serikali washindwe kuhudhuria shughuli hii muhimu? alihoji Profesa Lipumba.
Alisema umakini wa Profesa Mwaikusa katika utendaji kazi enzi za uhai wake, kumesaidia nchi kupiga hatua kwenye mambo mbalimbali, hivyo serikali kushidwa kuhudhuria mazishi yake ni jambo la kushangaza.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, alisema hakutarajia kutowaona viongozi wa serikali katika mazishi ya msomi huyo, kwani kwa namna moja au nyingine wanahusika na mauaji yake.
Hawawezi kuja hapa, yeye ndiye alishiriki katika kesi ya mgombea binafsi, na hawa ndio waliohusika na mauaji yake, alisema Mchungaji Mtikila bila kufafanua.
Mhadhiri Mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Issa Shivji, alisema haijawahi kutokea kwa serikali kushindwa kuleta hata mwakilishi wake kwa msiba wa aina hiyo, hasa ukizingatia kuwa Profesa Mwaikusa alikuwa mfanyakazi wa serikali.
Source: Tanzania Daima