Prof. Mbele na hoja zake: Amfagilia JK

Profesa Mbele: Wengi waanza kutambua ubora wa JK

Binafsi, niliona dalili za ubora wa uongozi wa JK tangu mwanzo, na sijaficha maoni yangu, pamoja na kushambuliwa na wengi, wengine wakidai kuwa nawania cheo katika serikali ya JK. Sijawahi kusikia mambo ya kipuuzi kama hayo, kwani mimi naamini kuwa kazi yangu ya ualimu nilipewa na Muumba, tangu nilipokuwa mtoto mdogo. Sijatetereka na sitatetereka; nina nadhiri ya ualimu.

Kuona mazuri ya JK kama kiongozi, kwa upande wangu, si sawa na kuipigia debe CCM. Tangu CCM ianze, nimekuwa nikiishutumu kwa namna mbali mbali, tena kimaandishi, ili kila mtu asome. Nimechapisha hata kitabu, wiki chache zilizopita, ambamo nimeendelea kuishutumu CCM.

Tatizo la waTanzania wengi ni ufinyu wa mawazo. Kwa vile wamezama mno katika siasa za vyama, wanayachukulia masuala kwa mtazamo wa kichama.

Ukisema hivi, wanaangalia unaunga mkono chama gani. Ukisema vile, wanaangalia kwa mtazamo wa chama fulani. Ukweli ni kuwa mimi si mwanachama wa chama chochote. Nina uhuru wa kusema chochote ninachofikiri, hata kama kinawaudhi watu wa chama fulani. Shauri lao na siasa zao za ufinyu na ukandamizaji wa fikra kwa maslahi ya chama.

Katika makala yangu mojawapo, kuhusu safari za JK nchi za nje, nilisema kuwa JK anafanya juhudi kubwa kama kiongozi wa nchi kuitangaza nchi na kutuwekea mazingira muafaka duniani. Lakini nililalamika pia kuwa waTanzania tunaoishi nje tunamwangusha JK kwa kutofuatilia yale anayoyaanzisha. Nilijenga hoja yangu kwa kutumia mfano wa waTanzania tuliko Marekani.

Ningependa kusisitiza jambo hilo. Wakati huu, wa-Tanzania wanaoishi nje wanapigania sheria ibadilike ili iruhusu uraia wa nchi mbili. Hoja moja ya msingi inayotolewa ni kuwa sheria hiyo ikibadilika, basi wa-Tanzania hao wataleta mitaji sana nchini.

Ninaposikia hoja hiyo, najiuliza masuali kadhaa. Kwanza, narudi kwenye usemi wangu wa namna waTanzania tunaoishi nje tunavyoshindwa kuendeleza yale ambayo JK anaanzisha katika ziara zake. Mianya ya kuwekeza nchini, mianya ya kushirikiana na wawekezaji anaokutana nao huku nje, sisi hatuifuatilii. Je, ni kweli kuwa tuna lengo la kuwekeza sana nchini?

Je, ni kweli kuwa bila uraia wa nchi mbili, inakuwa vigumu kuwekeza nchini? Kama ni hivi, mbona watu baki, wa mataifa mbali mbali, wanazichangamkia fursa zilizopo za uwekezaji nchini? Sheria za Tanzania za sasa zinaturuhusu sisi, na watu hao baki kuwekeza, nao wanachangamkia fursa hizo.

Iwapo kweli wa-Tanzania wanaoishi nje wana mitaji, kwa nini wasichangamkie fursa hizo kama hao wageni? Ni mwekezaji gani ambaye hachangamkii fursa zinapojitokeza? Nina mashaka sana hapo, kuhusiana na kinachosemwa na wa-Tanzania wanaodai uraia wa nchi mbili kwa hoja ya uwekezaji. Huenda kuna haja za kubadili sheria za uraia, lakini inatakiwa wanaopigania suala hilo watoe hoja zenye mantiki zaidi.

Watanzania wanaoishi nje wangekuwa wameonyesha ari ya kuwekeza tangu pale nchi ilipofungua milango, ningeielewa hoja hii vizuri. Hao wa-Tanzania wana ndugu zao nchini, na kwa hivi wangekuwa mstari wa mbele katika kuwekeza. Lakini iweje wanaweka pingamizi, kwamba bila uraia wa nchi mbili, wanashindwa kuleta hiyo mitaji yao? Suali linakuja: je, hao wana mitaji kweli? Je, kuna utafiti upi na takwimu zipi zinazothibitisha kuwepo kwa mitaji hiyo, au ni hadithi ya Abunuwasi?

