nguvumali
JF-Expert Member
- Sep 3, 2009
- 4,923
- 1,325
mchuano mkali ulionekana kwenye siasa za Jimbo la Rugwe Mashariki baina ya Prof DAVID Mwakyusa dhidi na Nd. Richard Kasesela, ambapo baada ya chakachua ya hapa na pale , Prof.Mwakyusa akaibuka na ushindi mwembamba ambapo nd.Kasesela hakuridhika na chakachua ile , akaamua kukata rufaa kwenye Kamati kuu ya CCM, ambapo hata hivyo Mwakyusa akapenya na kutangazwa mshindi.
katika hali inayoonyesha kumpooza adui yake (kisiasa) leo kupitia vyombo vya habari , amemteua ndugu Kasesela kuwa Mmoja kati ya wajumbe wa bodi ya Taasisi ya Mifupa MUHIMBILI, MOI, KUANZIA tarehe 10 Agosti,2010.
uteuzi huo umefanyika chini ya sheria ya MOI ya mwaka 1996, kifungu cha 5.
Je kwa kupoozana huko Mwakyusa atakua amevunja mpasuko wa kisiasa jimboni kwake, ambako kwa ccm , Kasesela ananguvu zaidi.
katika hali inayoonyesha kumpooza adui yake (kisiasa) leo kupitia vyombo vya habari , amemteua ndugu Kasesela kuwa Mmoja kati ya wajumbe wa bodi ya Taasisi ya Mifupa MUHIMBILI, MOI, KUANZIA tarehe 10 Agosti,2010.
uteuzi huo umefanyika chini ya sheria ya MOI ya mwaka 1996, kifungu cha 5.
Je kwa kupoozana huko Mwakyusa atakua amevunja mpasuko wa kisiasa jimboni kwake, ambako kwa ccm , Kasesela ananguvu zaidi.