Prof Shivji Ametumwa na Wazanzibari?

Asante mkuu yaani ingekuwa laptop like ingekuhusu.Ngoje niipige hapa hapa kwenye simu.LIKE
Na siyo lazima azungumze kama utakavyo, wala hatoi mihadhara kwa lengo la kukuridhisha kila utakalo. Chukua linalokufaa, potezea lisilokufaa hutabadili lolote
 
Hao tatizo sio muungano, tatizo lao ni udini tu. Hawapendi wakristu, wamejaaa complications kibao, wanasema dini yao hairuhusu kuua, sasa wale wanaolipua wezao kwa kujitoa mhanga ni akina nani?? si wao wenyewee?? kama maisha yamemshinda si ajinyongee mwenyewe pekeyake.

makanisa ndio yanayotumika kuwanyonya wazanzibari, kama yalivyo tumika katika vita vya Rwanda na Burundi.
 
Kutumwa maana yake nini??
Prof Shivji na mtu mwingine yoyote ambae hana bias ataongea lugha hiyo hiyo! Muungano una mapungufu hata ccm,chadema,nccr,makanisa na misikiti yote yanafahamu hili... Na ukisikia mapungufu ya Muungano ujue waathirika ni Zanzibar kwa asilimia kubwa! So kwa ushauri bwana mtoa hoja jipange uwe positive next time, Prof Shivji anaongea mambo kama yalivyo... Wenye ubongo mdogo lazima waogope kumsikiliza sababu hawajazoea kusikia Ukweli ukitamkwa Hadharani!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
tumwache prof aelimishe umma juu ya katiba ya sasa ili Watanzania wawe na uelewa mzuri wa kuchangia maoni yao badala ya kuachia vikundi vichache vya watu kuwasemea hivyo si busara kuanza kuhoji Prof Katumwa na nani wakati huu kwani yaliyotekea zanzibar na matamshi ya prof ni coincidence tu ,mimi binafsi nimependa kipindi chake
 
prof. issa chivji ametoa historia zote mbili bara na zanzbar inaonekana ww umefatilia mhadhara uliopita tu mfatilie utamwelewa...pia suala la udini zanzbar si sahihi kwa sbb makanisa yapo mda mrefu mbona hayajachomwa? mfano- sehem ya kihistoria jengo lililokua ni soko la watumwa enz hzo limegeuzwa kanisa kwann wazanzbar wacngekataa tangu kitambo huu ni mchezo ulipangwa ionekane waislamu wa zanzbar wabaya sio sahihi na pia bar wakat zinachomwa moto unaona watu wanafungua bia wanakunywa wakat mafundisho ya d
 
km huyu jamaa ni mmoja wa wahuni ,basi haaminiki.Anaweza mwaga junks zake nyingi zikawa nzuri na baadaye akamwaga moja uozo,then uozo, then wahuni wakaanza mlinda, then ukagundua kuwa naye kapata umaarufu kwa style ile ile ya "great...", "great historian" professor wa kigoda cha Nyerere halafu kidogo anaanza "uhuni" umanipualte watu kupitia uzalende na link ya nyerere "ku -arabize taifa na kila kilichopo".Jamaa ana unlimitted access to propaganda runway.
 
Chai chapatimaharage mchuziii vyaa jengamwili X 2
Chai chapatimaharage mchuziii vyaa jengamwili X 2

mayai aaaa, maziwa vyaa jengamwili X 2
Maini aaaa, dagaa vyaa jengamwili X 2

Chai chapatimaharage mchuziii vyaa jengamwili X 2
 
Kama Wazanzibari walikaa kimya wakati Mambo ya Muungano yanaongezwa Bungeni, kinachomuuma Prof ni nini hapo?
Kwani Ni BUnge gani Mkuu?La Jamhuri?Au la Tanganyika? Wale wabunge za Zenji walikuwa wakifanya nini?.Terroism ni ushetani kwani huwa inapata nguvu hata kwa vict wake.Tazama unakuwa useful i.d.i.o.t
 
Reasoning yako ni nzuri ila conclusion yako inaonysha kama reasoning umesaidiwa. Prof. Kawaeleza Watanzania historia ya muungano na maoni yake ya wakati muungano unaundwa kama mtafiti.
Hivi wewe kila msomi wa tanzania n Historia yake unaiamini?Bongo hatuna standards zinzozingatiwa na kuaminika hata na wanazozisimamia.TBS wenyewe hawaaminiki hata na wafanya biashara wa nje na hata wawekezaji wanaotaka peleka vitu vyao nje kwani wao hutumia ISO na nyingine.Sabau ya msingi kuwa TBS inaangalia final product lakini quality control and assessment inaanzia ktk initial stage za production hadi ktk product, na mara nyingi hadi ktk raw material.Uliza wauza asali wakibongo na asali zao zenye sumu za mimea na soko la ulaya.