Nafurahi kuwa kadiri siku zinavyopita, wengi wanaanza kutambua ubora wa JK kama kiongozi. Naamini kuwa kwa mahitaji ya nchi yetu, katika hali tuliyo nayo, tunamhitaji kiongozi wa aina yake, ambaye habagui waTanzania kwa msingi wa vyama, wala hajakatishwa tamaa na wale wanaofanya kila juhudi kutotambua juhudi zake za kuipeleka Tanzania mbele.

Nafahamu kuwa nimechanganya masuala hapo juu, lakini nimefanya hivyo kwa kuona kuwa yana uhusiano fulani muhimu.
 
Very interesting indeed. Ndio yale yale ya watu wanaopata Phd za vichochoroni, au watu wanaojiwekea tu title hizo hata bila kujua zaina maana gani kwa kinachotoka mdomoni. Kama huyo "Profesa" angeonesha matano tu ya maana aliyofanya JK yanomfanya yeye amwone bora, basi ningekubali kuwa wenye mashaka kuhusu ubora wa JK wana akili finyu. Otherwise hili litarudi kwa "profesa" mwenyewe.
 
Huyu mtu anaheshima zake kuwa sana katika chuo huku America na pia ni mzuri sana katika English sana
 
Wengi maanake nini? Na ubora unapimwa vipi. Ubora unapimwa kwa ilani ya uchaguzi. Na tangu lini kizuri kikatembezwa baada ya kujiuza? Swala la uraia ni dogo sana kwa watanzania katika bigger scheme of things. This is a very shoddy spin doctoring.
 
..mambo ya kuwapima viongozi wetu kwa "juhudi zao" au "nia njema" za kutuletea maendeleo ndiyo yaliyotufikisha hapa tulipo.

..wakati umefika tuwapime viongozi wetu kwa kuangalia MATOKEO ya "juhudi" zao na hizo "nia njema" za kuleta maendeleo.

..tatizo letu ni kwamba umasikini umetushika kabari kiasi cha kuwa na VERY LOW EXPECTATION kuhusu jinsi gani nchi yetu inapaswa kuendeshwa. Prof.Mbele pamoja na kuishi kwake nje kwa miaka lukuki nadhani amekumbwa na hili tatizo la low expectations.
 
Maelezo ni mazuri, ila sijaona hicho kinachomfanya aone kuwa JK ni kiongozi mzuri! Labda ni kwakuwa anatembelea nchi mbalimbali na hivyo wananchi wa nchi husika kufahamu kuwa kuna nchi inaitwa Tanzania, au ni kitu gani haswa? Nadhani Dr anatakiwa kuweka mambo wazi ili tuweze kuelewa anachotaka kutuambia juu ya JK.

Ukweli ninaoufahamu ni kuwa JK amekuwa kiongozi bora sana wa Tanzania kutembelea mataifa ya wenzie. Pia amekuwa hodari wa kutoainisha gharama na faida zilizotokana na safari zake nyingi nje ya nchi.

Urais, kama taasisi pia hatujui kuwa (labda zaidi ya 40%) ya muda aliotumia kwenye mataifa ya wenzie umeathiri vipi utendaji wake na shughuli zake za maswala ya ndani ya nchi hasa ukitilia maanani kuwa kuna maamuzi ambayo lazima afanye yeye kama rais. Dr. angeyaweka wazi ili tuweze kuupima utendaji wa JK. Ikibidi pia kulinganisha na marais watangulizi wake. Kwani inawezekana tukaona kuwa anaitangaza vyema nchi, lakini mikakati ya kuilinda nchi na rasilimali zake likawa jambo jingine, kwani hilo pia ni jukumu la rais.
 
by the way, prof huwa anapuliza tarumbeta lake? au watu ndio wanatakiwa kumsifia? maana niliona mahali anasema ingawa hatumtambui/kumuheshimu kuna watu wanafanya hivyo huko majuu? mbona sio Shivji akipuliza tarumbeta lake au Mareheme Prof Haroub Othman na wengineyo.
 
