M/kiti wa CUF Prof ibrahim Lipumba amesema inawezekana kila Mtanzania kulipwa sh 450000 kwa mwaka kutokana na raslimali zilizopo nchini. Prof Lipumba aliyasema hayo Dar es salaam jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya mwembeyanga na kusisitiza kuwa fedha hizo zinaweza kulipwa kama watanzania wataamua kuweka kipengele hicho kwenye katiba Mpya. "Tanzania ina raslimali nyingi za asili kama bahari, gesi, madini ya dhahabu, tanzanite, mbuga za wanyama na nyingine nyingi ambazo zinaweza kuingizia Tanzania sh. bilioni 2 kwa mwaka ambazo zinatosha watanzania milioni 40 kugawana sh. 450,000 kwa mwaka.