Wewe Prof. Abdallah Safari unaimbishiwa wimbo ambao hujui umeanzia wapi?
Utatumika na hao jamaa kama mwavuli kudhalilisha dini yako ukiiisha wanakutupa!
Ukitaka ku-proove gombea uongozi wa juu uone mziki wake
Hutakuwa Prof. wa ukweli tena utakuwa profesa njaa..pole sana
watch out ..we are watch the movie..jitambue
Mi nadhani Prof. Safari amefanya jambo zuri tu kuonyesha msimamo wa chama.
Chama lazima kionyeshe nini kinaamini na sio kuendeshwa na watu wanaojiita viongozi wa dini.
Hii nchi kwa ukweli sio rahisi kupiga hatua mana dini zimeingia sana jamii na watu wanakuwa influenced na statement za watu wachache wanaojiita viongozi wa dini.
Angalau kusikiliza viongozi wa siasa ambao wanachaguliwa na wananchi kuliko hawa wanaojiita viongozi wa dini ambao wengu huwa wanajipa madaraka kama vile wana mawasiliano na Mungu.
Mimi kwa kweli nachukia sana, japo naamini Mungu, lakini viongozi wa dini hasa tanzania mana ndio wanaongeza wananchi kuwa wajinga na waoga kutetea haki zao...na matunda yake ni umasikini.
Embu fikiria watu kama hawa wanaojiita viongozi wa waisilamu, wao wanajali HIJABU kuliko uovu ambao mamilioni ya watu wanafanyiwa na hao viongozi wadhalimu na wengine wanavaa Hijabu au kanzu au misalaba kuficha maovu yao. Huyu DC ni muhalifu kama wahalifu wengine, huwezi kutetea HIJABU na kusahau ukweli kuwa alitaka kuiba haki hata ya waisilamu ambao kweli wanataka mabadiliko.....
kama nchi yetu inasema haina dini mi nashauri ipige marufuku haya matamko yanayotolewa kiholela.....Huyu DC hakuhukumiwa kama Muislamu bali kama mhalifu.....kwani mhalifu wa kiislamu akipelekwa Gerezani wanavaa Hijabu? Ni kwa vile nchi haina dini so....tusiruhusu watu wachache wenye interests zao kupoteza malengo ya watu wanaotaka maendeleo....wao waendelee na imani zao na kuacha sheria isiyokuwa na dini ifanye kazi!