Naona huyu Profesa, hakutumia taaluma yake.
Profesa anaweza kutumia maneno kama mengi, ubora, nk. Hayo mambo hayana kipimo. Prof. Mbele tuambie ni yapi hayo mengi na bora. Acha papala ktk uleta sifa.

Unafikia kiwango cha kusema safari zinaitangaza nchi? SAFARI! Bora awe mwanariadha avae jezi ya Tanzania. Tukisha tangazwa na Rais, What next?

Haya prof. Nawe kweli umefikiria.
 
Prof.Mbele,
Hakika wewe ni miongoni mwa wasomi ambao wamebobea tu ktk elimu fulani na wanashindwa kufikiria nje ya elimu hiyo.Sijui Huo Uprofesa umetokana na kipi haswa ikiwa kweli wewe unaweza uliza maswali mengi mazito pasipo kuyafanyia kazi..Hiyo Phd unaipata vipi ikiwa unauliza maswali kuhusiana na Watanzania waishio nje kujenga hoja ya kumsifia Kikwete?..

Pengine jaribu kukaa na hao Watanzania waishio nje uwasilikize jifunze, tunga kitabu kisha njo na takwimu zakokutupa somo badala ya kuuliza maswali.
kwanza hufahamu nini maana ya Mtanzania aishie nje, huyu sii mwekezaji, kukaa kwake nje hakumfanyi awe mwekezaji anapotaka kurudi nyumbani..Diaspora na Foreign Investor ni vitu viwili tofauti kabisa..Mtanzania harudi nyumbani kwa sababu tu ya kuwekeza ati ana fedha kiasi gani?..Hivi kweli unafikiria fedha ndio iwe sababu ya kumruhusu mtu kuwekeza nchini?..Je mwenye elimu yake utamweka wapi fungu gani...Huoni kama ELIMU alopata nje ni mtaji tosha wa kuwekeza nyumbani...Na rais anapokuja nchi za nje husisitiza watu kurudi nyumbani sii kwa kufahamu kwamba Watanzania waishio nje wana mamillioni ya fedha, kwanza hakuna kitu kama hicho.....sijui mwenzetu umeitoa wapi hii?..

Labda nikupe somo dogo sana, jiulize hawa Wachina wanaokuja hapa nchini mwetu na nchi zote za nje inakuwaje wao bado ni raia wa China na wanatambuliwa na nchi yao tena basui kwa kuongezea tu hata hiyo miradi yao unayoiona Kariakoo inaudhamana wa benki za Kichina (creditline)..Inakuwaje hawa watu hufikia hata kuchukua sehemu nzima ya mji na kuibadilisha kuwa Chinatown wakiuza mali zao..

Mkuu wangu, hii ni dunia ya Utandawazi, watu wanasafiri kwenda nchi za nje kuua mali zao na sii kununua mali..wanakwenda nje kupata exposure na elimu ya teknologia ambayo itawawezesha wao kujijenga zaidi kiuchumi, na kufanikiwa kwao ndio kufanikiwa kwa nchi..Wapo watanzania kibao wenye elimu kubwa ktk nyanja mbali mbali ambazo leo imebidi tunawaita wazungu, wahindi ama Wakenya kuja kutusaidia tukiwalipa fedha za kigeni..lakini taabu kwenu kumwita Mtanzania ashike madaraka hayo hayo..

Hawa watu (wageni) hawana uchungu na nchi zetu hata kidogo, watafanya kazi kwa uzito wa mifuko yetu na sii uzalendo wao (pay as U go)..Hivyo dunia imebadilika kabisa mkuu wangu. Hiyop elimu ulokuwa nayo haifanyi kazi ktk dunia hii.. Watu wanakwenda nje kutangaza na kueneza bidhaa na tamaduni zao ili kukuza uchumi wa nchi zao pasipo kutegemea wageni waichue, waipimena kisha kufikiria kama itauzika..
Leo Wajapan kutuletea Sushi majumbani mwetu, kuna kila aina ya chakula cha nje kinauzwa Dar na hata mikoani na biashara hizo zikiendeshwa na wageni ambao ni main importer wa food product toka makwao. Kwa nini sisi tushindwe kufanya hivyo hivyo huko makwao?..Kila super Market hapa nchini imekuwa intoduced na bidhaa za nje sii kwa sababu demand ilikuwepo toka mwanzo ila tumeletewa vitu vipya kuvijaribu na tukavipenda na soko lake likawepo na linaendelea kukua..Matamanio ya binadamu huenda na majaribio yani kitu umekisha kiona, kukionja kisha ndio unajenga mapenzi na sii kufikiria tu kwamba Tanzania kuna nyama ya Nyati basi wazungu watajipanga kutaka kuinunua..

