Prof. Shivji: "Katiba ya Tanzania inampa Rais nafasi ya kuwa Dictetor!"

nsami

Senior Member
Jun 11, 2010
175
8
Mhadhiri mwandamizi wa UDSM (msitaafu) na mwenyekiti wa Kigoda cha Mwl Nyerere amewaambia wanafunzi wa Udom kuwa Katiba ya Tanzania ya 1977 inampa Rais mwanya wa kuwa dictator.

Amesema hayo jana katika mhadhara (public lecture) ulioandaliwa na serikali ya wanafunzi UDOSO chuo cha elimu kuhusu "Tafakuri Juu ya Mchakato wa Kutunga Katiba"

Amesema katiba hii inampa rais mamlaka ya kuwa mkuu wa nchi, mkuu wa serikali, sehemu ya bunge na Amiri jeshi mkuu wa nchi. Jambo ambalo hata mwalimu alishawahi kukiri kuwa inampa mwanya wa kuwa dictator ingawa yeye hakutaka kuwa dictator.

Kwa mujibu wa Prof. Suala la katiba mpya sio suala la muda au umri wa katiba iliyopo, kubwa na la msingi ni mchakato uliotumika kuipata katiba hiyo.

Tanzania tangu ipate uhuru imeshaandika katiba mpya tano kwa michakato tofauti.

Ya kwanza ni katiba ya uhuru (independence constitution) ya 1961, ilipitishwa na Bunge la waingereza.

Ya pili ni katiba ya jamhuri (Republican constitution) ya 1962 iliyopitishwa na bunge maalumu la katiba (constitution assembly)

Ya tatu ni ile ya muungano 1964 iliyotungwa na rais wa URT kwa mamlaka aliyopewa na article of union.

Nne ni (entering constitution) ya 1965 ilipitishwa na bunge la kawaida. Iliundwa kwa mfumo wa chama kimoja ingawa vilikuwepo viwili TANU-Tanganyika na ASP-Zenji.

Ya tano 1977 ya mfumo wa chama kimoja CCM ilipitishwa na bunge la katiba ingawa wajumbe wake ni walewale waliokuwa ktk kamati ya rais, na ktk tume.

Naomba kutoa hoja.
 
Mhadhiri mwandamizi wa UDSM (msitaafu) na mwenyekiti wa Kigoda cha Mwl Nyerere amewaambia wanafunzi wa Udom kuwa Katiba ya Tanzania ya 1977 inampa Rais mwanya wa kuwa dictator.

Amesema hayo jana katika mhadhara (public lecture) ulioandaliwa na serikali ya wanafunzi UDOSO chuo cha elimu kuhusu "Tafakuri Juu ya Mchakato wa Kutunga Katiba"

Amesema katiba hii inampa rais mamlaka ya kuwa mkuu wa nchi, mkuu wa serikali, sehemu ya bunge na Amiri jeshi mkuu wa nchi. Jambo ambalo hata mwalimu alishawahi kukiri kuwa inampa mwanya wa kuwa dictator ingawa yeye hakutaka kuwa dictator.

Kwa mujibu wa Prof. Suala la katiba mpya sio suala la muda au umri wa katiba iliyopo, kubwa na la msingi ni mchakato uliotumika kuipata katiba hiyo.

Tanzania tangu ipate uhuru imeshaandika katiba mpya tano kwa michakato tofauti.

Ya kwanza ni katiba ya uhuru (independence constitution) ya 1961, ilipitishwa na Bunge la waingereza.

Ya pili ni katiba ya jamhuri (Republican constitution) ya 1962 iliyopitishwa na bunge maalumu la katiba (constitution assembly)

Ya tatu ni ile ya muungano 1964 iliyotungwa na rais wa URT kwa mamlaka aliyopewa na article of union.

Nne ni (entering constitution) ya 1965 ilipitishwa na bunge la kawaida. Iliundwa kwa mfumo wa chama kimoja ingawa vilikuwepo viwili TANU-Tanganyika na ASP-Zenji.

Ya tano 1977 ilipitishwa na bunge la katiba ingawa wajembe wake ni walewale waliokuwa ktk kamati ya rais, na ktk tume.

