Press Release: Taarifa ya Maendeleo ya Kuchangia Wahanga Wa Mafuriko

Jul 14, 2008
1,820
1,031
Taarifa ya Maendeleo ya Kuchangia Wahanga Wa Mafuriko.



Mtandao Wa Wanataaluma Tanzania (TPN) Kwa kushirikiana na www.issamichuzi.blogspot.com na www.jamiiforums.com na kampuni ya Push Mobile ambayo inatuunganisha na mitandao ya simu ya ZAIN; TIGO na VODACOM imekuwa ikiendesha kampeni ya kusaidia wahanga wa mafuriko yaliyoikumba Tanzania ambayo ilizinduliwa tangu tarehe 12-01-2010 kwa ajili ya familia zaidi ya 8,000 zilizoathirika kwa kukosa makazi, vyakula, na huduma za afya na kupoteza mali nyingi. Misaasa yote itakayopatikana inapelekwa Chama cha Msalaba na Mwezi Mwekundu cha Tanzania ambao wako mstari wa mbele katika kuwasaidia wahanga. Awamu ya kwanza ilikwisha wakilishwa.

TPN na wadau wake inaendelea kuratibu harambee ya kuchangia wahanga wa mafuriko haya kwa kukusanya misaada ya vitu mbalimbali na pesa kwenda kwenye ofisi za Chama cha Msalaba na Mwezi Mwekundu cha Tanzania ambacho kiko mstari wa mbele kuongoza juhudi za kusaidia walioathirika ikishirikiana na taasisi mbalimbali binafsi na vyombo vya serikali. Michango inayopokelewa ni pamoja na fedha na Magodoro, Mahema, Vyandarua, Vyakula (visivyoharibika), Maji safi (masanduku ya chupa za maji), Madawa ya kuzuia maambukizi (ambayo hayajaharibika au kufunguliwa), Vifaa kwa ajili ya matumizi ya kina mama na watoto, Makaratasi ya kujipangusia (clean wipes), nguo, vyakula n.k.

TPN inapenda kuwahakikishia Wanachama na wadau wote waliofanya mawasiliano nasi kuwa TPN haijihusishi na kampeni yoyote mpya zaidi ya ile ya mwanzo iliyoiratibu na wadau wake na inazidi kutoa wito kuwa wote wanaopenda kuchangia wanaweza kufanya hivyo kupitia makato ya kila siku ya muda wa maongezi wa simu za mkononi (Tigo; Zain na Vodacom) kwa Kuchangia Shs 150 kwa siku kwa muda wa siku 30 kwa kutuma SMS yenye neno TPN kwenda 15522. Awali utakatwa Shs 250 kama ada ya kujisajili (Makato yote yanahusisha kodi na gharama za kuunganishwa). Kwa maelezo zaidi wasiliana na 0715 740 047”

TPN na Wadau wake ilikabidhi awamu ya kwanza ya misaada kwa Chama cha Msalaba na Mwezi Mwekundu cha Tanzania iliyokusanywa (haihusishi michango ya SMS) ikiwa ni pamoja na Ndoo za Plastic; Maji; Magodoro; Magodoro; Sembe; Chumvi; Mafuta ya kupikia; Miswaki na dawa za miswaki;Sabuni; Majani ya Chai; Mablanketi na Vyandarua vyote vikiwa na thamani ya TZS 1,381,000. Pia tulikabidhi pesa taslimu TZS 1,068,364.80. Tunawashukuru wote waliotoa. Misaada inayoendelea kukusanywa itakabidhiwa katika awamu ya pili siku ya Ijumaa tarehe 29-01-2010.

Misaada pia inaendelea kupokelewa katika makao makuu ya Chama cha Msalaba na Mwezi Mwekundu cha Tanzania Jijini Dar-es-Salaam Masaki na ofisi zake zote Tanzania. Unaweza pia kuchangia vitu mbalimbali kwa kuvilet ofisi za TPN zilizopo Barabara ya Nyerere; Jengo la TOHS (Dar Group); Ghorofa ya 1 karibu na Radio Tanzania au piga simu namba: 0715 740 047 ili ofisa wa TPN avifuate (utalipia usafiri). Hakuna msaada mdogo au usio na maana na misaada yote itapokelewa.

Pamoja Tunaweza!