Ndivyo tunavyomhitaji huyo Mtanzania aishie nje kuitangaza mali yetu kwa mfumo huu..Na kama hufahamu nitakujulisha tu kwamba biashara kubwa ya Tanzania Marekani ni uuzaji wa Vinyago.Biashara hii inafanywa na Mtanzania ambaye kwako wewe unataka kufahamu ataweza vipi kuisaidia Tanzania..Huyu Mtanzania ndiye maina Exporter (kusafirisha nje) na main Impoter (kuingiza vinyago Marekani) akitumia mfumo nilioutaja hapo juu..
Mkuu wangu, mjenzi wa soko hufuata wanakoishi watu na sii watu kulitafuta soko la Kariakoo ama Manseze, nikiwa na maana wakati wa kusubiri bidhaa zetu zipate demand soko la dunia umekwisha - ni wakati sisi tunpeleke mali zetu kwao wao ili wapate kuifahamu hata iwe kwa mara ya kwanza na kuzitangaza, kusambaza na hata kuziauza pasipo mkono wa mhindi wala mwarabu..tunaweza kuwa kama waokama tukijipanga na kuelewa tunafanya nini?

Hii ndio sababu unawaona Wachina na watu wa makabila wanakuja kwetu na kuzunguka nchi zote badala ya kusubiri sisi twenda makwao..na ajabu ni kwamba hao hao waChina mnaanza kuwachoka na kudai warudi makwao lakini unashindwa kuelewa kwamba kuna ndugu zako waishio nchi za nje ambao pia wamechokwa ama wanakabiriwa na matatizo kama ya hawa Wachina.. Tofauti moja tu - mentality...Wachina wamejipanga na wanarudisha makwao kila wanachovuna nje na hao Watanzania ni wana haramu waliokimbia nchi,basi bakieni huko huko...A threat to wasomi wazee!
 
Huyu mtu anaheshima zake kuwa sana katika chuo huku America na pia ni mzuri sana katika English sana


Ndugu yangu,
Kuwa na heshima Marekani hakumaanishi kuwa na pointi za msingi kuhusu Tanzania.Huyu profesa ni m-babaishaji flani linapokuja suala la uchambuzi wa masuala ya Tanzania.Pengine ni kwa sababu ya kukaa nje muda mrefu,au pengine anarukia eneo lisilo lake.Yaleyale ya Profesa wa Mifupa kumpa Uwaziri wa Ulinzi.
 
Huyu mtu anaheshima zake kuwa sana katika chuo huku America na pia ni mzuri sana katika English sana


Mtu kuwa na heshima si kila kitu anachosema basi tuzoe zoe kama taka na si kweli kuwa yeye anajua kila kitu na kujua kingereza siyo usomi ndugu JM.
 
Hogwash,

Uprofesa si tija, weka nondo za kipprofesa hapo tuzione.Acha longolongo.

Onyesha data zinazooana na maisha tukuelewe, si visingizio na acrobatics kama Cirque de Soleil.
 
( Kutoka kwanzajamii.com)

Kuona mazuri ya JK kama kiongozi, kwa upande wangu, si sawa na kuipigia debe CCM. Tangu CCM ianze, nimekuwa nikiishutumu kwa namna mbali mbali, tena kimaandishi, ili kila mtu asome. Nimechapisha hata kitabu, wiki chache zilizopita, ambamo nimeendelea kuishutumu CCM.

Tatizo la waTanzania wengi ni ufinyu wa mawazo. Kwa vile wamezama mno katika siasa za vyama, wanayachukulia masuala kwa mtazamo wa kichama. Ukisema hivi, wanaangalia unaunga mkono chama gani. Ukisema vile, wanaangalia kwa mtazamo wa chama fulani. Ukweli ni kuwa mimi si mwanachama wa chama chochote. Nina uhuru wa kusema chochote ninachofikiri, hata kama kinawaudhi watu wa chama fulani. Shauri lao na siasa zao za ufinyu na ukandamizaji wa fikra kwa maslahi ya chama.

