Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 864
Muda mfupi uliopita nimetoka kushiriki kwenye mdahalo wa kuandaa Agenda za Vijana za Tanzania tunayoitaka leo na baada ya uchaguzi kwa kifupi Ilani ya Vijana.
Mjadala huu uliandaliwa na Asasi ya Vijana ya TYVA na umefanyika katika Hotel ya Peacock Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.Mgeni rasmi katika mdahalo huo alikuwa ni Professa Issa Shivji Mwenyekiti wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere.
Katika ufunguzi wake kiongozi huyu machachari na mwenye uchungu wa dhati na nchi hii alisema mambo mengi lakini nitaleza machache yaliyonigusa sana.
Prof alisema kuwa Azimio la Arusha limesahaulika kabisa na alishangazwa sana mwaka 2007 amabpo azimio hili lilikuwa linatimiza miaka 40 lakini Serikali na watu wengine hawakuthubutu kulikumbuka lakini Serikali iliazimisha miaka 30 ya Chama Cha Mapinduzi.
Prof aliturudisha nyuma na kueleza kuwa Kauli Mbiu ya Azimio la Arusha ya Binadamu Wote ni Sawa na Afrika ni moja ni Kauli mbiu muhimu sana na yenye ku-inspire sana.
Akaponda kauli mbiu ya Maisha Bora kwa Kila Mtanzania kuwa hainspire wala haina mvuto badala yake inasababisha kila mmoja kuhangaika kivyake iwe kwa kula rushwa au kwa njia yeyote ile ilmradi tu afikie hayo maisha bora. Akasema Slogan hii ni ya kibaguzi inaleta matabaka.
Habari ndio hiyo.
Mjadala huu uliandaliwa na Asasi ya Vijana ya TYVA na umefanyika katika Hotel ya Peacock Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.Mgeni rasmi katika mdahalo huo alikuwa ni Professa Issa Shivji Mwenyekiti wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere.
Katika ufunguzi wake kiongozi huyu machachari na mwenye uchungu wa dhati na nchi hii alisema mambo mengi lakini nitaleza machache yaliyonigusa sana.
Prof alisema kuwa Azimio la Arusha limesahaulika kabisa na alishangazwa sana mwaka 2007 amabpo azimio hili lilikuwa linatimiza miaka 40 lakini Serikali na watu wengine hawakuthubutu kulikumbuka lakini Serikali iliazimisha miaka 30 ya Chama Cha Mapinduzi.
Prof aliturudisha nyuma na kueleza kuwa Kauli Mbiu ya Azimio la Arusha ya Binadamu Wote ni Sawa na Afrika ni moja ni Kauli mbiu muhimu sana na yenye ku-inspire sana.
Akaponda kauli mbiu ya Maisha Bora kwa Kila Mtanzania kuwa hainspire wala haina mvuto badala yake inasababisha kila mmoja kuhangaika kivyake iwe kwa kula rushwa au kwa njia yeyote ile ilmradi tu afikie hayo maisha bora. Akasema Slogan hii ni ya kibaguzi inaleta matabaka.
Habari ndio hiyo.