Professor Shivji, na a bunch of intelctuals wa kibongo, + wa REDET ni mazao ya siasa za zilizochanganyika na ukomunisty,mashariki ya kati na siasa za mtazamo wa kimapinduzi.Kazi zao ni manipulation kwa faida za mitazamo yao, na upande fulani.wametumia utaalamu wao na support ya makundi fulani kuibuka km waliobobea na baadaye kukabidhiwa vizazi vya wasomi waliopitia UDSM ili kubrainwash kadir iwezekananvyo, ndio maana ni vigumu Lissu na hata ma judge, madr. etc waliokuwa wanafunzi wake waliwekwa mizizi ya kufikiri km yeye, na hivyo hawawezi mshinda prof kwa kutumia mfumo wa kifikra ulioasisiwa na prof mwenyewe...So sasa ana piga free ride.

Unashangaa nikuambiacho ,utashangaa zaidi kumsikia mnyika anavyokwenda na mwanasheria mkuu bungeni hadi mabadiliko husika yanakubaliwa na Mnyika hana elimu ya darsani kama ya huyu jamaa.Sababu ni kwamba mnyika hakubaatika kuwa corrupted na fikra zao kwa hivyo ana addtional angle ya kuangalia tafsiri zao uku akiwa na freedom ya kutumia ubongo.In contrary wabunge na makda wa CCm hawaoni tofauti kwa vile wamekuwa programmed kufikiri kwa namna hiyo na kutotakiwa fikiri kwani chama kinaelewa kufikiri vyema zaidi kupitia mwenyekiti.

Bongo kuna version za historia za kila kiongozi na watu wake, wale wazee wa Yanga wana historia zao ktk ukombozi wa nchi na club yao kupitia michezo na wana command respect and recongition(unabisha muulize Mengi),Kuna wazee wa dar wan heroes/heroins wao na ndio wanabariki CCM kila mwaka ktk mkutano wa wazee.Na historia zao Si hizi tunazozisoma kuhusu baba wa Taifa na Simba wa nyika.Then kuna sijui akina Kombo, kuna kizazi ch akina Sykes,babu etc wan version yao, ya kila kitu hadi kuwa na Nchi,bado hujapita mikoani ukakuta wasisi wa TANU huko..wana version zao.Kuna version za Dini.Ukristu una zake, uislam una version zake zake za historia(Na wanadai share zao katika uhuru).

Cha kujiuliza Prof...ktk roho zake na balance zake ni vipi atakuwa consistency pale historia na malengeo ya makundi yenye maslahi kwake yanapingana na version yake anayotaka itoa ktk public.Ama uasia wake, dini yake, au umaarufu binafsi.

Na pia ujue kuna rubbish nyingi ktk historia tusomazo shule kuanzia shule za msingi hadi vyuo.Kwani imeandikwa si kwa misingi ya historia bali kutokana na kulinda mslahi ya mud amrefu ya matabaka fulani.Historia ikipingana na haya makunid inaitwa ya uogo.
 
Na siyo lazima azungumze kama utakavyo, wala hatoi mihadhara kwa lengo la kukuridhisha kila utakalo. Chukua linalokufaa, potezea lisilokufaa hutabadili lolote
Kwanini basi asizungumze na kutoa mihdhara km inavyohitajika na jamiiyetu?
 
shivji ni mkweli acha kuongea kama magamba wewe
Una hakika? kwanini basi pamoja na matamshi yake kuwa makali kuliko ya kina Baregu na wengine walijikuta UDSM si mahali pao.Na pia kapewa Kigoda cha baba wa taifa.Na ikibidi pamoja na kufagiliwa sana ili kutia uzito anachoongea,historia zake atoazo zinalandana na za wale wasiomkubali mwalimu kuwa baba wa taifa na pia nafsi yake ktk uleta uhuru.

km asingekuwa na masalahi na magamba angekuwa univeristy fulani za wahuni,au hata na kina baregu.
 
Huyu Prof ukimwangalia kwa makini kwenye Mhadhara wa Katiba katika ITV leo anaonekana kuwatetea Wazanzibari badala ya ku-balance mambo:
Anadai kwamba eti kuongeza mambo ya Muungano, Wazanzibari waliokuwa kwenye kuongeza mambo ya Muungano "
walikuwa hawaongei sana," na Karume alikuwa hajali! Sasa kama walikuwa hawasemi sana, mimi sioni tatizo, si wamekubaliana?
Hapa Prof Simwelewi kabisa, ni kama katumwa vile!