Katika makala yangu mojawapo, kuhusu safari za JK nchi za nje, nilisema kuwa JK anafanya juhudi kubwa kama kiongozi wa nchi kuitangaza nchi na kutuwekea mazingira muafaka duniani.

Ningependa kusisitiza jambo hilo. Wakati huu, wa-Tanzania wanaoishi nje wanapigania sheria ibadilike ili iruhusu uraia wa nchi mbili. Hoja moja ya msingi inayotolewa ni kuwa sheria hiyo ikibadilika, basi wa-Tanzania hao wataleta mitaji sana nchini.
Ninaposikia hoja hiyo, najiuliza masuali kadhaa. Kwanza, narudi kwenye usemi wangu wa namna waTanzania tunaoishi nje tunavyoshindwa kuendeleza yale ambayo JK anaanzisha katika ziara zake. Mianya ya kuwekeza nchini, mianya ya kushirikiana na wawekezaji anaokutana nao huku nje, sisi hatuifuatilii. Je, ni kweli kuwa tuna lengo la kuwekeza sana nchini?
Nafurahi kuwa kadiri siku zinavyopita, wengi wanaanza kutambua ubora wa JK kama kiongozi. Naamini kuwa kwa mahitaji ya nchi yetu, katika hali tuliyo nayo, tunamhitaji kiongozi wa aina yake, ambaye habagui waTanzania kwa msingi wa vyama, wala hajakatishwa tamaa na wale wanaofanya kila juhudi kutotambua juhudi zake za kuipeleka Tanzania mbele.
Nafahamu kuwa nimechanganya masuala hapo juu, lakini nimefanya hivyo kwa kuona kuwa yana uhusiano fulani muhimu.
CHANZO: Kwanzajamii.com


Kama kweli prof. Mbele umeandika habari hii basi u prof wako ni wa darasani tu nilifikiri utavitaja vitu vinavyokufanya uone ubora wa JK lakini zaidi umesifia safari zake kama ndio ubora wa uongozi.

Ndugu yangu prof. ni kitu gani kilikufanya uiponde CCM na JK kwenye kitabu chako halafu baada ya wiki chache kama ulivyosema umeanza kumsifia JK tusema hizi wiki chache amefanya nini unachoweza kutuambia

Unaaibisha hadhi ya uprof. huwezi kuandika kitu kama hiki kisichoendana na heading yake uchambuzi wa masuala mbalimbali unaujuzi wake si kulipuka tu alimradi wewe ni profesa ndiyo maana paragraph yako ya mwisho umekubali kuwa umechanganya mambo.

Kuna mwalimu mmoja aliniambia naye ni profesa kadri mtu anavyopata elimu ya juu zaidi ndivyo anavyogundua kuwa hajui vitu vingi kwa sababu anakuwa ume specialize kwenye kitu kimoja zaidi basi usichanganye mambo.
 
..mambo ya kuwapima viongozi wetu kwa "juhudi zao" au "nia njema" za kutuletea maendeleo ndiyo yaliyotufikisha hapa tulipo.

..wakati umefika tuwapime viongozi wetu kwa kuangalia MATOKEO ya "juhudi" zao na hizo "nia njema" za kuleta maendeleo.


..tatizo letu ni kwamba umasikini umetushika kabari kiasi cha kuwa na VERY LOW EXPECTATION kuhusu jinsi gani nchi yetu inapaswa kuendeshwa. Prof.Mbele pamoja na kuishi kwake nje kwa miaka lukuki nadhani amekumbwa na hili tatizo la low expectations.

Hivi unajua kuna president mmoja kapewa Nobel Prize kwa juhudi na nia njema??
 
Duh! nimesoma hiyo article kwa kifupi umenihuzunisha sana. Tatizo la professor Mbele ni asa na baadhi ya maproessor wengi Tz, they have their own world! professor kaandika hiyo article kana kwamba Tanzania ni USA!

