NGENDA NGOLOMA
Member
- Feb 18, 2012
- 23
- 10
Najitokeza kwa mara ya kwanza kumuomba na kumshauri mwenyekiti CUF Taifa mheshimiwa Profesa Lipumba kuachana na siasa ili kutenga muda wa kutosha na kulitumikia taifa kwa Uzalendo na umahiri mkubwa. Binafsi namheshimu sana na kumkubali msomi huyu. CV ya huyu jamaa imesheheni vilivyo na haitiliwi mashaka na ulimwengu ndiyo maana alikuwa anaongoza jopo la wasomi na wachumi Duniani. Kuachia ngazi kwa prof Lipumba kuna maana kubwa na kutawapa fursa kwa watanzania wote bila kujali itikadi zao za vyama kumpa ushirikiano wa kutosha. Tafadhali mheshimiwa Prof. Lipumba zingatia ushauri wangu kwa ajili ya mstakabali wa taifa letu