Nimekua nikijiuliza kuhusu mwenyekiti wa chama cha wananchi (CUF) Prof. Ibrahim Lipumba na tabia yake ya kuwakacha watanzania wakati wa matatizo kama haya tuliyonayo sasa na badala yake kujitokeza wakati wa uchaguzi mkuu tu; na kujifanya ana uchungu sana wa kuwakomboa watanzania kutokana na matatizo yanayowakabili.
Kila wakati uchaguzi unapokaribia tumekuwa tukishuhudia kujitokeza hadharani kwa Prof. huyu mahiri wa uchumi huku akiyasemea matatizo ya watanzani na kuahidi kuyatatua endapo angechaguliwa kuiongoza nchi. Lakini baada ya uchaguzi, huwa hatumsikii kiongozi huyu hadi uchaguzi mwingine unapokaribia.
Nilitarajia kumsikia na kumuona mwanasiasa huyu akiyasemea matatizo ya watanzania. Tunayo matatizo mengi sana ikiwa ni pamoja na kupanda kwa kasi kwa gharama za maisha na kuundwa kwa katiba mpya nchini.
Nilitarajia kumuona Prof. Lipumba kama mwanasiasa na mchumi mwandamizi akitoa mchango wake mkubwa katika maeneo hayo, lakini amekuwa kimya tangu uchaguzi mkuu ulipoisha.
Je ndio kusema kwamba Prof. Lipumba amewasusa watanzania kwa sababu nao walimtosa kwenye uchaguzi mkuu uliopita?
Au mchumi huyu ni mwanasiasa wa kipindi cha uchaguzi tu!?
Kila wakati uchaguzi unapokaribia tumekuwa tukishuhudia kujitokeza hadharani kwa Prof. huyu mahiri wa uchumi huku akiyasemea matatizo ya watanzani na kuahidi kuyatatua endapo angechaguliwa kuiongoza nchi. Lakini baada ya uchaguzi, huwa hatumsikii kiongozi huyu hadi uchaguzi mwingine unapokaribia.
Nilitarajia kumsikia na kumuona mwanasiasa huyu akiyasemea matatizo ya watanzania. Tunayo matatizo mengi sana ikiwa ni pamoja na kupanda kwa kasi kwa gharama za maisha na kuundwa kwa katiba mpya nchini.
Nilitarajia kumuona Prof. Lipumba kama mwanasiasa na mchumi mwandamizi akitoa mchango wake mkubwa katika maeneo hayo, lakini amekuwa kimya tangu uchaguzi mkuu ulipoisha.
Je ndio kusema kwamba Prof. Lipumba amewasusa watanzania kwa sababu nao walimtosa kwenye uchaguzi mkuu uliopita?
Au mchumi huyu ni mwanasiasa wa kipindi cha uchaguzi tu!?