Ataendela kujificha kwanza jamii huko, kama yeye mwanaume aje humu jamvini kwanza ajifunze kujibu hoja na kuwasha hoja

aliachoandika hapo juu nashindwa nijibu wapi nianzie wapi, sana sana namalizia kwa kuona hili zezeta

kuna haja ya kuanza kummulika kuna thread ya MKJJ ya 'huyu ni nani' tuendelee na huyu

Yes , usije ukakuta si mtanzania, au ana lake jambo!!

I consider professor Mbele as the enemy of Tanzania!
 
Kujiaibisha bure.... english literature na political science wapi na wapi!
 
( Kutoka kwanzajamii.com)



Binafsi, niliona dalili za ubora wa uongozi wa JK tangu mwanzo, na sijaficha maoni yangu, pamoja na kushambuliwa na wengi, wengine wakidai kuwa nawania cheo katika serikali ya JK. Sijawahi kusikia mambo ya kipuuzi kama hayo, kwani mimi naamini kuwa kazi yangu ya ualimu nilipewa na Muumba, tangu nilipokuwa mtoto mdogo. Sijatetereka na sitatetereka; nina nadhiri ya ualimu.
Kuona mazuri ya JK kama kiongozi, kwa upande wangu, si sawa na kuipigia debe CCM. Tangu CCM ianze, nimekuwa nikiishutumu kwa namna mbali mbali, tena kimaandishi, ili kila mtu asome. Nimechapisha hata kitabu, wiki chache zilizopita, ambamo nimeendelea kuishutumu CCM.
Tatizo la waTanzania wengi ni ufinyu wa mawazo. Kwa vile wamezama mno katika siasa za vyama, wanayachukulia masuala kwa mtazamo wa kichama. Ukisema hivi, wanaangalia unaunga mkono chama gani. Ukisema vile, wanaangalia kwa mtazamo wa chama fulani. Ukweli ni kuwa mimi si mwanachama wa chama chochote. Nina uhuru wa kusema chochote ninachofikiri, hata kama kinawaudhi watu wa chama fulani. Shauri lao na siasa zao za ufinyu na ukandamizaji wa fikra kwa maslahi ya chama.
Katika makala yangu mojawapo, kuhusu safari za JK nchi za nje, nilisema kuwa JK anafanya juhudi kubwa kama kiongozi wa nchi kuitangaza nchi na kutuwekea mazingira muafaka duniani. Lakini nililalamika pia kuwa waTanzania tunaoishi nje tunamwangusha JK kwa kutofuatilia yale anayoyaanzisha. Nilijenga hoja yangu kwa kutumia mfano wa waTanzania tuliko Marekani.
Ningependa kusisitiza jambo hilo. Wakati huu, wa-Tanzania wanaoishi nje wanapigania sheria ibadilike ili iruhusu uraia wa nchi mbili. Hoja moja ya msingi inayotolewa ni kuwa sheria hiyo ikibadilika, basi wa-Tanzania hao wataleta mitaji sana nchini.
Ninaposikia hoja hiyo, najiuliza masuali kadhaa. Kwanza, narudi kwenye usemi wangu wa namna waTanzania tunaoishi nje tunavyoshindwa kuendeleza yale ambayo JK anaanzisha katika ziara zake. Mianya ya kuwekeza nchini, mianya ya kushirikiana na wawekezaji anaokutana nao huku nje, sisi hatuifuatilii. Je, ni kweli kuwa tuna lengo la kuwekeza sana nchini?
Je, ni kweli kuwa bila uraia wa nchi mbili, inakuwa vigumu kuwekeza nchini? Kama ni hivi, mbona watu baki, wa mataifa mbali mbali, wanazichangamkia fursa zilizopo za uwekezaji nchini? Sheria za Tanzania za sasa zinaturuhusu sisi, na watu hao baki kuwekeza, nao wanachangamkia fursa hizo.
Iwapo kweli wa-Tanzania wanaoishi nje wana mitaji, kwa nini wasichangamkie fursa hizo kama hao wageni? Ni mwekezaji gani ambaye hachangamkii fursa zinapojitokeza? Nina mashaka sana hapo, kuhusiana na kinachosemwa na wa-Tanzania wanaodai uraia wa nchi mbili kwa hoja ya uwekezaji. Huenda kuna haja za kubadili sheria za uraia, lakini inatakiwa wanaopigania suala hilo watoe hoja zenye mantiki zaidi.
Watanzania wanaoishi nje wangekuwa wameonyesha ari ya kuwekeza tangu pale nchi ilipofungua milango, ningeielewa hoja hii vizuri. Hao wa-Tanzania wana ndugu zao nchini, na kwa hivi wangekuwa mstari wa mbele katika kuwekeza. Lakini iweje wanaweka pingamizi, kwamba bila uraia wa nchi mbili, wanashindwa kuleta hiyo mitaji yao? Suali linakuja: je, hao wana mitaji kweli? Je, kuna utafiti upi na takwimu zipi zinazothibitisha kuwepo kwa mitaji hiyo, au ni hadithi ya Abunuwasi?
Nafurahi kuwa kadiri siku zinavyopita, wengi wanaanza kutambua ubora wa JK kama kiongozi. Naamini kuwa kwa mahitaji ya nchi yetu, katika hali tuliyo nayo, tunamhitaji kiongozi wa aina yake, ambaye habagui waTanzania kwa msingi wa vyama, wala hajakatishwa tamaa na wale wanaofanya kila juhudi kutotambua juhudi zake za kuipeleka Tanzania mbele.
Nafahamu kuwa nimechanganya masuala hapo juu, lakini nimefanya hivyo kwa kuona kuwa yana uhusiano fulani muhimu.
CHANZO: Kwanzajamii.com

