Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,857
- 7,615
Taarifa iliyosomwa Bungeni na Waziri wa Nishati na madini Mh. Mhongo kuwa shule za St. Mary zinazomilikiwa na Mchungaji Getrude Rwakatale ni miongoni mwa wezi wakubwa wa shirika la umeme TANESCO imemvua nguo mama huyu ambaye pia ni mbunge viti maalum kupitia CCM.
Hizi si tetesi tena kwa kuwa mh. Waziri anaushahidi juu ya alichokisema Bungeni, hivyo sijui Mama huyu atakuwa na mahubiri yapi kujishafisha kwa kondoo wake. Pia hali hii inaleta picha kuwa kuna baadhi ya wabunge wamekuwa wakitumia Ubunge wao kama kivuli ili waweze kuiba rasilimali za nchi hii. Inasikitisha kuona mchungaji, mbunge, tena wa viti maalum anafanya upuuzi kama huu.
Kwa ushahidi huu kweli ni rahisi ngamia kupenya katika tundu la sindano kuliko tajiri kuuona ufalme wa mbinguni.
Mkuu acha kuipersonalize hii ishu