Kama jk anataka kweli kuondoa fitina na kulitakia mema taifa hili-basi watu hawa wawili wanafaa kabisa kwa vyovyote na kwa maslahi ya umma kuongoza tume ya katiba mpya.
1. Prof issa shivji amekuwa katika mchakato wa kudai katiba mpya kabla na baada ya mfumo wa vyama vingi. Sio mnafiki, hanunuliki kama wasomi wetu wengi -anayetaka ukweli asome raia mwema la wiki ya jana atapata ukweli huu kutoka katika makala yake. Hayumbishwi. Nampendekeza awe mwenyekiti wa tume hiyo
2. Dr w. P. Slaa ni mtanzania mwenye msimamo aliyesababisha chachu ya katiba mpya, kama ilivyo kwa shivji slaa(phd) hanunuliki na hayumbishwi. Ni mtanzania aliyekuwa anagombea urais agenda yake kubwa ya kwanza ikiwa ni kuanzisha mchakato wa katiba mpya. Ni mtanzania anayeona mbali na anayeitakia mema nchi hii, mwenye kuchukizwa na umaskini, ufisadi, ujinga, na maradhi ya nchi. Huyu anafaa kuwa katibu wa tume hii -aombwe ashiriki hatakama yeye mwenyewe hakubaliani na approach ya serikali ya jk. Lakini kwa jk kumuomba na kumtumia katika tume hii wote wawili watakuwa wameweka historia ya aina yake kwa maslahi ya umma.
Tunao watanzania wengine kama jaji kisanga,ulimwengu, ayoub lioba, amiri maneto, bomani -hawa wanaweza kutumika kama wajumbe pamoja na mama nkya, ila hoja kubwa ni kutaka watanzania wazalendo wa kweli -nilisikitishwa na tume ya bomani ya madini ambayo mpaka leo bado wizi wa madini unaendelea -ndio maana slaa(phd) hataki tume hizi kwa kuwa zinakuwa hazipo huru.
Haya ni maoni yangu na ninaamini wapo wana jf watakubaliana na mimi kwa kupitia reference ya tume zilizowahi kuundwa huko nyuma na matunda yake.
1. Prof issa shivji amekuwa katika mchakato wa kudai katiba mpya kabla na baada ya mfumo wa vyama vingi. Sio mnafiki, hanunuliki kama wasomi wetu wengi -anayetaka ukweli asome raia mwema la wiki ya jana atapata ukweli huu kutoka katika makala yake. Hayumbishwi. Nampendekeza awe mwenyekiti wa tume hiyo
2. Dr w. P. Slaa ni mtanzania mwenye msimamo aliyesababisha chachu ya katiba mpya, kama ilivyo kwa shivji slaa(phd) hanunuliki na hayumbishwi. Ni mtanzania aliyekuwa anagombea urais agenda yake kubwa ya kwanza ikiwa ni kuanzisha mchakato wa katiba mpya. Ni mtanzania anayeona mbali na anayeitakia mema nchi hii, mwenye kuchukizwa na umaskini, ufisadi, ujinga, na maradhi ya nchi. Huyu anafaa kuwa katibu wa tume hii -aombwe ashiriki hatakama yeye mwenyewe hakubaliani na approach ya serikali ya jk. Lakini kwa jk kumuomba na kumtumia katika tume hii wote wawili watakuwa wameweka historia ya aina yake kwa maslahi ya umma.
Tunao watanzania wengine kama jaji kisanga,ulimwengu, ayoub lioba, amiri maneto, bomani -hawa wanaweza kutumika kama wajumbe pamoja na mama nkya, ila hoja kubwa ni kutaka watanzania wazalendo wa kweli -nilisikitishwa na tume ya bomani ya madini ambayo mpaka leo bado wizi wa madini unaendelea -ndio maana slaa(phd) hataki tume hizi kwa kuwa zinakuwa hazipo huru.
Haya ni maoni yangu na ninaamini wapo wana jf watakubaliana na mimi kwa kupitia reference ya tume zilizowahi kuundwa huko nyuma na matunda yake.