Prof Lipumba azidi kumshambulia Mengi

kutoka mwananchi

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF) Taifa, Profesa Ibrahim Lipumba amesema malumbano ya wafanyabiashara yanayoendelea kushika kasi nchini kuhusiana na ufisadi, hayana tija kwa taifa badala yake yanalitoa katika harakati zake ya kukabiliana na changamoto za maendeleo.

Profesa Lipumba alisema hayo jana katika mahojiano na gazeti hili kuhusiana na kauli ya mfanyabiashara maarufu nchini, Rostam Aziz aliyemtuhumu Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi kuwa ni ‘nyangumi wa ufisadi’.

Alisema malumbano hayo yanawafanya Watanzania wengi kuacha kujadili mambo muhimu ya kimaendeleo na kubaki kwenye fitina zinazosambazwa na wafanyabiashara hao.

Aliitaka serikali ya Rais Jakaya Kikwete kukomesha tabia ya wafanyabiashara kukamiana kupitia vyombo vya habari, kwa lengo la kuwashirikisha wananchi kwenye chuki zao ambazo zinaotesha mbegu za rangi na ukabila, hivyo kutishia amani ya nchi.

“Tanzania ni nchi maskini ingawa tuna rasilimali nyingi. Tumekuwa na tatizo kubwa la kushindwa kujipanga vizuri katika kuzitumia. Kwa jinsi suala hili la ufisadi linavyokwenda, linazidi kutuvuruga,” alisema Lipumba na kufafanua: “Mijadala (malumbano) hii inazidi kututoa kwenye mstari.”

Hata hivyo, alisema katika maelezo ya Rostam, ambaye pia ni Mbunge wa Igunga, kuna hoja nzito alizozitoa na ambazo zimewafumbua macho Watanzania, hivyo Rais Kikwete hana budi kuzishughulikia kikamilifu.

Alitaja miongoni mambo hayo kuwa ni tuhuma kuwa Mengi alikopa mabilioni Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kabla haijabinafsishwa na hakurejesha na vile vile alichukua mabilioni mengine kwenye mfuko unaochangiwa na wahisani; Kuagiza Bidhaa kutoka Nje (CIS) ambazo pia hakuzirudisha serikalini kama ilivyo utaratibu wa mfuko huo.

Aliitaka Wizara ya Fedha na Uchumi kuutangazia umma wote waliokopa NBC na CIS na kuwaamuru walipe na kwamba, wachukuliwe hatua kama ilivyokuwa kwa mafisadi wengine waliochota mabilioni ya fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Profesa Lipumba, alisema kama nyaraka zinazohusu fedha za CIS zitakosekana Hazina, serikali iwasiliane na nchi wahisani wa mfuko huo, kwa sababu wana kumbukumbu za kampuni zote zilizokopa.

Alimtaka Rais Kikwete kuonyesha dhahiri nia yake ya kupambana na ufisadi kwa kutowaonea huruma wafanyabiashara wote wawili ambao kila mmoja anaonekana yuko karibu naye (rais).

Profesa Lipumba alisema anamtambua Rostam kuwa ni Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mengi ni mwanachama wa CCM ambaye amekuwa akijinadi kuwa anamsaidia Rais Kikwete kwenye vita dhidi ya mafisadi; hivyo akasisitiza wote wako karibu na Rais Kikwete.

Alisema fedha za Mfuko wa CIS hutolewa na wahisani ili kuwasaidia wafanyabiashara kuagiza bidhaa nje na hutakiwa kurejeshwa serikalini kwa shughuli nyingine za maendeleo, hivyo kama hazikurudishwa, huo utakuwa ni wizi wa mali ya Watanzania.

Kuhusu EPA, Profesa Lipumba aliendelea kusisitiza kuwa ripoti ya awali ya ukaguzi ilionyesha kampuni ya Kagoda ilighushi nyaraka ili kuzichota hizo fedha, hivyo haoni sababu ya serikali kutowapeleka mahakamani wahusika au wamiliki wake ambao mpaka sasa wanafichwa.


lipumba unataka kikwete amshughulikie mengi je marafiki zako RA, manji(nssf). tanil, jetu et al vipi.