Imetolewa na:

Mtandao Wa Wanataaluma Tanzania
(Tanzania Professionals Network)
25-Januari-2010
 
mtatangaza lini majimbo yenu mnayogombea?????

manake bongo ukiona misele kama hii, ujue siasa is around the corner! lakini hongereni wazee manake sio siri, mmeula wa nguvu!
 
mtatangaza lini majimbo yenu mnayogombea?????

manake bongo ukiona misele kama hii, ujue siasa is around the corner! lakini hongereni wazee manake sio siri, mmeula wa nguvu!

Mzalendo Akili Kichwani;

TPN katika hili halina mlengo wowote wa kisiasa. Binafsi pia sina malengo yoyote ya kisiasa.

Hizi ni juhudi za TPN, Wadau wake na Wazalendo wote wenye mapenzi mema na nchi yetu na ndugu zetu waliopatwa na hili janga.

Pamoja tunaweza!
 
mtatangaza lini majimbo yenu mnayogombea?????

manake bongo ukiona misele kama hii, ujue siasa is around the corner! lakini hongereni wazee manake sio siri, mmeula wa nguvu!

unashauri tusitishe hii kampeni ya kusaidia wahanga hadi uchaguzi upite ili ujue kuwa wengine hatuna hamu, njozi, au mipango ya kugombea nafasi yoyote ya kisiasa?
 
Mzalendo Akili Kichwani;

TPN katika hili halina mlengo wowote wa kisiasa. Binafsi pia sina malengo yoyote ya kisiasa.

Hizi ni juhudi za TPN, Wadau wake na Wazalendo wote wenye mapenzi mema na nchi yetu na ndugu zetu waliopatwa na hili janga.

Pamoja tunaweza!

Mkuu Mtsimbe,

Ukiona mtu anaanza kufanya swali la hesabu bila kuweka kwanza data chini (nzuri zaidi kwenye Engineering) basi huyu lazima ufahamu anadandia train la Kifaransa (TGV) kwa mbele. Nina wasiwasi kama anafahamu maana ya TPN.

Mkuu, kuna wasomi wengine wanaheshimu taaluma zao na wameridhika. Pia kuna wengine hawana kabisa hamu ya kutukanwa na MIJITU inayojipendekeza kwa akina RA na inafanya hivyo kwa sababu hata shule haikupata ya nguvu. Wako tayari kufanya/kufanywa lolote ili muradi washinde ubunge. Watakutukana wewe na usomi wako hadi ujione umekuwa kama Afande wa Msange JKT (Wee kuruta, what is my name......... ??!!!??!)
 
Mkuu Mtsimbe,

Ukiona mtu anaanza kufanya swali la hesabu bila kuweka kwanza data chini (nzuri zaidi kwenye Engineering) basi huyu lazima ufahamu anadandia train la Kifaransa (TGV) kwa mbele. Nina wasiwasi kama anafahamu maana ya TPN.

Mzalendo Sikonge;

Umenichekesha sana mpaka Mamaa anashangaa kulikoni JF . .

Naomba nimwachie mwenyewe atakuja kukujibu.

Pamoja Tunaweza.

NB: Mkuu Umeangalia Movie moja inaitwa INVICTUS? Ni ya babu Madiba alipochaguliwa kuwa Rais wa S.A. na akatumia mchezo wa Rugby kuwaunganisha wasouth. Very inspiring . . .
 
Mzalendo Sikonge;

Umenichekesha sana mpaka Mamaa anashangaa kulikoni JF . .

Naomba nimwachie mwenyewe atakuja kukujibu.

Pamoja Tunaweza.

NB: Mkuu Umeangalia Movie moja inaitwa INVICTUS? Ni ya babu Madiba alipochaguliwa kuwa Rais wa S.A. na akatumia mchezo wa Rugby kuwaunganisha wasouth. Very inspiring . . .

Mtsimbe,

Hii picha sijaiona. Ngoja niingie ONLINE nianze kuisaka.
Unafahamu, miaka ya 90 nilipoenda kufungua macho nchi za watu, tukiwa darasani kwenye somo la hesabu, kijana mmoja wa Kiganda alianza kusolve swali kwa kutumia njia ambayo Profesa wetu alikuwa hajawahi kuiona. Kwanza alimpiga kijana STOP. Baadaye vijana wa Tanzania tukasimama na kusema jamaa yuko sawa. Basi akasolve na mwisho akaweka jibu la kweli. Yule Prof. alishangaa sana na akachukua kikaratasi na ku-copy jinsi jamaa alivyofanya. Akaweka swali jingine na mwingine akafanya kwa kutumia njia hiyohiyo na akatuachaa tuendelee kutumia.

