Wajameni kunani CUF mbona Prof. Lipumba yu kimya namna hii kipindi hiki muhimu? au ndo katika ule mgomo baridi nathani mambo yameiva ndani ya CUF mshindo mkuu unakuja! ile dhana ya kwamba CUF ni Maalim na Maalim ni CUF itakizamisha CUF tega sikio!
hata MTATIRO MBONA KIMYA WAPI KINA JUSA
Yupo USA anakula bata na kina Obama na kuendeleza siasa za kimagharibi.
Ni bora akae huko huko mana ni mtu gani asiyekubalika kwao, kwao Tabora hakubaliki hata kidogo hata akigombea uenyekiti wa mtaa hapati. Angalia wenzake wote wenyeviti wa vyama wanavyokubarika kwao, Kikwete, Chalinze anakubalika na alishawahi kuwa mbunge, John Cheyo,kwao Bariadi anakubalika na mpaka leo mbunge, Mbowe kwao Hai, anakubalika hadi leo mbunge, Dr slaa kwao Karatu anakubalika na alikuwa Mbunge, Mrema kwao anakubalika Vunjo na leo hii Mbunge. Sasa huyu Lipumba ana matatizo.
Duuh! kwahiyo mkuu ndiyo kusema CUF kwishiney kabisa? Nafikiri wakimsamehe Hamadi Rashidi na wenzie....cuf inaweza fufukaHivi kaka unategemea lolote jipya kutoka CUF? Wenzio wako kwenye mahaba mazito na CCM wewe unataka kuingilia mambo ya watu. Upinzani wa kweli hautakaa utoke CUF hii ya sasa; labda wajipange upya tena wajipange haswa.
Walivyokuwa wanakaa kwenye vikao vyao vya miafaka kwa kificho wenye akili zao walionya na kupiga kelele, CUF wakaona wanaonewa gere kumbe ndio hivyo chama kilikuwa kinaelekea kaburini kwa faida ya wachache. Inahuzinisha lakini hakuna neno jingine zaidi ya R.I.P. CUF.
Duuh! kwahiyo mkuu ndiyo kusema CUF kwishiney kabisa? Nafikiri wakimsamehe Hamadi Rashidi na wenzie....cuf inaweza fufuka
Bado yupo hai na anaendelea na majukumu ya kibunge....ila ki ukweli HR atawasumbueni kweliKwani huyu Hamad Rashid bado yupo hai!!
unahamu ya kujiunga na CUF nini ???? Mbowe ameshindwa anaatafuta msaada wa Lipumba?????
Bado yupo hai na anaendelea na majukumu ya kibunge....ila ki ukweli HR atawasumbueni kweli
Atawasumbuweni nyinyi Watanganyika tu sisi huku hata hatumjadili habari yake imekwisha na sasa tuna deal na mambo mengine ikiwemo kujipanga kwa kutoa maoni katika katiba mpya. Pia Hamad Rashid hajakatazwa kuendelea na shughuli zake za Bunge ila kwa sasa sio mwanachama wa CUF tena, hata ukimuona mtu yuko hivyo jua ana matatizo; mtu akisha kupewa talaka na mume hurejea kwao lakini sisi tunashangaa kwanini amefika hadi mahakamani anang'ang'ania ili arejewe!
Mpemba mbishi, NYIe ndo wale mnaoamini eti kwa kuwa Mbili mara Mbili na Mbili jumlisha Mbili zote jibu lake nne, mnalazimisha na nne mara nne na nne jumlisha nne majibu yake lazima yafanane.....imekula kwenu. Acheni kuabudu watu NINYI.
hiyo cuf hamad keshasema kioo kikiingia vumbi hupanguswa ila kikipasuka kutolewa na kuwa replaced.......nami nasema hvii taka usitake CUF ishapasuka hvyo subirini REPLACEMENT YAKE NA ANAYO HAMAD NA TIMU YAKE......
Ndugu yangu hassan nakuomba sana usihame hapa JF ipo siku tena haipo mbali utajua kama kweli Wapemba nuksi, na utakuja kuthibitisha mwenyewe ya kwamba kumbe Wapemba (Wazanzibari) wakiamua lao liwe lazima linakua kwa Uwezo wa Mungu. Hamad Rashid ataumbuka vibaya sana! Zanzibar Daimaaa Mbeleeee. Am proud to be Zanzibari