Naomba kutoa hoja.

Namkubali shvji az a critical thinker,siku zote huwa mkwel na haogopi,ni miongoni mwa wasomi wachache waliobakia,mwingne aliyebakia ni DR AZAVELI LWAITAMA,PROFESA BAREGU,PROFESA OMARI,namkumbuka sana mwanaharakat PROF HAROUB OTHMAN,huyu nae alikua mwanaharakat wa kweli,RIP,but nina imani mwanaye anayesoma huko cuba atafuata nyayo,nae ni radical,wasomi wengne wamuige shvji,kuiga jambo jema si vibaya
 
Na Proffessor Chachage Chachage jamani,Rest in peace.Shivji is an asset to this nation,he is never biased na always considers what benefits the majority.Live long Prof.We need a new constitution.
Namkubali shvji az a critical thinker,siku zote huwa mkwel na haogopi,ni miongoni mwa wasomi wachache waliobakia,mwingne aliyebakia ni DR AZAVELI LWAITAMA,PROFESA BAREGU,PROFESA OMARI,namkumbuka sana mwanaharakat PROF HAROUB OTHMAN,huyu nae alikua mwanaharakat wa kweli,RIP,but nina imani mwanaye anayesoma huko cuba atafuata nyayo,nae ni radical,wasomi wengne wamuige shvji,kuiga jambo jema si vibaya
 
Na Proffessor Chachage Chachage jamani,Rest in peace.Shivji is an asset to this nation,he is never biased na always considers what benefits the majority.Live long Prof.We need a new constitution.

yeah,chachage aliandika kitabu chake cha MAKUWADI WA SOKO HURIA,ukibahatika kisome ndugu-ni riwaya nzuri,dah cku zote watu wazuri ndio hufa mapema,maneno hayo aliwah kuyazungumza shvj pale NKRUMAH HALL UDSM
 
Inafahamika. Na mkwere ndo anatumia ubovu wa katiba yetu kutu dictate waTZ! Jambo la msingi katika kuja na katiba mpya ni aina ya mchakato utakaotumika. Mi sioni umuhimu wa kua na tume,tume zilishakuwepo za jaji Nyalali na Kisanga. Na zilitoa mapendekezo mazuri sana. Kwa sasa,mi nataka elimu juu ya katiba itolewe,then wawakilishi wa makundi yote ya kijamii wakae na kuandaa rasimu,then wanasheria waliobobea ambao watachaguliwa na mkutano wa hayo makundi ya kijamii,wapewe jukumu la kuandika katiba mpya kwa kuzingatia rasimu ya hayo makundi.
 
Nimekisoma Bababiri,nafikiri members wote wa Jamii Forums wangekisoma pengine tungekuwa na majibu mazuri sana ya matatizo mengi tunayopitia kama nchi maskini sijui na pengine kupata majibu ya maswali magumu tunayojiuliza kila siku ya maendeleo,siasa,uchumi na jamii kwa ujumla?
yeah,chachage aliandika kitabu chake cha MAKUWADI WA SOKO HURIA,ukibahatika kisome ndugu-ni riwaya nzuri,dah cku zote watu wazuri ndio hufa mapema,maneno hayo aliwah kuyazungumza shvj pale NKRUMAH HALL UDSM
 
Please jamani, kama kuna mwenye soft copy ya hiki kitabu atuwekeee jamvini. Mbarikiwe sana
 
yeah,chachage aliandika kitabu chake cha MAKUWADI WA SOKO HURIA,ukibahatika kisome ndugu-ni riwaya nzuri,dah cku zote watu wazuri ndio hufa mapema,maneno hayo aliwah kuyazungumza shvj pale NKRUMAH HALL UDSM

Yes, ni kitabu kizuri sana na nilibahatika kuhudhuria mhadhara wake kuhusu kitabu hicho, R.I.P Chachage, kumbukeni ndo huyu aliekataa uwekezaji feki wa MLIMANI CITY na kugawanywa kwa UDSM kuwa na Colleges with reasons
 
Back
Top Bottom