Mhadhiri mwandamizi wa UDSM (msitaafu) na mwenyekiti wa Kigoda cha Mwl Nyerere amewaambia wanafunzi wa Udom kuwa Katiba ya Tanzania ya 1977 inampa Rais mwanya wa kuwa dictator.
Amesema hayo jana katika mhadhara (public lecture) ulioandaliwa na serikali ya wanafunzi UDOSO chuo cha elimu kuhusu "Tafakuri Juu ya Mchakato wa Kutunga Katiba"
Amesema katiba hii inampa rais mamlaka ya kuwa mkuu wa nchi, mkuu wa serikali, sehemu ya bunge na Amiri jeshi mkuu wa nchi. Jambo ambalo hata mwalimu alishawahi kukiri kuwa inampa mwanya wa kuwa dictator ingawa yeye hakutaka kuwa dictator.
Kwa mujibu wa Prof. Suala la katiba mpya sio suala la muda au umri wa katiba iliyopo, kubwa na la msingi ni mchakato uliotumika kuipata katiba hiyo.
Tanzania tangu ipate uhuru imeshaandika katiba mpya tano kwa michakato tofauti.
Ya kwanza ni katiba ya uhuru (independence constitution) ya 1961, ilipitishwa na Bunge la waingereza.
Ya pili ni katiba ya jamhuri (Republican constitution) ya 1962 iliyopitishwa na bunge maalumu la katiba (constitution assembly)
Ya tatu ni ile ya muungano 1964 iliyotungwa na rais wa URT kwa mamlaka aliyopewa na article of union.
Nne ni (entering constitution) ya 1965 ilipitishwa na bunge la kawaida. Iliundwa kwa mfumo wa chama kimoja ingawa vilikuwepo viwili TANU-Tanganyika na ASP-Zenji.
Ya tano 1977 ya mfumo wa chama kimoja CCM ilipitishwa na bunge la katiba ingawa wajumbe wake ni walewale waliokuwa ktk kamati ya rais, na ktk tume.
Naomba kutoa hoja.
Amesema hayo jana katika mhadhara (public lecture) ulioandaliwa na serikali ya wanafunzi UDOSO chuo cha elimu kuhusu "Tafakuri Juu ya Mchakato wa Kutunga Katiba"
Amesema katiba hii inampa rais mamlaka ya kuwa mkuu wa nchi, mkuu wa serikali, sehemu ya bunge na Amiri jeshi mkuu wa nchi. Jambo ambalo hata mwalimu alishawahi kukiri kuwa inampa mwanya wa kuwa dictator ingawa yeye hakutaka kuwa dictator.
Kwa mujibu wa Prof. Suala la katiba mpya sio suala la muda au umri wa katiba iliyopo, kubwa na la msingi ni mchakato uliotumika kuipata katiba hiyo.
Tanzania tangu ipate uhuru imeshaandika katiba mpya tano kwa michakato tofauti.
Ya kwanza ni katiba ya uhuru (independence constitution) ya 1961, ilipitishwa na Bunge la waingereza.
Ya pili ni katiba ya jamhuri (Republican constitution) ya 1962 iliyopitishwa na bunge maalumu la katiba (constitution assembly)
Ya tatu ni ile ya muungano 1964 iliyotungwa na rais wa URT kwa mamlaka aliyopewa na article of union.
Nne ni (entering constitution) ya 1965 ilipitishwa na bunge la kawaida. Iliundwa kwa mfumo wa chama kimoja ingawa vilikuwepo viwili TANU-Tanganyika na ASP-Zenji.
Ya tano 1977 ya mfumo wa chama kimoja CCM ilipitishwa na bunge la katiba ingawa wajumbe wake ni walewale waliokuwa ktk kamati ya rais, na ktk tume.
Naomba kutoa hoja.