Prof. Maji Marefu Bungeni aonya waganga wa jadi kutodharauliwa

mkuu usiseme hivyo, unaweza kwenda kwenye kisanduku cha kura na hasira zote kwamba iwe na iweje huumpigii kura kufika pale ndio kwanza unapowe vema ya ndio bila kujua ndio kwake. inabidi tujue huyu jamaa alishinda kwa kura ngapi huko jimboni kwake, tunaweza pata picha

Thubuuuut! Any empirical evidence?
 
Ukishangaa ya musa utaona ya …! subiria kuona shekhe Yahaya nae mjengoni ili hata wakiwa kwenye misafara ya mzee wa kabunda nyau kama timu ya ufundi tusisitukie kitu!si wabunge wako kwenye msafara.
 
Mbunge wa Korogwe Vijijini Mr. Ngonyani au almaarufu Prof. Maji Marefu ameanza rasmi kuchangia bungeni sasa hivi. Na katika shukrani zake amewapongeza waganga wa jadi wote nchini kwa kumwuunga mkono na kuwezesha kuchaguliwa kwake.

Hii inamaanisha nini? ni kwamba huyu jamaa waganga au wachawi wamechangia kwa kiasi kikubwa katika kuchaguliwa kwake kuwa mbunge. Kwa maana nyingine huyu bwana ameingia bungeni kugombea maslahi ya waganga wenzake.

Na ameanza rasmi kuwaonya wanaowadharau na kuwa donoa donoa waganga wa jadi. Ameonya kila mtu inampasa aheshimu fani ya mwenzake

hii inanifanya ni amini kuwa hata waliopiga kura inawezekana kwa macho walionekana ni watu lakini kimazingaumbwe walikuwa ghosts na hii inaonyesha kwa mtaji huu atakuwa mbunge mpaka atakapoamua kuacha mwenyewe.

Yes,ukishaona taifa viongozi wake wanakula sahani moja na wachawi na waganga(to me they are all witches),ujue taifa hilo limesambaratika.Mimi pia nina hakika kwamba Ngonyani kaingia bungeni kwa kutumia nguvu za kichawi na yuko bungeni si kwa ajili ya wananchi anaodai wamemchagua, ila kwa ajili ya kutimiza ajenda za wachawi wa Tanzania na dunia nzima kwa ujumla.
 
PORAFEZA MAJIMAFUPI ATANGAZA BIASHARA BINAFSI YA UGANGA
BUNGENI KWA GHARAMA YA NANI??


Mbunge wa Korogwe Vijijini Mr. Ngonyani au almaarufu Prof. Maji Marefu ameanza rasmi kuchangia bungeni sasa hivi. Na katika shukrani zake amewapongeza waganga wa jadi wote nchini kwa kumwuunga mkono na kuwezesha kuchaguliwa kwake.

Hii inamaanisha nini? ni kwamba huyu jamaa waganga au wachawi wamechangia kwa kiasi kikubwa katika kuchaguliwa kwake kuwa mbunge. Kwa maana nyingine huyu bwana ameingia bungeni kugombea maslahi ya waganga wenzake.

Na ameanza rasmi kuwaonya wanaowadharau na kuwa donoa donoa waganga wa jadi. Ameonya kila mtu inampasa aheshimu fani ya mwenzake

hii inanifanya ni amini kuwa hata waliopiga kura inawezekana kwa macho walionekana ni watu lakini kimazingaumbwe walikuwa ghosts na hii inaonyesha kwa mtaji huu atakuwa mbunge mpaka atakapoamua kuacha mwenyewe.

Hivi ndio sehemu rasmi ya kamati ya ufundi wa CCM hii katika karne ya 21 sio??

Watanzania baaado tunayo safari ndefu sana kupata bunge KIWANGO chenye ubora unaoendana na huu wakati wetu!!! Hapana sina utani hapa hata kidogo jamani hebu fikirieni kwamba kichwa cha aina hii ndio kabisa utaikuta eti ni Mwanakamati ya bunge pengeni hata wa kuamrisha Profesa Nkoma wa tume ya Mawasiliano, Mutamwega wa kile chama cha Mbatia au hata Prof Mukandala kwenda kujieleza mbele yake kuhusu maendeleo yetu.

Msicheke hata kidogo kwani wataalam wengi wa nchi hii hasa huko katika Halmashauri zetu mbalimbali nchi WANATESEKA KWELI NA HATA WANANCHI TUNAFIKIA MAHALA KUWAONA WATU WA OVHYO KABISA kushindwa kutumia elimu yao kuwa chachu ya kutuletea maendelea tunayoyataka. Sababu kubwa ni kwamba MABOSI WAO NI MADIWANI ambao wengi wao ndio hao hao akili za akina PORAFEZA MAJIMAFUPI; kila wanaloambiwa kitaalam wao kazi yao ni kupinga tu na hata kukupiga uhamisho ka si juju.

