Presidential Delivery Unit - Kitengo kipya chini ya Rais - chatengewa Bilioni 29!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,929
Kumbe muda wote serikali ya CCM inapanga na kutekeleza miradi mbalimbali haikuwa na chombo cha kusimamia miradi hiyo ili kuhakikisha matokeo. Sasa wameamua kuwa ili matokeo ya miradi hiyo yaonekane basi wameamua kuunda chombo kipya ambacho kazi yake itakuwa ni kufuatilia utekelezaji miradi mbalimbali. Sasa najiuliza kama miaka yote hii hawakuwa na vyombo vya kusimamia na kufuatilia miradi hiii walikuwa wanafikiria nini wakati wanaandaa miradi hiyo.

Wenyewe wanaita "Big Results Now"...

Halima Mdee kasema kweli hili ni "chaka la ulaji tu" na kasema yote yanayofanywa na Malaysia siyo lazima na sisi tuige tu kwa 'kucopy na kupaste". Sasa sijui ni wazo la nani hili.

Uchunguzi wangu wa haraka haraka unaonesha kuwa hili ni wazo la wafadhili ambao wanatoa kiasi kikubwa cha fedha; wafadhili wanatoa bilioni 25 na ni vigumu serikali kukataa.

Ilianzia wapi?

Dodoma — TANZANIANS should expect reformed leadership and government in its delivery of development programmes, President Jakaya Kikwete said on Sunday.
The president said this in his closing remarks of a two-day seminar on implementation, monitoring and evaluation framework of National Development Plans and Programmes.
President Kikwete said a team that will evaluate the existing structure will be established and propose an effective delivery unit in the Tanzania context, learning from the Malaysian model.
He has directed all ministries to start setting up and organising their own system of supervision, monitoring and evaluation, as they wait for the national system to be set up by the team.
"The seminar has made a huge difference from the way the government delivers its duties, we have learnt that we need to be focused with clear goals and targets and we already have the Vision 2025.
"We have learnt hat we cannot do everything at the same time," he noted. He said the team will present its report in another government retreat in October, which will kick start the process of adopting and customising the Malaysian Big Fast Results model to suit Tanzanian environment.
"The proposed team will come up with proposals on best way to adopt the Malaysian model so that we can deliver our duties better," he explained. He said 50 years ago, Malaysia was at the same level with Tanzania, but 50 years down the line, Malaysia has made big strides in development.
"The important thing, we have learnt from this is that, we can also make it," he added. President Kikwete expressed gratitude to the Malaysian team that provided the knowledge, noting that they have been generous in sharing the knowledge and experience.
"We have come out of this historic and ground breaking seminar transformed. The public should expect transformed delivery of government responsibilities from now on," he added.
He said the Malaysians took all participants slowly through process of the mechanisms of how to make things happen, analysing issues, and agreeing on how to solve problems, monitoring and evaluation. "It's not rocket science; it's not hard to comprehend. It's simply easy to understand and do. You gave us the ABCs of doing it, I promise we will do it," he stressed.
Reading out the resolutions, the Chief Secretary, Ambassador Ombeni Sefue, said the government commits itself to improve delivery and accountability by emulating the Malaysian model. He said the participants learnt from the experience of Malaysia on framework for implementation monitoring and evaluation of their economic and government transformation programmes to achieve fast results.
He said the way forward a multidisciplinary team drawn from a wide spectrum of stakeholders will be established that will propose and prepare a roadmap for operationalisation of an effective delivery government unit, learning from the Malaysian model.

AllAfrica
 
Kuna fungu la ajabu sana hapa liinaelekea kupitishwa, hili ni fungu la kutumia 29 Billion kwa ajili ya kuanzisha chombo cha ufwatiliaji wa Miradi ya Kitaifa. Chombo hiki kazi kubwa itakuwa ni kufwatilia utekelezaji wa haraka wa miradi ya kitaifa kazi ambayo sasa hiv inafanywa na Tume ya Mipango. Hivi kweli hii hoja ina mashiko na maswahi kwa wananchi??? Hivi kweli sisi shida yetu ni chombo cha kufwatilia miradi???? Hiyo fedha 29 Bilion ingeweza maliza Miradi mingapi ya maana kabisa kwa wananchi???