Mengi ameshamaliza hizo kesi zote mahakamani!

Kweli RA payroll yake ni kubwa mpaka Lipumba....![/QUO


Lipumba nina wasiwasi ajenda yake ina ashiria udini.
 
Lipumba .....Lipumba .....Lipumba .....Lipumba .....Lipumbaa.....
gone........... gone........... gone ........... gone......... gooneeee ........kaput !!
 
Kwanini watu wanapenda kutetea ujinga? RA kila mtu anamjua Mengi mtu wa watu mzalendo kila mtu anamjua na nini hawa watu wanafanya, point ni kwamba tunaikubali hali tulionayo ya kukalia maneno tu na kila mtu anajua kuwa hatuwezi kufanya kitu bila ya kusukumwa.But I promise siku inakuja tutabadilika na kujituma.
 
Nimesoma post huku nimebana pumzi, siamini Lipumba kama anakuja na mashambulizi namna hii dhidi ya mtu aliyejitoa mhanga kuwataja mafilisi wa nchi hii!

Sasa naanza kuamini kuwa Lipumba si tu kwamba yupo ktk payroll ya mafilisi bali pia zile kelele zake alizokuwa anapiga dhidi ya mafisadi ni kwamba alijua hakuna hatua zitakazochukuliwa dhidi yao na alikuwa tu anatimiza wajibu ili kupata reputation ya kisiasa. Wanasiasa bwana ni kama upepo vile.

Anyway sasa naamini kuwa CUF si chama makini kama alivyosema Prof. Safari na wanajua wanachokifanya, they just stir in order to survive and who knows, may be wanasiasa wa kulipwa.
lipumba chuki yake ni MENGI kujipendekeza kwa KIKWETE jambo ambalo ni dhahiri...

kwa nini MENGI anajipendekeza kwa KIKWETE?????
 
Maalim Seif kupitia Ismail Jussa amemuingiza Lipumba kwenye shimo la kisiasa. Rostam Aziz aliwaahidi nguvu zake zote kuwezesha CUF kushinda Zanzibar. Kinachoendelea sasa ni nikune nikukune. Tamko la Rostam lina mchango mkubwa wa mmoja wao. Kosa lao ni kuwa hawa-cross check nyaraka walizopewa kupata latest information. Matokeo yake wamemwachia Mengi mahali pa kuibukia. Hata kwenye uchaguzi wa Busanda, sehemu kubwa ya fedha za CUF zimetoka kwa Rostamu Aziz na mtu mmoja kati ya wale mapapa wanne waliobaki. Pindi nikipata taarifa kamili nitawaletea

PM
 
Wakuu kwa hakika msimamo wa Prof.Lipumba katika sakata hili la kuwaumbua mafisadi wanaoitesa nchi umenishangaza sana.
Pamoja na ukweli kuwa ufisadi upo na unaonewa haya katika sehemu fulani fulani za jamii, lakini msimamo wa huyu msomi, Proffessor wa Uchumi na anayeheshimika kwa misimamo juu ya uchumi ,hakika unashangaza.
Pesa zilizopotea katika sakata lote , iwe EPA,BOT,KAGODA,CIS au RICHMOND na wizi mwingine mwingi wa fedha za serikali zinafikia matrillioni.
Msimamo wake unaelekea kuegemea kuwatetea wezi wa fedha nyingi ambao by coincidence ni wahindi kwa wingi wao.
Je Prof anaukaribu gani na Rostam? au kwa vile wanatoka wote Tabora?
Nini kimempofusha huyu msomi?
 
kela72,

..mara ya mwisho nilisikia Prof ameoa mwanamke toka lile kabila linalochukiwa kabisa hapa jamii forums.

