Fasta Fasta, Prof atashinda hii kesi kwa haki!. Property Tax kwa nchi za wenzetu iko juu sana hivyo ukiuza nyumba unaweka bei mbili, ya chini ambayo ndio iko kwenye risiti na kulipiwa kodi za serikali, na bei halisi kwa mwenye nyumba. Mkataba halali ni ule wa bei ya chini ya serikali. Serikali inajua kila kitu na kila hatua!.
Bomu lilipo lipuka, mwenyenyumba inambidi lazima aruke malipo ya pili maana ikijulikana ni jela!. Ndio maana mnunuzi kagoma katakata kuja kutoa ushahidi!.
Kwa vile kwa sheria yetu ushahidi wa video sio permisable, Prof. Mahalu ataachiwa kwa kukosekana ushahidi, ila hii kesi ni muendelezo wa kesi za visasi za mkuu wetu. Yeye akiwa MFA kuna mahali walipitiana na Mahalu, kwa vile Mahalu alikuwa ni best na Mkapa, baadhi ya mambo yalipitishwa juu kwa juu na kumbypass yeye, hivyo sasa ndio anakomoa!.
Inawezekana wewe ndiyo umetoa ufafanuzi mzuri.