Kiuchumi kushuka kwa bei za bidhaa mbalimbali kunawezekana, nadhani Lipumba akiwa kama mchumi analielewa hili vizuri sema tuu labda alipitiwa au alikuwa na maana ya tofauti au alikosa muda wa kulielezea kwa kinagaubaga pale alipohoji hoja ya Dr. Slaa kuhusu kushusha bei. Kiuchumi ni wazi kabisa kuwa serikali ina uwezo mkubwa wa kushusha au kushindikiza ushushaji wa bei za vitu nchini. Kama prof alisahau hili naomba ni mkumbushe baadhi ya concept kwenye uchumi ambazo zinaweza kumpa mwananchi nafuu kwenye bei. Baadhi ya topic hizo ni price discrimination(bei ndogo kwa watu wa kipato kidogo na kubwa kwa watu wa kipato kikubwa), government interventionist, subsidies (serikali inauweza kumlipia mwananchi asilimia fulani ya bei), Supply theories (ongezeko la makampuni ya watoa huduma hushusha bei ya huduma) etc. Hivyo hapa Prof. Lipumba kama alimaanisha alichosema basi alikosea kwani kiuchumi bei kushuka inawezekana.