..pia mwanamke huyo ni alikuwa muumini wa dini inayochukiwa na chama cha CUF.

Pole mkuu limekuletea matatizo hili lakini usife moyo, ulichosema ni ukweli mtupu ila kawaida ya binadamu wanapenda kufichaficha mambo. Ulichokisema kila mtu anacho rohoni lakini ni mwiko kukisema waziwazi!!
Mfano, mniwie radhi lakini.... "Rashidi Mfaume Kawawa alikuwa ndiye waziri mkuu mfupi kuliko mawaziri wakuu wote waliopita katika katika nchi yetu" kweli haipendezi kumtambulisha mtu kwa sifa hii, lakini ni kweli mheshimiwa alikuwa mfupi.
Hivyo Joka Mkuu, kuna gharama za kuongea ukweli, na kwako ndiyo hayo mashambulizi uliyoyapata.
 
Wakuu kwa hakika msimamo wa Prof.Lipumba katika sakata hili la kuwaumbua mafisadi wanaoitesa nchi umenishangaza sana.
Pamoja na ukweli kuwa ufisadi upo na unaonewa haya katika sehemu fulani fulani za jamii, lakini msimamo wa huyu msomi, Proffessor wa Uchumi na anayeheshimika kwa misimamo juu ya uchumi ,hakika unashangaza.
Pesa zilizopotea katika sakata lote , iwe EPA,BOT,KAGODA,CIS au RICHMOND na wizi mwingine mwingi wa fedha za serikali zinafikia matrillioni.
Msimamo wake unaelekea kuegemea kuwatetea wezi wa fedha nyingi ambao by coincidence ni wahindi kwa wingi wao.
Je Prof anaukaribu gani na Rostam? au kwa vile wanatoka wote Tabora?
Nini kimempofusha huyu msomi?

Yumo ndani ya Pay Roll ya Rostam Aziz.
Hivi wewe ukiambiwa Rostam ameajiri waTanzania 6000 na anawalipa vizuri unadhani ni Wakwere wachovu wa kule Bgagamoyo???

Ni Wanasiasa, Polisi ,Majaji na viongozi wa vyombo vya serikali.


Unaweza kuwa kwenye Pay Roll kwa muda mrefu sana ukaendelea kula fedha ukidhani ni bure.
Siku ikifika unaambiwa haya bwana zamu yako ya kulipa wema wetu ndo hii.
Mkandie Mengi.
Kwa vile mkataba wenyewe ni wa KIMAFIA inabidi upande jukwaani na kuanza kubwabwaja Pumba.

Unalo?? Inabidi Usomi wako wote uuweke pembeni uikwae elimu halisi Upewa na Bwana wako Rostam Aziz.

Wengi wako kweny Pay Roll.

Tulidai Uhuru kutoka kwa Waingereza tukapa, sasa Uhuru wetu umepokonywa na Makaburu wa Kiarabu na Kihindi, sawa kabisa na ilivyokuwa South Afrika.
Makaburu wa South Afrika waliowakalia weusi walio wengi kwa miaka kibao walikuwa ni Raia wazawa wa South Afrika lakini wenye rangi nyeupe, walitumia uraia wao na rangi yao kuwanyanyasa na kuwadharirisha weusi.
Rostam na Timu yake yote ni Watanzania wa kuzaliwa lakini walio Makaburu kwa asili.
Hawa weusi kama sisi wapigao viukelele kuwaunga mkono ni Vibaraka kama walivyokuwa vibaraka wengi weusi huko Afrika ya kusini.

hii PayRoll ya Rostam muda usipofupishwa itawamaliza hata waliomashujaa wa vita.
 
lipumba chuki yake ni MENGI kujipendekeza kwa KIKWETE jambo ambalo ni dhahiri...

kwa nini MENGI anajipendekeza kwa KIKWETE?????


kikulacho ki nguoni mwako hiyo ndio story apa... Mengi anajipendekeza kwa Kikwete kwa kuwa anataka kuficha uozo wake na ndio maana anajidai kutoa toa vimisaada saada kwa watu kadhaa ili aonekane mwema ila akae akijua mtu mwenye akili lazima amuone kuwa yeye ni Mwizi tu.. ila kwa mwenye akili kama zake ataona kuwa ni mwema...