Bwanae, demokrasia inayofanya kazi ipasavyo ni SHARTI IPEWE MWELEKEO MZURI; wananchi tunataka

(1) elimu ya chini zaidi kugombea udiwani walau Diploma na uzoefu wa kazi wala miaka mitano;
(2) Umeya, walau Digri ya kwanza, ki-Diploma juu na uzoefu wa kazi miaka 8;
(3) Mwenyekiti wa serikali za Mitaa; walau Form 6 na uzoefu wa kazi ya aina hiyo kwa miaka 3;
(4) Mkurugenzi wa Manispaa / Jiji, wawe na Digri za pili katika eneo la utawala na uzoefu walau wa miaka 3;
(5) Wakuu wa Mashirika yetu ya Umma; walau digrii ya pili na ka Diploma juu na uzoefu wa kazi za aina husika kwa walau miaka 8
(6) Uongozi wa nafasi yoyote kisiasa chamani (ambayo yote ni mali ya umma) kuanzia Wilayani kwenda juu; walau digree ya kwanza na uzoefu wa kazi ya uongozi kwa zaidi ya miaka 5;
(7) Katibu kata; Digrii ya kwanza na uzoefu wa kazi za utawala kwa walau miaka 5;
(8) Ukuu wa Wilaya awe na walau Digree ya kwanza katika eneo la utawala, uzoefu wa kazi miaka 5;
(9) Ukuu wa Mkoa Digri ya pili katika Utawala na uzoefu wa kazi miaka 10; Ubunge,
(10) Nafasi yoyote Ubalozini; walau Digri ya pili na uzoefu wa kazi miaka walau 5;

Hivi kweli huyu Porafeza Majimafupi pindi Profesa Mwandosya anapoangusha tirio kuhusu MABADILIKO YA TABIA YA NCHI na jinsi itakavyowaathiri wakulima wa vijiji vya Korogwe na viunga vyake na kutaadharsha mtu yeyote kutokata miti ovyo, kuchuna mgongo wake, majani wala kuchimbua mizizi kwa sababu zozote zile na Mhe Zitto Zuberi Kabwe kutia lesi katika fikra hizo kwamba sheria za umiliki wa ardhi vijijini hairuhusu kurandaranda ovyo katika misitu ilioko nje ya mipaka uliomegewa na uongozi wa kijiji, hivi kweli huyu bwana naye bado yumo tu????

Jamani hebu fikirieni matatizo ya umeme ambayo yanamnyima hata huyu baba kufanya mazingaombwe yake, Magomeni barabara ya Kawawa, na kukutana na Wadanganyika wengi zaidi katika imani yake hiyo, ajira kupungua kwa wananchi ya Korogwe, Dowans kuzulumu wakulima wake wa maeneo ya jirani pale lakini yeye anainuka Bungeni na kuanza tu kujitangazia biashara yake ya uganga wa kienyeji!!!!!

Hapana, 'Prof.' Majimafupi aende Korogwe akawalipe kabisa HELA YA MATANGAZO YA BIASHARA BINAFSI bungeni huku akitumia kiti chao na kutelekeza yale mambo ya msingi waliomtuma huko. Hakika huu ni mfano mzuri sana wa aina ya Wabunge wengi sana tulionao wanaoenda kule mjengoni hasa kwa ajili ya biashara binafsi.

Kwa jinsi hii ya KUTAFUTA KUIHEMEA DEMOKRASIA YA NCHI HEWA SAFI YA ELIMU katika nafasi mbali mbali nchini hakika tutakua tumejiweka tayari KUPIGA HATUA KIMAENDELEO, kuchukua muda mfupi zaidi kuelewa mambo na kutoa maamuzi yenye tija, ubunifu zaidi na uwajibikaji mkubwa kazini, kuondoa tabia za uswahilini kama vile fitna, mizengwe na umbeya usioletea taifa tija na maendeleo.

Wananchi tunakwama mambo mengi sana kwa sababu watumishi wetu katika ofisi za kiserikali au za kisiasa hatujaweza KUTOA NAFASI NA MWONGOZO WA KISHERIA kuipa nafasi kwa Elimu tunayoilipia sana kwa kodi zetu KUTUTUMIKIA IPASAVYO kwa maendeleo zaidi.

Watanzania TUTAFAKARI HILI KIUNDANI NA TUCHUKUE HATUA kuendana na hali halisi ya karne ya 21 na ushindani wake!!!
 
Back
Top Bottom