Nafikiri kwa kusema maneno hayo, SI MUHIMU kuangalia mtu anatumia njia gani ila la MUHIMU ni MATOKEO. Hili watu siku zote huwa wanalisahau na kuanza kuvunja watu nguvu kuwa "mnakosea" au "mna lenu jambo".

Nimalize kwa kusema Asante kwa jina la FILM ya INVICTUS.
 
Kwangu naona attack zilizopo zinathibisha ukweli kwamba sio mapenzi ya kila mtu, especially wababaishaji kuona kwamba tunakuwa responsible kwa mambo yanayotuhusu maana wengi ndio wanaponea humo.
TPN na wadau wengine, kuongoza njia sio lelema, msikate tamaa.
Inanikumbusha usemi fulani hivi kwa sisi tuliochezea vishada wakati tunakua kwamba, the kite of success generally rises against the wind of adversity.
 
Mtsimbe,

Hii picha sijaiona. Ngoja niingie ONLINE nianze kuisaka.
Unafahamu, miaka ya 90 nilipoenda kufungua macho nchi za watu, tukiwa darasani kwenye somo la hesabu, kijana mmoja wa Kiganda alianza kusolve swali kwa kutumia njia ambayo Profesa wetu alikuwa hajawahi kuiona. Kwanza alimpiga kijana STOP. Baadaye vijana wa Tanzania tukasimama na kusema jamaa yuko sawa. Basi akasolve na mwisho akaweka jibu la kweli. Yule Prof. alishangaa sana na akachukua kikaratasi na ku-copy jinsi jamaa alivyofanya. Akaweka swali jingine na mwingine akafanya kwa kutumia njia hiyohiyo na akatuachaa tuendelee kutumia.

Nafikiri kwa kusema maneno hayo, SI MUHIMU kuangalia mtu anatumia njia gani ila la MUHIMU ni MATOKEO. Hili watu siku zote huwa wanalisahau na kuanza kuvunja watu nguvu kuwa "mnakosea" au "mna lenu jambo".

Nimalize kwa kusema Asante kwa jina la FILM ya INVICTUS.

Asante sana Mzalendo; nina uhakika sasa tunaongea lugha moja.

Haijalishi sana, hata katika msafara wa Mamba, Kenge watakuwepo . . .

Katika INVICTUS Madiba alitofautiana na blacks kwamba katika SA mpya whites wasipewe nafasi. Alikataa akasema lazima wawepo kwa kuwa the past is the past, and we cant dwell on that, we look for the better future.
 
Kwangu naona attack zilizopo zinathibisha ukweli kwamba sio mapenzi ya kila mtu, especially wababaishaji kuona kwamba tunakuwa responsible kwa mambo yanayotuhusu maana wengi ndio wanaponea humo.

TPN na wadau wengine, kuongoza njia sio lelema, msikate tamaa.
Inanikumbusha usemi fulani hivi kwa sisi tuliochezea vishada wakati tunakua kwamba, the kite of success generally rises against the wind of adversity.


Kamanda Ndahani;

Asante sana. Nimekusoma vema. Maneno yako ni mazito sana na yanatia moyo.
 
Angalizo:

Kuna ambao wameshaanza kutoa vitu kama ndoo; vyombo vya kupikia; nguo; mablanketi; vyandarua nk. Kama ungependa kuchangia vitu vya namna yoyote tafadhali wasiliana na TPN simu namba: 0715 740 047 .
 
Nasikia Nipashe wameandika vizuri sana..

Ni kweli kabisa MKJJ;

Nipashe ya leo katika Jarida la Ndani (Nipashe Jamii) Page number 2 ina makala ya "Makazi" yenye kichwa cha habari "Jamii ichangie waathirika wa mafuriko", imetoa ufafanuzi wa kina sana kuhusu kampeni yetu.
 
Taarifa ya Maendeleo ya Kuchangia Wahanga Wa Mafuriko.




Mtandao Wa Wanataaluma Tanzania (TPN) Kwa kushirikiana na www.issamichuzi.blogspot.com na www.jamiiforums.com na kampuni ya Push Mobile ambayo inatuunganisha na mitandao ya simu ya ZAIN; TIGO na VODACOM imekuwa ikiendesha kampeni ya kusaidia wahanga wa mafuriko yaliyoikumba Tanzania ambayo ilizinduliwa tangu tarehe 12-01-2010 kwa ajili ya familia zaidi ya 8,000 zilizoathirika kwa kukosa makazi, vyakula, na huduma za afya na kupoteza mali nyingi. Misaasa yote itakayopatikana inapelekwa Chama cha Msalaba na Mwezi Mwekundu cha Tanzania ambao wako mstari wa mbele katika kuwasaidia wahanga. Awamu ya kwanza ilikwisha wakilishwa.

TPN na wadau wake inaendelea kuratibu harambee ya kuchangia wahanga wa mafuriko haya kwa kukusanya misaada ya vitu mbalimbali na pesa kwenda kwenye ofisi za Chama cha Msalaba na Mwezi Mwekundu cha Tanzania ambacho kiko mstari wa mbele kuongoza juhudi za kusaidia walioathirika ikishirikiana na taasisi mbalimbali binafsi na vyombo vya serikali. Michango inayopokelewa ni pamoja na fedha na Magodoro, Mahema, Vyandarua, Vyakula (visivyoharibika), Maji safi (masanduku ya chupa za maji), Madawa ya kuzuia maambukizi (ambayo hayajaharibika au kufunguliwa), Vifaa kwa ajili ya matumizi ya kina mama na watoto, Makaratasi ya kujipangusia (clean wipes), nguo, vyakula n.k.

TPN inapenda kuwahakikishia Wanachama na wadau wote waliofanya mawasiliano nasi kuwa TPN haijihusishi na kampeni yoyote mpya zaidi ya ile ya mwanzo iliyoiratibu na wadau wake na inazidi kutoa wito kuwa wote wanaopenda kuchangia wanaweza kufanya hivyo kupitia makato ya kila siku ya muda wa maongezi wa simu za mkononi (Tigo; Zain na Vodacom) kwa Kuchangia Shs 150 kwa siku kwa muda wa siku 30 kwa kutuma SMS yenye neno TPN kwenda 15522. Awali utakatwa Shs 250 kama ada ya kujisajili (Makato yote yanahusisha kodi na gharama za kuunganishwa). Kwa maelezo zaidi wasiliana na 0715 740 047”

TPN na Wadau wake ilikabidhi awamu ya kwanza ya misaada kwa Chama cha Msalaba na Mwezi Mwekundu cha Tanzania iliyokusanywa (haihusishi michango ya SMS) ikiwa ni pamoja na Ndoo za Plastic; Maji; Magodoro; Magodoro; Sembe; Chumvi; Mafuta ya kupikia; Miswaki na dawa za miswaki;Sabuni; Majani ya Chai; Mablanketi na Vyandarua vyote vikiwa na thamani ya TZS 1,381,000. Pia tulikabidhi pesa taslimu TZS 1,068,364.80. Tunawashukuru wote waliotoa. Misaada inayoendelea kukusanywa itakabidhiwa katika awamu ya pili siku ya Ijumaa tarehe 29-01-2010.

Misaada pia inaendelea kupokelewa katika makao makuu ya Chama cha Msalaba na Mwezi Mwekundu cha Tanzania Jijini Dar-es-Salaam Masaki na ofisi zake zote Tanzania. Unaweza pia kuchangia vitu mbalimbali kwa kuvilet ofisi za TPN zilizopo Barabara ya Nyerere; Jengo la TOHS (Dar Group); Ghorofa ya 1 karibu na Radio Tanzania au piga simu namba: 0715 740 047 ili ofisa wa TPN avifuate (utalipia usafiri). Hakuna msaada mdogo au usio na maana na misaada yote itapokelewa.

Pamoja Tunaweza!

Imetolewa na:

Mtandao Wa Wanataaluma Tanzania
(Tanzania Professionals Network)
25-Januari-2010

Bora kama mmewahi kuitaarifu jamii mapema.Je mmesambaza taarifa vya kutosha? Mmetumia mechanism gani kuhakikisha taarifa zinasambaa kwa wingi na kwa haraka?
 
Bora kama mmewahi kuitaarifu jamii mapema.Je mmesambaza taarifa vya kutosha? Mmetumia mechanism gani kuhakikisha taarifa zinasambaa kwa wingi na kwa haraka?

Mkuu; hatuna haja ya kufanya nao mashindano. Wadau wote walioshuhudia hii kampeni wanajua ni nini kinaendelea. Kwa sasa Press Release hii imekuwa posted JF na kwa Michuzi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom