Prof Lipumba alishawahi kupata elective post hapa nchini?

Lipumba ni moja kati ya watu makini! Hana tamaa ya madaraka kama ilivyo kwa baadhi ya viongozi wa kisiasa hapa nchini. Vilevile anaheshimika si Africa tu bali Duniani kwa ujumla! Taaluma ya uchumi aliyonayo imetumika kuimarisha hali za kiuchumi katika baadhi ya Mataifa duniani.

Tatizo letu sisi watanzania ni ushabiki/unazi,hatuwezi kabisa kupima uwezo wa mtu na kumpa heshima anayostahili. Na ushabiki/unazi huu utatufanya tuendelee kuwa duni hadi kiama!
Kama hana tamaa ya madaraka na ni mtu aliyebobea kwenye taaluma ya Uchumi,kwenye siasa anafanya nini? Mchumi asiye na tamaa ya madaraka kwa nini asiishi kwa taaluma yake badala ya kujidhalilisha kwa kupambana na madongo ya kisiasa ambayo katika kuyakabili wakati mwingine anafanya usomi wake uwe questionable?
 
Mkuu, ushabiki pembeni,tuwe objective tuu, jaribu kupata resume ya huyu jamaa. Ni mtaalamu wa ukweli. Angeweza kuwa mbunge wa jimbo lolote lile na angeweza kuwa waziri wa wizara yeyote ile...He is by far better than viongozi wengi sana wa kuchaguliwa nchini(actually than viongozi wote wa CCM). Ameonesha uwezo mkubwa tu wa kuongoza. Chama alichopo na anachokiongoza ndio tatizo lake la msingi. Hana watu wa kumfanania hata kidogo. "wanamnyonya" tu uwezo wake na hataishia mahali pazuri nna uhakika!
Hata uenyekiti wa kitongoji hawazi shinda angalia kura za kikwete 2005 kule kwao ilolangulu kikwete alipata kura 4500, lipumba 345, mbowe 200, hiyo inaonesha kabisa hata mama zake hawakumpigia kura , anategemea kura from Zanzibar je yeye ni mzanzibar?hana chochote cha kujivunia nchi hii amekuwa mshauri wa rais mwinyi uchumi ulifika wapi? hatujawahi kusikia mtu aliyekuwa mshauri wa uchumi wa mkapa akijigamba hadharani ambaye ndiyo alifanya kazi nzuri ambayo kila mmoja aliuona
Labda unajua marais wote waislam tanzania ni tatizo, kama watanzania tungelogwa tukampa hii nchi Lipumba leo uchumi ungekuwa worse kuliko tunavyoweza fikiria , ni mchumi asiyejua uchumi , ni kama dowans kampuni ya kufua umeme ambayo haifui umeme
 
kutokugombea ubunge kwa profesa kunaonyesha jinsi asivyo natamaa za madaraka kama alivyo mbowe wa chadema!! Profesa ameridhika na kazi aliyonayo ya uenyekiti wa cuf na anauwezo wa kuteuliwa ubunge kupitia kapu lao maalum lakini hajawahi kufanya hivyo!
Huyu ndio kiongozi na anafaa kuigwa na wengine! Wala hakuna ulazima wa kuwa mbunge kama unavyoelekeza!
basi anamatatizo kama yupo kwa ajili ya kuimalisha chama tuu wenyekiti wengine wapo bise na mambo mengi na yeye ni mwenyekiti tuu mbona cuf inalegalega!!
 
basi anamatatizo kama yupo kwa ajili ya kuimalisha chama tuu wenyekiti wengine wapo bise na mambo mengi na yeye ni mwenyekiti tuu mbona cuf inalegalega!!

Angalizo hapo kwenye red Mkuu: Wenye chama chao hawakubaliani na hilo -- kulegalega kwa chama -- na kama lipo basi ni kutokana na kampeni za maaskofu!
 
Pia nafahamu fika kwamba Profesa ni mgombea urais wa kudumu mzuri hapa nchini...
-----------------------------------------------------------------------------------------------------
Nitaandaa tuzo za mgombea uraisi
mara nyingi zaidi.
1.Lipumba - 1995, 2000,2005,2010.
2.Mrema -
1995,2000,2005.
3..............-
 
WanaJF Nauliza: Hivi Kiongozi Mkuu (Mwenyekiti) wa CUF alishawahi kupata position ya kuchaguliwa (elective post) kitaifa? Alishawahi, kwa mfano, kuchaguliwa kuwa Mbunge? Sikumbuki sawasawa.

Nasema hivi kwa sababu katika vyama karibu vyote vikuu vya kisiasa sasa hivi -- yaani CCM, Chadema, TLP, NCCR, UDP viongozi wake wakuu (wenyeviti) ama ni wabunge sasa hivi au walishawahi kuwa wabunge huko nyuma.

Inakuaje kwa CUF si hivyo? Nauliza tu na ninafahamu fika kwamba siyo lazima mwenyekiti wa chama cha siasa awe Mbunge. Pia nafahamu fika kwamba Profesa ni mgombea urais wa kudumu mzuri hapa nchini, lakini rekodi inaonyesha hajawahi kabisa kuchaguliwa kwa nafasi yoyote kwa njia ya kura, ukiacha kugombea kwake katika chaguzi za ndani ya chama chake. Jee inawezekana akastaafu siasa bila ya kupata elective post yopyote?

Nawasilisha.

Prof. Lipumba ameshawahi kuchaguliwa na kuwa kiongozi. Alishindana na Prof A. Safari katika cheo cha Uenyekiti wa Taifa wa CUF na kushinda kwa asilimia zaidi ya 98%. Aaaaaaaaaaaaaaaahhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh !!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Lipumba ni moja kati ya watu makini! Hana tamaa ya madaraka kama ilivyo kwa baadhi ya viongozi wa kisiasa hapa nchini. Vilevile anaheshimika si Africa tu bali Duniani kwa ujumla! Taaluma ya uchumi aliyonayo imetumika kuimarisha hali za kiuchumi katika baadhi ya Mataifa duniani.

Tatizo letu sisi watanzania ni ushabiki/unazi,hatuwezi kabisa kupima uwezo wa mtu na kumpa heshima anayostahili. Na ushabiki/unazi huu utatufanya tuendelee kuwa duni hadi kiama!

Waache hao waongee watakavyo kwa milengo yao iliyofungamana na itikadi, imani na baguzi kila kona. Kwangu LIPUMBA ni miongoni mwa wanasiasa wazalendo wa Ukweli. Siasa zake zinajiweka huru na itikadi na imani. Ninampenda zaidi LIPUMBA anapokuwa anahojiwa na wanahabari makini kama Hamisi Damu Mbaya-MLIMANI TV au EZEKIEL-MwanaHalisi na akatakiwa kutoa maoni yake juu ya mustakabali wa nchi, ku-rank ya wanasiasa wenziwe na mtazamo wake kwenye matamko toka kwa viongozi wa Jamii na Dini. Lipumba hana U-CHAMA, U-Kajanja wala U-DINI. Daima yuko kwenye mizania ya UKWELI na UHALISIA.
 
Prof. Lipumba ameshawahi kuchaguliwa na kuwa kiongozi. Alishindana na Prof A. Safari katika cheo cha Uenyekiti wa Taifa wa CUF na kushinda kwa asilimia zaidi ya 98%. Aaaaaaaaaaaaaaaahhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh !!!!!!!!!!!!!!!!!


Acha kukurupuka. Soma tena thread yangu. Sisemei uchaguzi wa ndani ya chama, bali wa nje kwa wananchi kwa ujumla wake.
 
Back
Top Bottom