Huyu prof. Shivji ili kuamua kama anapendelea wazanzibar au la, ni vizuri kuifuatilia falsafa yake ya sheria kuhusiana na muungano. Mimi nimepata kusoma maandiko yake mengi kuhusiana na muungano na mengine ameyaandika miaka ya 80 na 90. Msimamo wake siku zote umekuwa kwamba msingi wa muungano wa Tanzania ni Mkatataba wa Muungano wa 1964. Kwa maoni yake, Katiba ya Jamhuri ya Muungano ilipaswa kuuzungumzia muungano kwa namna ile ile ulivyokusudiwa katika Mkatba wa Muungano. Falsafa ya Prof ni kwamba makubaliano ya tunaungana katika mambo gani yalijengwa na Mikataba ya Muungano. Haikuwa sahihi, kwa maoni yake, kwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano kurekebishwa ili kuonngeza masuala ya muungano bila kuwa na mkatba mpya kati ya nchi zilizoungana ili kuhalalisha masuala hayo mapya.

Maoni yake katika hili yanatokana na mtizamo wake wa kuwepo asili ya sheria iliyo juu katika msonge mzima wa sheria ambayo baadhi ya magwiji wa zamani wa falsafa ya sheria wanaita "Grandnorm". Kwa mtizamo wake Mkatba wa Muungano ndio "Grandnorm" ya Katiba ya Jamhuri ya Mungano ya 1977. Kwa hali hiyo, kwa maoni yake, huwezi ukawa na marekebisho ya Katiba ya 1977 yanayokinzana na "Grandnorm" ya katiba hiyo bila kuifuta katiba hiyo na kuandika nyingine.

Japo kuna kambi mbili zinazokinzana katika maoni haya, mtizamo wa prof unapaswa kuheshimiwa kama msimamo wake wa kianazuoni na kama kuna mabishano ni bora yakawa mabishano ya kianazuoni na sio kama yeye napendelea upande wowowte wa Muungano. Mmoja wa wanazuoni wa sheria anayepingana nayo katika falsafa hii ni Prof Kabuda ambaye naye amezama sana katika falsafa ya sheria ya katiba na ameandika majuzuu mengi katika mada hii.
 
Mimi ningewaomba wachangiaji tuwe fair na watu tunaowajadili bila wao wenyewe kuwepo.

Kwa waliopitia UDSM hata kaka yangu Tundu Lisu, prof Shivji anabaki kuwa anaheshimika katika fani ya sheria bila kujali kwamba tunamuunga mkono au la katika falsafa zake za sheria. Yapo mambo mengi ambayo tunatofautiana naye na huo ndio ukomavu wa kitaaluma. Lakini hilo haliwezi kunipa haki miimi na watanzania wengi tuliopitia chuo cheti ya Dar Es Salaam kukanisha mchango wake mkubwa katika ufahamu wangu wa sheria. Hoja nyingi tunazozijenga kuhusiana na mapungufu yaliyomo katika katiba yetu zina mchango mkubwa wa prof Shifti. Hata submission aliyofanya kiongozi wa upinzani Bungeni kuhusiana na Sheria ya Mabadiliko makubwa ilikuwa ina simenti nyiki zinazotokana na tanukuru za prof japo baadhi ya conclusions alizozitoa zilipingana na falsafa zake. Na hio ndio kawaida ya wasomi.

Kwa unyenyekevu mkubwa ningewaomba wana JF wenzangu tujenge tabia ya kujadili hoja badala ya kujadili mtu. Maana hoja za mtu hubadilika bali mtu hubaki yule yule. Mfano mzuri ni DR Slaa. Dr Slaa wa leo ambaye ni mwenyekiti wa Chadema ni yule yule aliyekuwa mwanachama wa CCM. Hata hivyo, mawazo ya mh Dr Slaa ya miaka ya 1994 yanapishana na mawazo na mtizamo wake wa siasa za Tanzania pengine umbali wa anga na mbingu. Tukimjadili yeye kama yeye, tutakuwa tunamuona. Tunaweza kujadili hoja zake bila kumkabili yeye mwenyewe binafsi.
 
..Prof.Shivji ni mtaalamu wa sheria, kwa hiyo mchango wake kuhusu muungano umezama ktk taaluma yake.

..Likija suala la uchumi wa-Zanzibari wanatunyonya sana wa-Tanganyika.

..Tunawapa umeme bure, mishahara ya watumishi wa SMZ inalipwa na wa-Tanganyika.

..pia wa-Zanzibari wanaruhusiwa kumiliki ardhi na majumba huku Tanganyika, wakati sisi tukijaribu kufanya hivyo huko Zanzibar wanatia kiberiti.
 
Nyinyi wakristo wa tanganyika kweli niwapenda haki nyinyi? Kumlaumu profesa shivji kwa kuitetea zanzibar ni kuendelea kudhihirisha chuki zenu tu kwa zanzibar,mara hii lazima tupumue tu.
 
makanisa ndio yanayotumika kuwanyonya wazanzibari, kama yalivyo tumika katika vita vya Rwanda na Burundi.

makanisa yanawanyonya vipi! Au ndo yanayoongoza SIRIKALI yenu? Jaribuni kujenga hoja za msingi, kama hamuutaki muungano muwe na sababu zenye tija na sio kuropoka kwamba makanisa yanawanyonya, wakati hata members wa makanisa hayo ni Wazanzibar.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom