President Jakaya Kikwete flies to Addis Ababa..!!!

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797

The Chairman of the African Union Commission (AU) Jean Ping welcomes to Addis Ababa President Jakaya Mrisho Kikwete shortly after he arrived at Bole International airport for a special summit on Ivory Coast Crisis (Photo by Freddy Maro)


There is a communication vacuum and the result is hyped up perceptions that are influencing peoples actions. This is not good at all!It could result in the wrong actions being taken leaving bitterness and anger in its wake.These are two feelings you do not want to contend with as a leader. People need to know the true facts so they can filter the real from the chaff.
 

The Chairman of the African Union Commission (AU) Jean Ping welcomes to Addis Ababa President Jakaya Mrisho Kikwete shortly after he arrived at Bole International airport for a special summit on Ivory Coast Crisis (Photo by Freddy Maro)


There is a communication vacuum and the result is hyped up perceptions that are influencing peoples actions. This is not good at all!It could result in the wrong actions being taken leaving bitterness and anger in its wake.These are two feelings you do not want to contend with as a leader. People need to know the true facts so they can filter the real from the chaff.

hawezi rudi nyumbani mpaka apate mgawo wake wa dowans.

ndo maana aliondoka na mshrika mwenzake (ngeleja) kwenda paris. najua watakuwa wamekutana na RA, brigedia na wadau wote wa dowans.
 
Du Jamaa siku hizi hata haagi, kimya kimya tu mtamkoma, halafu anawahi hata mwenyekiti hajafika, sijui alihonga achaguliwe mjumbe kwenye hii nafasi, anaifanyia kazi hasa. Lakini labda ni dalili ya kwamba kelele za mlango sasa zinamzuia mwenye nyumba kupata usingizi, anaenda kulala kwa Jirani.
 

The Chairman of the African Union Commission (AU) Jean Ping welcomes to Addis Ababa President Jakaya Mrisho Kikwete shortly after he arrived at Bole International airport for a special summit on Ivory Coast Crisis (Photo by Freddy Maro)


There is a communication vacuum and the result is hyped up perceptions that are influencing peoples actions. This is not good at all!It could result in the wrong actions being taken leaving bitterness and anger in its wake.These are two feelings you do not want to contend with as a leader. People need to know the true facts so they can filter the real from the chaff.

utampenda kwenye ishu kama hizo..
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumatano, Machi 9, 2011, anaungana na marais wenzake wa Afrika waliopewa jukumu la kutafuta suluhu ya mgogoro wa kisiasa katika nchi ya Afrika Magharibi ya Ivory Coast, katika hatua za mwisho za jitihada za kujaribu kumaliza mgogoro huo.

Rais Kikwete na marais wenzake wanakutana mjini Addis Ababa, Ethiopia, katika jitihada mpya za kutafuta jawabu la mzozo huo uliolipuka mwishoni mwa mwaka jana kufuatia matokeo ya raundi ya pili ya uchaguzi wa Rais wa nchi hiyo uliofanyika Novemba 28, 2011.

Katika mkutano huo wa siku mbili, marais hao wanatarajiwa kukabidhi ripoti yao kwa Kamati ya Amani na Usalama ya Umoja wa Afrika (AU), ili kuuwezesha Umoja huo kuchukua uamuzi kamili wa jinsi ya kumaliza mgogoro huo.

Ripoti hiyo ni matokeo ya mikutano ya marais hao mjini Addis Ababa, huko Mauritania ambako walikutana mara mbili, na mjini Abidjan, Ivory Coast. Marais hao waliteuliwa na Kikao cha Wakuu wa Nchi Wanachama wa AU katika mkutano wao wa Januari mwaka huu.

Rais Kikwete ameondoka nchini leo asubuhi kwenda Ethiopia kwa kikao hicho cha siku mbili ambako ataungana na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Rais Idriss Deby wa Chad, Rais Blaise Campaore wa Burkina Faso na Rais Mohamed Abdel Aziz ambaye ni mwenyekiti wa kundi hilo.

Wengine wanaotarajiwa kushiriki katika kikao hicho ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) Bwana Jean Ping na wawakilishi wa Jumuia ya Uchumi ya Afrika Magharibi (ECOWAS) na Umoja wa Mataifa (UN).

Mzozo wa Ivory Coast ulianza baada ya taasisi mbili zinazosimamia uchaguzi nchini humo kutangaza matokeo tofauti ya washindi wa raundi hiyo ya pili ya upigaji kura kati ya Mheshimiwa Laurent Gbagbo, aliyekuwa anatetea kiti chake na mpinzani wake mkuu, Mheshimiwa Alassane Quattara.

Tume ya Uchaguzi ya nchi hiyo ilimtangaza Quattara kuwa mshindi wa uchaguzi huo kwa asilimia tisa, lakini siku nne baadaye, Baraza la Katiba la nchi hiyo lilimtangaza Gbagbo kuwa mshindi kwa asilimia moja.

Baraza hilo lilimtangaza Gbagbo mshindi baada ya kuwa limefuta matokeo katika majimbo saba aliyokuwa ameshinda Quattara, kaskazini mwa nchi hiyo ambako ndiko ngome kuu yake ya kisiasa. Kwa kufuta matokeo katika majimbo hayo, Baraza lilimpunguzia Quattara kura 600,000.

Tokea wakati huo, viongozi hao wawili wote wamejitangaza marais na kila mmoja kuunda Serikali yake. Nchi hiyo sasa imetumbukia katika mgogoro kamili wa kisiasa na vita ya wenyewe kwa wenyewe ambako yamekuwepo mauaji ya watu na uharibifu mkubwa wa mali nchini humo.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu

DAR ES SALAAM



09 Machi, 2011
 
bon voyage mr president,ingekuwa vyema kama ungeenda kimya kimya mana safari zako zinakera masikioni mwa wa-tz weng.
 
Mbona Paris alikwenda kimya kimya? au kurugenzi ya mawasiliano ikulu haikuona umhimu wa kutoa taarifa?
 
ndani ya siku 100 kaenda nje mara 5,..piga hesabu kwa miaka 5 atasafiri mara ngapi??tushamzoea na aibu hana huyu jamaa duh!!
 
Hivi ukichaguliwa kwenye kamati huwezi kukataa..? bwana mkubwa punguza safari shughulikia wapiga kura wako kwanza..
 
Kwa wenzetu mtu kama huyo anaitwa Roving Ambassador lakini hapa kwetu tunamwita Mtukufu Raisi, ni tafsiri tu!
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumatano, Machi 9, 2011, anaungana na marais wenzake wa Afrika waliopewa jukumu la kutafuta suluhu ya mgogoro wa kisiasa katika nchi ya Afrika Magharibi ya Ivory Coast, katika hatua za mwisho za jitihada za kujaribu kumaliza mgogoro huo.

Rais Kikwete na marais wenzake wanakutana mjini Addis Ababa, Ethiopia, katika jitihada mpya za kutafuta jawabu la mzozo huo uliolipuka mwishoni mwa mwaka jana kufuatia matokeo ya raundi ya pili ya uchaguzi wa Rais wa nchi hiyo uliofanyika Novemba 28, 2011.

Katika mkutano huo wa siku mbili, marais hao wanatarajiwa kukabidhi ripoti yao kwa Kamati ya Amani na Usalama ya Umoja wa Afrika (AU), ili kuuwezesha Umoja huo kuchukua uamuzi kamili wa jinsi ya kumaliza mgogoro huo.

Ripoti hiyo ni matokeo ya mikutano ya marais hao mjini Addis Ababa, huko Mauritania ambako walikutana mara mbili, na mjini Abidjan, Ivory Coast. Marais hao waliteuliwa na Kikao cha Wakuu wa Nchi Wanachama wa AU katika mkutano wao wa Januari mwaka huu.

Rais Kikwete ameondoka nchini leo asubuhi kwenda Ethiopia kwa kikao hicho cha siku mbili ambako ataungana na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Rais Idriss Deby wa Chad, Rais Blaise Campaore wa Burkina Faso na Rais Mohamed Abdel Aziz ambaye ni mwenyekiti wa kundi hilo.

Wengine wanaotarajiwa kushiriki katika kikao hicho ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) Bwana Jean Ping na wawakilishi wa Jumuia ya Uchumi ya Afrika Magharibi (ECOWAS) na Umoja wa Mataifa (UN).

Mzozo wa Ivory Coast ulianza baada ya taasisi mbili zinazosimamia uchaguzi nchini humo kutangaza matokeo tofauti ya washindi wa raundi hiyo ya pili ya upigaji kura kati ya Mheshimiwa Laurent Gbagbo, aliyekuwa anatetea kiti chake na mpinzani wake mkuu, Mheshimiwa Alassane Quattara.

Tume ya Uchaguzi ya nchi hiyo ilimtangaza Quattara kuwa mshindi wa uchaguzi huo kwa asilimia tisa, lakini siku nne baadaye, Baraza la Katiba la nchi hiyo lilimtangaza Gbagbo kuwa mshindi kwa asilimia moja.