Upuuzi mtupu!Hakuna corelation yoyote hapo,profesa mzima anashindwa kukaa chini na kuandika hoja zenye msingi,profesa huyu ni mvivu wa kufikiri....Halafu akamalizia kwa kusema kuwa eti anafahamu kuwa amechanganya lakini vina uhusiano.....hopeless.....Ufanisi wa kazi wa JK una uhusiano gani na uraia wa nchi mbili?Uraia wa nchi mbili utawaletea watanzania wote maisha bora?Upuzzi mtupu!
 
Prof. Mbele weka vigezo vingine licha ya "JK kuitangaza Tanzania nchi za nje" ambavyo unadhani vinakufanya kutambua huo ubora wa JK kama kiongozi. Tumeweka mabalozi kuitangaza Tanzania huko nje - JK anaweza kuongezea huo utangazaji lakini si sifa ya kutufanya tupige vigelegele kuwa tuna kiongozi bora! Tanzania ina matatizo mengi ya msingi ambayo JK anapaswa kuyatatua kama kiongozi na si kila leo kutembeza bakuli akitangaza 'umaskini' wa Tanzania wakati tuna utajiri kibao. Tatizo ni udhaifu wa JK katika kuhakikisha rasilimali tulizo nazo zinatumika kuinua kipato cha mtanzania na kujenga nchi. Kama JK angekuwa na huo uongozi bora unaoupigia upatu, basi watu wasingefanya ufisadi kama ajira. Uongozi bora ni pamoja na kuchukua hatua madhubuti katika kuhakikisha nchi inaendelea kwa matumizi bora ya rasilimali ilizonazo pamoja na kutafuta teknolojia na uwekezaji makini si huu wa mwekezaji kulipa mrahaba wa asilimia 3 na yeye kuondoka na asilimia 97. Kiongozi hapimwi ubora kwa ziara ngapi kafanya nje ya nchi, bali uchumi wa nchi umepanda kwa kiasi gani tangu aingie madarakani. Sidhani kama JK hata ile ahadi ya ajira milioni moja keshatimiza hata robo yake labda kama anajumuisha na wapiga debe!

Unadai "Tatizo la waTanzania wengi ni ufinyu wa mawazo" - ungejiuliza nini kinasababisha hao watanzania kuwa na "ufinyu wa mawazo". Watakosaje ufinyu wa mawazo wakati wana lishe duni, elimu duni, uelewa duni huku kila kukicha wakiambiwa ni 'kisiwa cha amani na utulivu"? Amani ipi huku nchi ikiendelea kuporwa? Utulivu upi nchi ikiendeshwa kisiasa na utaalamu kuwekwa kapuni?

...kwa taarifa yako kadiri siku zinavyopita, wengi wa watanzania wanaanza kutambua udhaifu wa JK kama kiongozi licha ya propaganda za kumpamba kila siku!
 
Back
Top Bottom