Ninachoamini ni kuwa Mengi ni FISADI na ndio maana anajipendekeza kwa kikwete..hii staili ya kujipendekeza haijaanza leo na mara nyingi huwa successful
 
hivi mnamkumbuka lipumba huyu huyu alitetea kwa mishipa yote ya shingo kuhusu unuliwaji wa DOWANS? watu tulitaka itaifishwe yeye alitaka inunuliwe, je alikuwa na maslahi ktk deal ile?
 
kutoka mwananchi


malumbano hayo yanawafanya Watanzania wengi kuacha kujadili mambo muhimu ya kimaendeleo na kubaki kwenye fitina zinazosambazwa na wafanyabiashara hao.

Aliitaka serikali ya Rais Jakaya Kikwete kukomesha tabia ya wafanyabiashara kukamiana kupitia vyombo vya habari, kwa lengo la kuwashirikisha wananchi kwenye chuki zao ambazo zinaotesha mbegu za rangi na ukabila, hivyo kutishia amani ya nchi.

“Tanzania ni nchi maskini ingawa tuna rasilimali nyingi. Tumekuwa na tatizo kubwa la kushindwa kujipanga vizuri katika kuzitumia. Kwa jinsi suala hili la ufisadi linavyokwenda, linazidi kutuvuruga,” alisema Lipumba na kufafanua: “Mijadala (malumbano) hii inazidi kututoa kwenye mstari.”

Prof, do not patronize us.
 
hivi mnamkumbuka lipumba huyu huyu alitetea kwa mishipa yote ya shingo kuhusu unuliwaji wa DOWANS? watu tulitaka itaifishwe yeye alitaka inunuliwe, je alikuwa na maslahi ktk deal ile?


Unajua haya majina yanakuwa na maana, Li-pumba...lazima atajaa pumba tu.
 
Mengi anajipendekeza kwa Kikwete kwa kuwa anataka kuficha uozo wake na ndio maana anajidai kutoa toa vimisaada saada kwa watu kadhaa ili aonekane mwema ila akae akijua mtu mwenye akili lazima amuone kuwa yeye ni Mwizi tu.. ila kwa mwenye akili kama zake ataona kuwa ni mwema...
Ninachoamini ni kuwa Mengi ni FISADI na ndio maana anajipendekeza kwa kikwete..hii staili ya kujipendekeza haijaanza leo na mara nyingi huwa successful[/QUOTE]

Mkuu mbona unakosa analysis ya mambo na kuishia na rhetoric?
Kwa hiyo Mengi amejikomba kwa MH Ali Hassan Mwinyi, Mh. Mkapa na sasa JK au siyo? bila kujulikana nia yake?
Utasema nini kwa wale wanaojikomba kwa mafisadi, watu kama Makamba, Sofia Simba, Mkuchika Prof Lipumba n.k
Jaribu kuwa analytical mzee!
 
It test so bitter to find that even an educated politician can foolishly handle matters of national interests just for his own interests, as for this Lipumba I dont get how did you become a professor, a professor with non executing head. I can notice something, it seems Lipumba and Mengi are rivals, why you only look Mengi's weaknesses?? Forget your differences Lipumba, be patriotic! You seem to be on the side of Rostam and his fellows despite the bad accusations they have not only from Mengi but from many patriotic leaders and journalists, it seems you have common interests with RA team....., See now Mengi has already defended himself with proof of Rostam lies, shy............!!!!! Oh my God....., Lipumba open your eyes!!! see.., are you not from the same poor society protected by Mengi???

Imenibidi niseme.....,
Mchumia juani
Kijijini
 
Back
Top Bottom