Baraza hilo lilimtangaza Gbagbo mshindi baada ya kuwa limefuta matokeo katika majimbo saba aliyokuwa ameshinda Quattara, kaskazini mwa nchi hiyo ambako ndiko ngome kuu yake ya kisiasa. Kwa kufuta matokeo katika majimbo hayo, Baraza lilimpunguzia Quattara kura 600,000.

Tokea wakati huo, viongozi hao wawili wote wamejitangaza marais na kila mmoja kuunda Serikali yake. Nchi hiyo sasa imetumbukia katika mgogoro kamili wa kisiasa na vita ya wenyewe kwa wenyewe ambako yamekuwepo mauaji ya watu na uharibifu mkubwa wa mali nchini humo.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu

DAR ES SALAAM



09 Machi, 2011
vp kaenda kutalii?
 
Anadhani kuwa yeye bado ni waziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa....
 
Anaogopa kukaa nyumbani kusikiliza matatizo ya wananchi; Ni bora kwenda nje na kula vizuri
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumatano, Machi 9, 2011, anaungana na marais wenzake wa Afrika waliopewa jukumu la kutafuta suluhu ya mgogoro wa kisiasa katika nchi ya Afrika Magharibi ya Ivory Coast, katika hatua za mwisho za jitihada za kujaribu kumaliza mgogoro huo.

Rais Kikwete na marais wenzake wanakutana mjini Addis Ababa, Ethiopia, katika jitihada mpya za kutafuta jawabu la mzozo huo uliolipuka mwishoni mwa mwaka jana kufuatia matokeo ya raundi ya pili ya uchaguzi wa Rais wa nchi hiyo uliofanyika Novemba 28, 2011.

Katika mkutano huo wa siku mbili, marais hao wanatarajiwa kukabidhi ripoti yao kwa Kamati ya Amani na Usalama ya Umoja wa Afrika (AU), ili kuuwezesha Umoja huo kuchukua uamuzi kamili wa jinsi ya kumaliza mgogoro huo.

Ripoti hiyo ni matokeo ya mikutano ya marais hao mjini Addis Ababa, huko Mauritania ambako walikutana mara mbili, na mjini Abidjan, Ivory Coast. Marais hao waliteuliwa na Kikao cha Wakuu wa Nchi Wanachama wa AU katika mkutano wao wa Januari mwaka huu.

Rais Kikwete ameondoka nchini leo asubuhi kwenda Ethiopia kwa kikao hicho cha siku mbili ambako ataungana na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini, Rais Idriss Deby wa Chad, Rais Blaise Campaore wa Burkina Faso na Rais Mohamed Abdel Aziz ambaye ni mwenyekiti wa kundi hilo.

Wengine wanaotarajiwa kushiriki katika kikao hicho ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) Bwana Jean Ping na wawakilishi wa Jumuia ya Uchumi ya Afrika Magharibi (ECOWAS) na Umoja wa Mataifa (UN).

Mzozo wa Ivory Coast ulianza baada ya taasisi mbili zinazosimamia uchaguzi nchini humo kutangaza matokeo tofauti ya washindi wa raundi hiyo ya pili ya upigaji kura kati ya Mheshimiwa Laurent Gbagbo, aliyekuwa anatetea kiti chake na mpinzani wake mkuu, Mheshimiwa Alassane Quattara.

Tume ya Uchaguzi ya nchi hiyo ilimtangaza Quattara kuwa mshindi wa uchaguzi huo kwa asilimia tisa, lakini siku nne baadaye, Baraza la Katiba la nchi hiyo lilimtangaza Gbagbo kuwa mshindi kwa asilimia moja.

Baraza hilo lilimtangaza Gbagbo mshindi baada ya kuwa limefuta matokeo katika majimbo saba aliyokuwa ameshinda Quattara, kaskazini mwa nchi hiyo ambako ndiko ngome kuu yake ya kisiasa. Kwa kufuta matokeo katika majimbo hayo, Baraza lilimpunguzia Quattara kura 600,000.

Tokea wakati huo, viongozi hao wawili wote wamejitangaza marais na kila mmoja kuunda Serikali yake. Nchi hiyo sasa imetumbukia katika mgogoro kamili wa kisiasa na vita ya wenyewe kwa wenyewe ambako yamekuwepo mauaji ya watu na uharibifu mkubwa wa mali nchini humo.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu

DAR ES SALAAM



09 Machi, 2011

Mbona hakutani na wananchi wa Gongo la Mboto na watanzania wengi wasio na umeme?
 
Back
Top Bottom