afrodenzi
Platinum Member
- Nov 1, 2010
- 18,145
- 9,207
Hongera zikufikie, kimwali kumtwaa
Wambea msiwasikie, nyumba na mitaa
Karaha msizishike, msingenyo kukataa
Hongera zikufiee, kimwali kumtwaa...
Kwa mbali msikike, mkipeta na ku ng'aa
Pamoja mshikike, kwa dhiki na rahaa
Wawili muhangaike, kulea na kuzaa
Hongera zikufike, kimwali kumtwaa..
Kazi zisikuzidie, nyumbani ukakaa
Kwa wema umsikie, usiwe ka kichaa
Ndugu muhudhurie, mfikapo mkaa
hongera zikufikie, kimwali kumtwaa
Wana JF tunapaa, na la kheri tunawapa
Msiwe kama mkaa, kutumiwa na kuchakaa
Pamoja mnang'aa, na sifaa mwazitwaa
Hongeara zikufike, kimwali kumtwaa..
Wambea msiwasikie, nyumba na mitaa
Karaha msizishike, msingenyo kukataa
Hongera zikufiee, kimwali kumtwaa...
Kwa mbali msikike, mkipeta na ku ng'aa
Pamoja mshikike, kwa dhiki na rahaa
Wawili muhangaike, kulea na kuzaa
Hongera zikufike, kimwali kumtwaa..
Kazi zisikuzidie, nyumbani ukakaa
Kwa wema umsikie, usiwe ka kichaa
Ndugu muhudhurie, mfikapo mkaa
hongera zikufikie, kimwali kumtwaa
Wana JF tunapaa, na la kheri tunawapa
Msiwe kama mkaa, kutumiwa na kuchakaa
Pamoja mnang'aa, na sifaa mwazitwaa
Hongeara zikufike, kimwali kumtwaa..