Kwanini wasijengewe uwezo hao wanaosimamia sasa hvi na wakizembea kwa nini wasiwajibishwe?????Inasikitisha sana. Wananchi hawana maji, hawana madawa, hatuna madawati,walimu wanadai miaka nenda rudi, serikali imepuuza yote haya na inaamua kutenga 29 Bilion kwa matumiz yasiyo ya lazima kabisa. Hili huitaji kufika chuo kikuu ili kuona ni la kipuuzi.

Haya wabunge wa CCM wameshapitisha matumizi ya 29 bilions na hivyo chombo hicho kitaundwa na kutumia ma bilioni hayokwa ajili ya kufwatilia utekelezaji wa Miradi.

Ndugu zangu watanzania, kama hatutajipanga vizur na kuongeza idadi ya wabunge wa upinzani bungeni na kuwatoa CCM madarakani, maendeleo nchin kwetu ni ndoto za alinacha. Shime watanzania tujipange kuingia Bungeni mana kwa kuwaachia Bunge watu wasio na uzalendo ni kujimaliza wenyewe.
 
Bado kuna tume ya Mipango, hii tume inapanga nini?

Halafu vyote chini ya Rais tu?

Naona hela ya kampeni hamna kabisa na Epa haiwezzi fanikiwa tena.

Halafu wamainuka karibu wote kutetea, bila aibu Simbachawene anasema 'ni kwa ajili ya miradi kama bomba la gesi lisimaniwe' really? Siku zote lilikuwa halisimamiwi?

Shame on this govnt kwa kweli.
Hii kitu imeniudhi sana.
 
Suala hapa ni maandalizi ya EPA nyingine tu, kwani kuna chombo cha kufuatilia utekelezaji wa miradi , Tume ya mipango ndio jukumu lake tena kisheria , ukisoma nyaraka zao wanasema kuwa Hii President' s Delivery Bureau inaenda kufanya kazi chini ya Tume ya Mipango, inatengewa bilioni 29 eti za kufuatilia miradi , sasa kama kufuatilia kwa mwaka tunahitaji fedha zote hizo ni za kazi gani ? Huu ni wendawazimu, ama wavunje tume ya mipango , wavunje mamlaka zote zenye jukumu la kufuatilia etc ......nitaweka kambi ya upinzani walisema nini jana. Kwenye hotuba kivuli kuhusu hilo
 
MKJ, hata kama ni wazo la wafadhili, ina maana serikali haiwezi kujitetea hata kidogo.

Hivi mtu atakuja kwako akupe msaada wa vipodozi wakati huna hata unga wa uji?
 
My Signature it say all about CCM, nilishasema na ninasema tena CCM ni Chama cha wahuni na Nchi yetu inaongozwa na Wahuni na sisi tukubali matokeo ya kihunihuni kama yanayotokea sasa serikalini na Bungeni
 
wasambaa tuna msemo wetu ''mfena gemo aweeea kigha''
CCM wanaangalia maslahi yao kwanza.
 
Its crazy jamani
Kwani hakuna wizara husika?

Hata kama wamekataa hoja ya Mnyika but wananchi tumeelewa.

Go mnyika, go Halima!

Hii kitu inakera hasa pale ambapo pale mbunge anapokuwa na hoja ya msingi alafu anashindwa na Ndiyooooo za magamba zisizo na msingi.
 
Malengo yaweza kuwa mazuri, but siyo watekelezaji wawe hawa wanaolindana usiku kucha.
 
This is daylight theft! Whats the use of flash reports? Vote books? Statement of vote? Appropriation acc? National Audit Office? Pay Master General? Accounting Officers? RAS? DAS? RCs? DCs?
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom